Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Watu wanasema tunajisahau eti kwakua timu inafanya vibaya saivi ndio tunatoa lawama kwa kocha. Hapana, mimi nimeanza kuonya kuhusu maamuzi na vitendo vya kocha toka msimu uliopita kuna mechi tunashinda kuna mechi tunatoa sare na kuna mechi tunafungwa kihalali kwa kuzidiwa kimbinu.

Mfano mechi na Bayern tunafungwa goli tatu walituzidi kiasi unaona timu imejitahidi ila ubora umeamua. Sasa mechi na Atalanta ni mawenge ya kocha mwenyewe. Kuanzia kupanga kikosi mpaka sub zake, huwezi kuweka mabeki watano na wakati una Santos anaweza kaba pia akasaidia kushambulia.

Yan sisi kila siku ni watu wa kuomba kocha aamke vizuri apange kikosi vizuri na asipate bipolar hapa katikati. Maisha gani haya
 
Na hata ya PSG haikuwa ngumu fainali
Mimi naona timu yeyote ikifungwa fungwa kidogo tu, mashabiki wanapoteana na akili inahama na kusahau mema yote ya nchi. Ni kawaida ya mwanadamu
Chelsea shida zake za msingi zinajulikana
Cole Palmer ni achitech wa mashambulizi hawa wengine wanaigiza tu
Difensi yetu is still "UNDER CONSTRUCTION"
Winga wetu is still "UNDER DEVELOPMENT"
Striker wetu bado wako "UNDER TEST"
Muwe na subiri na aminini PROCESS bado hatujafika nchi ya ahadi, Confernece league na FIFA WC ilikuwa tu ni asali na maziwa njiani
Ila ww jamaa kigeugeu sana aisee 😂
 
Ila ww jamaa kigeugeu sana aisee 😂
Ukigeugeu wangu uko wapi. Ninajaribu tu kama binadamu nisichukuliwe na upepo unavuma ambao saa nyingine hautabiriki. Niliwahi kumchukia Maresca kipindi Cha Dec 2024 hadi March 2025 kwa ajili ya zile press conference zake mbovu na mnazijua. March alibadilika akawa positive na kuwaingizia wachezaji energy na positive mentality ambayo ilionekana kwenye performnace nzuri kwenye mechi 24 mfululiza walishinda 20, dro 2 na defeat 2.
Alituwezesha kututoa kimaso maso mtaani kwa kubeba Conference league na FIFA CWC katikati ya litimu bovu.
Lakini humu ndani kuna watu hawabadiliki hata akibeba UEFA mtawaona tu wanamrushia madongo na mawe.
Kwa sasa naona Marecsa anafanya vizuri, madhaifu aliyonayo hata kama nitamkosoa ni ya kawaida, hata tungelewa PEP, Arteta, Hans Flick au Luiz Enique kwa timu tuliyonayo wangeboronga tu tena si ajabu zaidi ya Maresca
 
Watu wanasema tunajisahau eti kwakua timu inafanya vibaya saivi ndio tunatoa lawama kwa kocha. Hapana, mimi nimeanza kuonya kuhusu maamuzi na vitendo vya kocha toka msimu uliopita kuna mechi tunashinda kuna mechi tunatoa sare na kuna mechi tunafungwa kihalali kwa kuzidiwa kimbinu.

Mfano mechi na Bayern tunafungwa goli tatu walituzidi kiasi unaona timu imejitahidi ila ubora umeamua. Sasa mechi na Atalanta ni mawenge ya kocha mwenyewe. Kuanzia kupanga kikosi mpaka sub zake, huwezi kuweka mabeki watano na wakati una Santos anaweza kaba pia akasaidia kushambulia.

Yan sisi kila siku ni watu wa kuomba kocha aamke vizuri apange kikosi vizuri na asipate bipolar hapa katikati. Maisha gani haya
Haya nmaamuzi ni typical ya PEP, kajifunza huko. The only diference ni wkamba Chelsea bado haina kikosi kilichoshiba.

Hizi tactics ndizo zilizotumika kumtwanga Barcelona na PSG 3-0. Saa nyingine tactics zinafanya kazi na saa nyingine zinabuma. Hii ni kawaida kwenye football.

Kila kocha duniani anayetegemea tactics saa nyingine anapatia na saa nyingine anafeli. Akipatia anaonekana GENIOUS na akifeli anaoneka kocha wa HOVYO kabisa
 
Nilimwambia lembu kuwa team yetu haina sharpness kwenye kushambulia tupo slow sana ndio maana tunashindwa kumudu hizi team za kawaida tunashida kwenye ubunifu ndio maana sometime forward wetu Kama Jaoa Pedro anaonekana kawaida kwa sababu chances hazitenezwi za kutosha inamfanya muda mwingine ashuke chini achukue mipira, Enzo ni mpambanaji lakini hakuna anachooffer mbele uongozi ulizingua kutomsajili Xavi Simons yule jamaa angetusaidia wameenda kumsajili unproven player focundo ambaye hafiti aina ya uchezaji unatakiwa Kama no 10.Mpira ule wa msimu uliopita mpaka tukashika nafasi ya 2 ndio mzuri si huu wa Sasa ambayo tunapata shida kutengeneza nafasi kwa sababu tunawapa muda mpinzani kujipanga kwenye kujilinda
Jana issues sio sharpness, goli la Chelsea lilipatikana kwa sharpness
Issue ya kwanza huyo kocha wa Atalanta (Raffaele Palladino), ni wa special case.

Anatumia mfumo ambao makocha kama Maresca watastrugle tu ukiongeza na mstakes za sub alizofanya Maresca jana.
Pili, Palladino, kocha wa Atalanta, alikuja Cobham (uwanja wa mazoezi wa Chelsea) kujifunza mazoezi ya Chelsea na kupata maarifa ya kimbinu kabla ya mechi yao ya Ligi ya Mabingwa. Hii inaonyesha wao walidhamiria kushinda hii mechi huku sisi tulichukulia business as usual

Tatu, ameiridhi Atalanta ambayo tayari ilishakomaa na ina wachezaji waliocheza pamoja kwa miaka mingi tangu 2014.

Nne, wao walikuwa nyumbani. Saa nyinngine kucheza nyumbani ni sawa na kucheza na mchezaji wa 12 plus energy wanayopewa na mashabiki wao

Kuchangiua hoja yako
Kwanza, kuweka sharpness kwenye hii gemu na akina Gittens, Joao Pedro (anacheza kama retired officer) na Neto yuko kama ana fatique huku Cole Palmer mmiliki ya hiyo foward ameachwa nyumbani unategemea nini?

Pili, Xavi Simon ni wa hovyo bora 3 times Enzo Fernandez. Kwa sasa Enzo anahitaji tu kupumzishwa ili aregain energy
 
Haya nmaamuzi ni typical ya PEP, kajifunza huko. The only diference ni wkamba Chelsea bado haina kikosi kilichoshiba.

Hizi tactics ndizo zilizotumika kumtwanga Barcelona na PSG 3-0. Saa nyingine tactics zinafanya kazi na saa nyingine zinabuma. Hii ni kawaida kwenye football.

Kila kocha duniani anayetegemea tactics saa nyingine anapatia na saa nyingine anafeli. Akipatia anaonekana GENIOUS na akifeli anaoneka kocha wa HOVYO kabisa
Sio kwamba tunazidiwa na mpinzani ni vile aina ya uchezaji wetu, upangajiwa kikosi , sub na makosa binafsi ya wachezaji ndio huwa inatucost ni team chache ndio walituzidi kimbinu we fikiria Tosin ametucost sana na unahitaji ushindi alafu unaenda kumuingiza alafu utegemee matokeo?
 
Sio kwamba tunazidiwa na mpinzani ni vile aina ya uchezaji wetu, upangajiwa kikosi , sub na makosa binafsi ya wachezaji ndio huwa inatucost ni team chache ndio walituzidi kimbinu we fikiria Tosin ametucost sana na unahitaji ushindi alafu unaenda kumuingiza alafu utegemee matokeo?
Wanaomtetea Maresca nikiwemo mimi bado ninaamini Maresca hana wachezaji wanaoendana na mfumo wake. Huyu ni paste and copy ya PEP. Hii ni pamoja na wachezaji walioko Majeruhi kama Cole Palmer na Colwill. Unamuona PEP anapoangaika kama akiwakosa wachezaji wanaoendana na mfumo wake

Mfano Maresca anapenda mawinga wawe na uwezo wa kufanya dribling na kukaa na mpira kama ile style ya Bernado Silva na kuwa mbunifu akiwa na mpira. Hao Chelsea hawapo, Neto hawezi kufanya dribling Garanacho hawezi ni mbio tu ndizo wanazofa.
Mfumo wake unahitaki no. 10 mbunifu na mwenye na uwezo mkubwa wa kutengeneza nafasi. Hiyo anayo Cole Palmer tu, Enzo Fernandez anafuatilia kwa mbali
Mfumo wake unahitaji kiungo au CM playmaker na mkabaji mzuri, tunaye Moises Caicedo anajitahidi ila kwenye playmaking sio mzuri sana. Andrey Santos naye bado anahitaji muda kukua

So cut short the story, Waqchezaji wengi tulionao sio profile kamili ya Maresca. Hapa alipofika amejitahidi na tumpe maua yake
 
Wanaomtetea Maresca nikiwemo mimi bado ninaamini Maresca hana wachezaji wanaoendana na mfumo wake. Huyu ni paste and copy ya PEP. Hii ni pamoja na wachezaji walioko Majeruhi kama Cole Palmer na Colwill. Unamuona PEP anapoangaika kama akiwakosa wachezaji wanaoendana na mfumo wake

Mfano Maresca anapenda mawinga wawe na uwezo wa kufanya dribling na kukaa na mpira kama ile style ya Bernado Silva na kuwa mbunifu akiwa na mpira. Hao Chelsea hawapo, Neto hawezi kufanya dribling Garanacho hawezi ni mbio tu ndizo wanazofa.
Mfumo wake unahitaki no. 10 mbunifu na mwenye na uwezo mkubwa wa kutengeneza nafasi. Hiyo anayo Cole Palmer tu, Enzo Fernandez anafuatilia kwa mbali
Mfumo wake unahitaji kiungo au CM playmaker na mkabaji mzuri, tunaye Moises Caicedo anajitahidi ila kwenye playmaking sio mzuri sana. Andrey Santos naye bado anahitaji muda kukua

So cut short the story, Waqchezaji wengi tulionao sio profile kamili ya Maresca. Hapa alipofika amejitahidi na tumpe maua yake
Mbona Estevao hamchezeshi Sasa maana ni winga mwenye sifa zote zinazohitajika
 
Mbona Estevao hamchezeshi Sasa maana ni winga mwenye sifa zote zinazohitajika
Maresca anataka kumuweka Estevao Willian kwenye low profile
Media na mashabiki wanamsakama sana na wengine kumpa hypes mpaka zile ambazo hazistahili na wengine kumkandia hadi kumtukana na kumbeza. Yote hayo kijana wa umri wa miaka 18 tu kutoka Brazili hajazoea presures kama hizi. Ni low profile peke yake ndio itakayopunguza hizi presure na kumpa nafasi ya kukua. Mimi nakubaliana na Maresca kwa 100% kuhusu namna ya kumhandle Estevao. Apewe game chache na zile tu ambazo atacheza bila presure angalau kwa msimu mmoja ili azoea na media na mashabiki nao waache kumkuzia mambo
 
Yani timu inafanya vibaya wote tunaona ni mistake anazofanya kocha lakini bado kuna watu wanatetea anafanya majaribio kila mechi kama tupo preseason kikosi kila siku kipya wachezaji anachezesha out of position
 
Kuijadili hii THE BLUES chini ya Maresca ni kupoteza muda. Mjinga sana huyu kocha
Hey hey, give me a break
Kama una bad mood kwa sababu ya D9 usitegemee Maresca, Chelsea au Simba itakuondolea hiyo mood yako
Sisi tutasonga mbele hata kama ninyi mtakuwa mmekata tamaa, najua mtakuja tu meli ikitulia kama ilivyokuwa msimu uliopita. Nina uhaklika asilimia 99.99999999999% kwamba jahazi litarudi mahali pake na top 4 tutaingia na UEFA tuenda mbali na hivi vikombe uchwara tutabeba kamoja Mungu akijalia
 
Kuijadili hii THE BLUES chini ya Maresca ni kupoteza muda. Mjinga sana huyu kocha
Maresca sio Mungu, ni binadamu anakosea na hakuna anayepinga,
Najua kabisa kuwa hata yeye anajua amekosea na atajirekebisha.
Mbona ile gemu na Leeds United alikiri kumpanga Tosin badala ya Josh Acheampong ilikuwa ni makosa?
Msimu wake wa kwanza kafanya vizuri na amezidi matarajio. Naamini hata huu msimu atafanya vizuri. Kama kuna sehemu anashindwa ni kwa sababu ya bodi, alilalamika apewe mabeki bodi ikaminya na kumuachia Tosin na Disasi.
Tumkosoe lakini anapostahili maua, tumpe maua yake. Huo ndio UUNGWANA
 
Wanaomtetea Maresca nikiwemo mimi bado ninaamini Maresca hana wachezaji wanaoendana na mfumo wake. Huyu ni paste and copy ya PEP. Hii ni pamoja na wachezaji walioko Majeruhi kama Cole Palmer na Colwill. Unamuona PEP anapoangaika kama akiwakosa wachezaji wanaoendana na mfumo wake

Mfano Maresca anapenda mawinga wawe na uwezo wa kufanya dribling na kukaa na mpira kama ile style ya Bernado Silva na kuwa mbunifu akiwa na mpira. Hao Chelsea hawapo, Neto hawezi kufanya dribling Garanacho hawezi ni mbio tu ndizo wanazofa.
Mfumo wake unahitaki no. 10 mbunifu na mwenye na uwezo mkubwa wa kutengeneza nafasi. Hiyo anayo Cole Palmer tu, Enzo Fernandez anafuatilia kwa mbali
Mfumo wake unahitaji kiungo au CM playmaker na mkabaji mzuri, tunaye Moises Caicedo anajitahidi ila kwenye playmaking sio mzuri sana. Andrey Santos naye bado anahitaji muda kukua

So cut short the story, Waqchezaji wengi tulionao sio profile kamili ya Maresca. Hapa alipofika amejitahidi na tumpe maua yake
Sasa kama kocha hana wachezaji anaowahitaji waachane nae walete kocha atakaeweza kufit kimfumo na wachezaji waliopo
 
Sasa kama kocha hana wachezaji anaowahitaji waachane nae walete kocha atakaeweza kufit kimfumo na wachezaji waliopo
Ni ngumu kumpata kocha atakayefit in kwa wachezaji wa makocha wengine. Na best and cheap way ni kuwaondoa wachezaji wasioendana na yeye ambayo kazi hiyo ilishaanza kitambo ila bado haijamaliziwa
 
1765367771523.png
 
Wachambuzi wikendi ijayo utawasikia wakidai: "Chelsea wanahitaji kusaini golikipa mwingine. Sanchez hatoshelezi." 😂


1765389049134.png
 
🚨🔵 EXCLUSIVE: Kundi la umiliki la Chelsea la BlueCo lashinda mbio za kumsajili kiungo wa kati wa miaka 16 Muhammad Zongo, haya hapa! 🇧🇫

Dili limekamilika kutoka kwa Sporting Cascade FC baada ya kutafutwa kwenye Kombe la Dunia la U17.

Hatua inayofuata itakuwa ni Strasbourg

1765389095304.png
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom