Ili Nicolas Jackson asajiliwe moja kwa moja na Bayern Munich, lazima aanze mechi 40 kabla ya msimu kumalizika.
Uli Hoeneß—mjumbe wa bodi, rais, na mwenyekiti wa bodi ya usimamizi—alisema jana kuwa uwezekano wa mkopo huu kugeuka uhamisho wa kudumu ni mgumu kutokea.
Hoeneß pia alidai kuwa mawakala wa Jackson walilipa €3 milioni ili kufanikisha mkopo huo.
Maoni yangu:
Hizi mbwembwe za Jackson na agent wake kukimbilia Bayern na kuiacha Chelsea—ambapo alikuwa na nafasi ya kuanza mechi nyingi—ni za kushangaza. Kwa hali ilivyo, sidhani kama ataweza kuanza hata mechi 20 kule Bayern, sembuse 40. Atarudi Chelsea tarehe 30 Juni 2026, na kambi aliyoinyea ataikuta inanuka vile vile. Marecsa? Sidhani kama atamkubali tena baada ya zengwe alilolifanya.
Atakuwa kama Ben Chilwell au Raheem Sterling—mchezaji asiyehitajika, akisubiri timu ya kumnunua.
Atakuwa pia kama Kepa aliyepelekwa Real MAdrid kwa mkopo akaanza kuisema Chelsea vibaya na kukandia huku kumbe ni mkopo tu. Alipomaliza mkopo wake Real MAdrid alirudi Chelsea huyo kapigwa mkopo mkopo hadi sasa yuko anapumulia benchi la Arsenal.
Kama Jackson hatapata dakika za kutosha kule Bayern, thamani yake sokoni itaporomoka vibaya. Hata kurudisha
€37 tulizotumia itakuwa ngumu. Tayari €16 za mkopo tunazo bado mil €31
Kwa kifupi: Mkopo huu ni miongoni mwa mikopo ya kipumbavu kuwahi kutokea Chelsea. Na kwa mchezaji na agent kama Diomansy Kamara, ni fedheha ya kiwango cha juu.
View attachment 3467742