Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Ndondo zimeisha karibuni Epl sasa acheni na matakataka mliyokuwa mnacheza nayo.
Ndg ebu jaribu kupambana kwanza na hali yako. Unatokaje kwenda kwa jirani kuzopmea wakati kwako kunateketea? au mmezoez vipigo hadi chumbani kwenu?
 
Gittens hamna kitu, afadhali aliyoingia Estêvão game likaanza kuchangamka.

Palace wamecheza kibingwa sana, wangekuwa wanaingia sana kwenye goli pinzani wangeondoka na point tatu leo mapema sana.
Gittens ameonyesha Uchnga na ugeni kwa EPL. Baada ya muda atakuwa mchezaji mzuri, ndio maana Chelsea wanamsajili Garnacho ili asibebe mzigo mwenyewe
 
Mimi si huwa nawambia hapa? Nikiwambia mchezaji fulani ni takataka muwe mnaelewa, nafuatilia sana michezo na wachezaji.

Narudia tena, hawa wachezaji ni matakataka.

Nicolas Jackson
Christopher Nkunku
Liam Delap
Jamie Gittens
Romeo Lavia
Wesley Fofana
Jorrel Hato
Benoit Badiashile
Axel Disasi
Robert Sanchez
Takata zako ebu weka kwenye ndoo kwanza muda bado. Kumbuka hawa Palace ndio waliwafunga City, Liverpool. Mimi sipimi mechi ya leo kwamba eti wachezaji ni takataka
 
Wazee vip wazee ligi inaanza lini tuwanze kuwala watu vichwaa, unajuwa sisi Chelsea bwana ni noma sanaa
 
Performance ya Chelsea leo kupooza ilitokana na kutokuwepo kwa Colwill na Palace kuwawekea ulinzi shirikishi Caicedo na Enzo. Andrey Santos angeweza kuleta mabadiliko kama angeingizwa kabla ya dakika ya 80. Maresca kwa busara alimtoa Gittens katika dakika ya 54 na angefanya vivyo hivyo kwa Enzo Fernandez kumtoa mapema ili kumuingiza Andrey Santos.
 
Je, Marc Cucurella ni beki wa kushoto au kiungo wa kati wa box-to-box? nauliza hivi kwa sababu leo alikuwa kila mahali, akipress kama mwendawazimu kwenye uwanja. Ikiwa tumepata cleasheet ni kwa sababu ya Cucurella
1755455049222.png
 
Mkuu kama nyeupe sema nyeupe, acha kulea lea ujinga. Chelsea kuna matakataka mengi mno, bila kuyatoa kila msimu itakuwa ni kusindikiza wengine tu.
Sio kwamba kila mchezaji namtetea mbona Madueke nilimkataa kwasababu muda alipewa na akawa anafanya madudu, Kuna wachezaji wanatakiwa wapewe muda ndio uwezo wao utaonekana kwani Mohamed Salah si alichezea Chelsea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom