Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Maresca kuhusu kupata beki mbadala wa Levi Colwill:

"Ni kipaumbele [kuimarisha safu ya ulinzi] kwa sababu Levi ni mchezaji wa kipekee. Kile tulichofanikisha msimu uliopita ni kwa sababu yake. Alicheza mechi zote nami, nampenda sana, tutamkosa.

Ukweli kuhusu mabeki wanaocheza nafasi ya Colwill

Anselmino na Badiashile hawawezi kuchukua nafasi ya Levi Colwill 👟
Ingawa wote ni wachezaji wenye vipaji, bado hawajafikia kiwango cha uthabiti, uelewa wa mchezo, na uwezo wa kushika safu ya ulinzi kama Colwill. Colwill alikuwa na utulivu, uwezo wa kupiga pasi kutoka nyuma, na ujasiri wa kucheza dhidi ya washambuliaji wakali — kitu ambacho Anselmino bado anajifunza, na Badiashile hajathibitisha kwa kiwango cha juu mara kwa mara.

Nini kifanyike?
Sajili beki wa kati mwenye kiwango, au tubaki na waliopo Ikiwa hakuna usajili bora unaopatikana, ni busara kuendelea na waliopo kama Trevoh Chalobah au Sarr (kama atarejeshwa). Lakini kama kuna nafasi ya kuleta mtu wa daraja la juu, basi klabu inapaswa kuchukua hatua.

Futa mkopo wa Mamadou Sarr kutoka Strasbourg
Sarr ni kijana mwenye kipaji kikubwa, na alionyesha uwezo mzuri akiwa Strasbourg. Badala ya kumtoa kwa mkopo, Chelsea inaweza kumweka kikosini na kumpa nafasi ya kukua ndani ya mfumo wa timu.

Tukisajili mpya, chaguo bora ni Murilo, Guehi au Branthwaite
Sababu zangu ni hizi hapa
  • Murilo: Ana kasi, nguvu, na uwezo wa kupiga pasi — amekuwa nguzo muhimu Nottingham Forest.
  • Marc Guehi: Aliwahi kuwa Chelsea, ana uzoefu wa EPL na ni kiongozi mzuri uwanjani.
  • Jarrad Branthwaite: Mchezaji wa Everton mwenye urefu, uwezo wa kuzuia mipira ya juu, na utulivu mkubwa kwa umri wake.
🔥🔵 Wote hawa wana uwezo wa kufikia au hata kuzidi kile Colwill alitoa — kwa hivyo kama Chelsea inataka kuimarisha safu ya ulinzi, ni lazima ichukue hatua sahihi.
Tath

Viwango vya wastani vya WhoScored kwa msimu wa 2024/25
1754704514896.png
 
Ebu tuambie kuhusu mawinga wa msimu huu wa 2025/26 kama endapo Garnacho atajiunga kundini?
1754706085324.png
 
Baba mwenye nyumba "Chelsea FC Thread" hebu watulize watoto wako hao, wanatufanya sote tuonekane akili fupi sababu tu ya kupishana kwa hoja na ni kitu kisichoepukika pia huchangamsha jukwaa letu.
Ebu tuambie kuhusu mawinga wa msimu huu wa 2025/26 kama endapo Garnacho atajiunga kundini?
View attachment 3436393
Ubinadamu ni kazi/The humanity is work.
 
Performances ya academy jana
Acheampong aliyeanzisha build up kutokea golini
Samwel Rack Sakyi aliyejenga buildup
Genesis Antwi (beki RWB) aliyetoa assists ya goli la pili

 
Baba mwenye nyumba "Chelsea FC Thread" hebu watulize watoto wako hao, wanatufanya sote tuonekane akili fupi sababu tu ya kupishana kwa hoja na ni kitu kisichoepukika pia huchangamsha jukwaa letu.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is work.
Nimeshacoment waache, wakiendelea tuwaripoti wapigwe ban kwanza wakirudi watakuwa wameshapoa
 
Ebu tuambie kuhusu mawinga wa msimu huu wa 2025/26 kama endapo Garnacho atajiunga kundini?
View attachment 3436393
Nilisoma comment mahali kwa maana sikuweza kuiona mechi ..comment ilisema estevao William anafaa atokee kulia kama alivyoanza mechi ya Jana Kwasababu kwa huo muda alioffer vitu ambavyo madueke au Pedro neto hawawezi kukupa...hata huyo gittens naye namuona mzuri sana 1v1 si haba
 
Nilisoma comment mahali kwa maana sikuweza kuiona mechi ..comment ilisema estevao William anafaa atokee kulia kama alivyoanza mechi ya Jana Kwasababu kwa huo muda alioffer vitu ambavyo madueke au Pedro neto hawawezi kukupa...hata huyo gittens naye namuona mzuri sana 1v1 si haba
Muache basi kushindana na Mkohoti, kutofautiana hoja haitakiwi ifikie kwenye kutukanana. Mmoja ni lazima abackdown.

Kumhusu Estevão Willian, alimezwa alipohamia katikati — pembeni ana uhuru, anang'ara bila presha 💫. Gittens alithibitisha hype ya watu jana, ana-scan kabla ya kupasi tofauti na Madueke/Sancho⚽. Delap pekee hakuniridhisha jana, wengine wote walicheza vizuri — wenyeji na wageni 🔥 Kongole Chelsea, The blues
 
Maresca kuhusu kupata beki mbadala wa Levi Colwill:

"Ni kipaumbele [kuimarisha safu ya ulinzi] kwa sababu Levi ni mchezaji wa kipekee. Kile tulichofanikisha msimu uliopita ni kwa sababu yake. Alicheza mechi zote nami, nampenda sana, tutamkosa.

Ukweli kuhusu mabeki wanaocheza nafasi ya Colwill

Anselmino na Badiashile hawawezi kuchukua nafasi ya Levi Colwill 👟
Ingawa wote ni wachezaji wenye vipaji, bado hawajafikia kiwango cha uthabiti, uelewa wa mchezo, na uwezo wa kushika safu ya ulinzi kama Colwill. Colwill alikuwa na utulivu, uwezo wa kupiga pasi kutoka nyuma, na ujasiri wa kucheza dhidi ya washambuliaji wakali — kitu ambacho Anselmino bado anajifunza, na Badiashile hajathibitisha kwa kiwango cha juu mara kwa mara.

Nini kifanyike?
Sajili beki wa kati mwenye kiwango, au tubaki na waliopo Ikiwa hakuna usajili bora unaopatikana, ni busara kuendelea na waliopo kama Trevoh Chalobah au Sarr (kama atarejeshwa). Lakini kama kuna nafasi ya kuleta mtu wa daraja la juu, basi klabu inapaswa kuchukua hatua.

Futa mkopo wa Mamadou Sarr kutoka Strasbourg
Sarr ni kijana mwenye kipaji kikubwa, na alionyesha uwezo mzuri akiwa Strasbourg. Badala ya kumtoa kwa mkopo, Chelsea inaweza kumweka kikosini na kumpa nafasi ya kukua ndani ya mfumo wa timu.

Tukisajili mpya, chaguo bora ni Murilo, Guehi au Branthwaite
Sababu zangu ni hizi hapa
  • Murilo: Ana kasi, nguvu, na uwezo wa kupiga pasi — amekuwa nguzo muhimu Nottingham Forest.
  • Marc Guehi: Aliwahi kuwa Chelsea, ana uzoefu wa EPL na ni kiongozi mzuri uwanjani.
  • Jarrad Branthwaite: Mchezaji wa Everton mwenye urefu, uwezo wa kuzuia mipira ya juu, na utulivu mkubwa kwa umri wake.
🔥🔵 Wote hawa wana uwezo wa kufikia au hata kuzidi kile Colwill alitoa — kwa hivyo kama Chelsea inataka kuimarisha safu ya ulinzi, ni lazima ichukue hatua sahihi.
Tath

Viwango vya wastani vya WhoScored kwa msimu wa 2024/25
View attachment 3436391
Ndio ninaona hakuna umuhimu wowote wakumsajili Garnacho Kama tukimsajili Xavi Simons badala yake tuongeze beki mmoja ili tu balance vitabu vyetu vizuri
 
Unajua wewe mtoto ni maku sana,mkishawashwa miqundu mnatafuta wa kuwakuna,Kaangalie huko livescore utuscreen shotie then utiwekee hapa kama wameonyesha chochote.
Mkuu wanasema samehe mara 7 mara 70. Potezea inapotokea mtu kukukwanza haya maneno si mazunri kwa watu wanaishi nyumba moja hata kama ni wa mpinzani.
 
Ndio ninaona hakuna umuhimu wowote wakumsajili Garnacho Kama tukimsajili Xavi Simons badala yake tuongeze beki mmoja ili tu balance vitabu vyetu vizuri
Bado wewe hujaelewa. Wamiliki wa Chelsea wanasajili kwa malengo mawili, ninyi mashabiki mnang'ang'ana na mchezaji anayeweza kucheza uwanjani tu ila kwenye market opportunity hamuangalii.
Malengo ya usajili
  1. Kuwa na pool ya kutosha ili kocha achague wa kwake wanaofit kwenye mfumo
  2. Wanaobaki wauze kama wana faida au watolewe mkopo ili wakaimarike wauzwe kwa faida
Garnacho aklija akafanya vizuri watabaki kupena rotation na ushindani na Gittens. Akishindwa kufitin atauzwa kwa faida na ndio maan wamiliki hawtaki kumnunua kwa mahela mengi. Market opportunity.

Timu hadi sasa imesukwa vizuri na bado hamuwaamini scout, SD na wamiliki?

Kwa approach hii naiona Chelsea ikimudu kuwa na nguvu ya pesa ya kusajili wakati wowote na pia kuwa na timu imara yenye kuweza kushindana kwenye ligi zote

Kudos Wamiliki
Kudos SDs
Kudos Maresca
Chemistry imematch
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom