Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC imeripotiwa kuamua kuwaita baadhi ya wachezaji wake kutoka likizo kutokana na wasiwasi unaoongezeka kuhusu hali yao ya akili baada ya msimu mkali. Uamuzi huu unakuja kufuatia picha na taarifa za kushangaza zinazoonyesha wachezaji wakijihusisha na tabia za ajabu na hatarishi wakati wa mapumziko yao.

Kuanzia kuruka angani na ndege, kuingiliana na simba na chatu, hadi kushindana na pomboo na kufanya mizunguko angani, tabia hizi zimezusha taharuki ndani ya klabu. Vyanzo vinasema baadhi ya mashabiki na hata viongozi wa juu wa klabu walilazwa hospitalini baada ya kushuhudia matukio hayo ya kushtua.
View attachment 3419025View attachment 3419028View attachment 3419029
Hii taarifa imenichekesha 😂
 
Huwezi kumlinganisha Chalobah na top defenders la sivyo timu kubwa kubwa zingemfukuzia hasa wakati na wakati huu Chelsea ina mpango wa kumuuza tena wangekuwa Tayari kumnunua kwa zaidi ya pauni milioni 60 au 70.

Chalobah hawezi kuwania mipira ya juu kwenye presha kubwa kama Colwill anavyofanya
Chalobah anakuwa na maamuzi hatarishi wakati wa presha kubwa
Chalobah sio mzuri sana kwenye kufanya interceptions
Pia sio mzuri kwenye kuusoma mchezo kama mabekli wakubwa wanavyofanya
Chalobah hawezi kucheza vizuri kwa kutumia mguu wake wa kushoto
Hivi vitu ndivyo vinamuangusha na kocha asimuweke kwenye mahesabu yake
Japokuwa hauzwi kwa kutupa ila kwenye peking order Chalobah yuko nyuma ya Fofana na Tosin na ndio sababu kubwa ya kuuzwa. Maresca anapenda kuwatumia zaidi Fofana na Tosin zaidi yake
Ipi sababu ya chalobah kurudishwa?
Kwahy hy sababu imeshaisha?
 
Huwezi kumlinganisha Chalobah na top defenders la sivyo timu kubwa kubwa zingemfukuzia hasa wakati na wakati huu Chelsea ina mpango wa kumuuza tena wangekuwa Tayari kumnunua kwa zaidi ya pauni milioni 60 au 70.

Chalobah hawezi kuwania mipira ya juu kwenye presha kubwa kama Colwill anavyofanya
Chalobah anakuwa na maamuzi hatarishi wakati wa presha kubwa
Chalobah sio mzuri sana kwenye kufanya interceptions
Pia sio mzuri kwenye kuusoma mchezo kama mabekli wakubwa wanavyofanya
Chalobah hawezi kucheza vizuri kwa kutumia mguu wake wa kushoto
Hivi vitu ndivyo vinamuangusha na kocha asimuweke kwenye mahesabu yake
Japokuwa hauzwi kwa kutupa ila kwenye peking order Chalobah yuko nyuma ya Fofana na Tosin na ndio sababu kubwa ya kuuzwa. Maresca anapenda kuwatumia zaidi Fofana na Tosin zaidi yake
Mbona nusu fainal na fainal amecheza chalobah na sio Tosin
 
kwani ukiwa likizo kuna shughuli hutakiwi kuyafanya kama hayavunji sheria? japo sijaelewa hapo uliposema viongozi na mashabiki kulazwa hospitali, ni baada ya kushudia yanayotendwa na wachezaji wa Chelsea wakiwa mapumzikoni?
🤣🤣
 
Ipi sababu ya chalobah kurudishwa?
Kwahy hy sababu imeshaisha?
Chelsea ilishindwa kusajili wachezaji January na majerruhi ya Wesley Fofana and Benoît Badiashile ndio miliyolazimu management kuita kuja kuziba nafasi ya Wesley Fofana and Benoît Badiashile
Hao wachezaji wawili na usajili wa Mamadou Sar aliyerudi mkopo Strasbourg inatosha kabisa kusikiliza ofa nzuri kama Chalobah atakuwa na suitors wa kutoie pesa nono. Wakikosekanma Chalobaha atabaki kikosini kutekeleza majukumu yake kama mchezaji wa Chelsea
 
Uza Fofana na Disasi ,after all tuna Lundo la mabeki leta yule dogo Muargentina ,atacheza na akina Colwill ,Tosin , Chalobah na hata Badiashile kama atakuwepo kama center backs inatosha sana hii idadi
 
Yaani uuze kitasa Chalobah ubakize galasa Disasi na mgonjwa wa kudumu Fofana ,aisee utakuwa na ugonjwa wa akili .
Chalobah tusiwe wanafiki kaimprove sana , si Chalobah yule wa zamani , sometimes wachezaji wanahitaji kupewa muda
Nakubaliana na ww Chalobah kaemprove sana.
Fofana ni wa kuuza anakula mshahara bure tu. Kama hamna mteja tuwape hata Arsenal bure kama asante yetu.
 
Lavia
Fofana
Jackson
Hall
Tosin
Sterling
Felix
Disasi
ndg acha mhemko
Fofana, Lavia na Jackson ni wachezaji wazuri sana
Jackson kama atauzwa ni kwa sababu ya sajili mpya ya Delap na Pedro ila hatauzwa bei chee, hii nakuhakikishia
Jackson akiunlock clinbicality kwenye neti atakuwa ni striker wa 100+ fee
Lavia na Fofana wanapatiwa dawa ya majeruhi msimu ujao kama ilivyokuwa kwa James
Hall ni squad playuer mzuri, karidhika kuwa backup na akiingizwa anacheza vizuri na kwa kujitoa
 
Wewe kwa kutetea matakataka uko vizuri, Fofana ni lini amekiwasha?
Wewe na wewe unashida, kila mtu anamjua Fofana alivyo mzuri
Wamiliki, SDs, kocha, bencji la ufundi wachezaji wenzake na kundi kubwa la mashabiki. Ni wewe tu unamuona taklataka, hapo ndio shida yako inaanzia.

Mazuri ya Wesley Fofana (Anapokuwa Fiti)
  • Ana kasi kubwa ya ball Recovery: Fofana ana mwendo wa ajabu, huweza kufunika maeneo kwa haraka na kufanya tackle za dharura dhidi ya washambuliaji wa kasi.
  • Beki Mpeleka mipira mbele: Ana ujasiri wa kusukuma mpira mbele kutoka safu ya ulinzi kwenda mashambulizi—ni nadra kwa mabeki wa kati.
  • Nguvu Angani: Ni imara kwa mipira ya juu, akitamba kwa kuondoa hatari na pia kutishia goli wakati wa mipira ya adhabu.
  • Utulivu kwenye presha kubwa: Hutulia akiwa na mpira, haogopi hata akibanwa—ni wa msaada mkubwa katika ujenzi wa mashambulizi kutoka nyuma.
  • Uwezo wa Kubadilika: Anaweza kucheza kama sehemu ya safu ya mabeki watatu au wanne, na mara chache kama beki wa kulia.
  • Uongozi: Licha ya umri wake mdogo, anaonesha ukomavu na uwezo wa kuongoza—anaweza kuwa mhimili wa ulinzi baadaye.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom