Sikuona mchezo wowote mzuri wa PSG jana, wanaonekana wazuri kwa sababu wale wapuuzi wa Real Madrid hawakucheza kama vile walikuwa kwenye mgomo.
Nilitazama hadi dakika ya 70 nikaenda kulala, kwani mchezo ulikuwa wa kuchosha kutokana na Real Madrid kutokuwa na ari ya kushindana.
PSG walitumia vyema mapengo, mapenyo na makosa ya Real Madrid,
Walicheza mpira na mabeki, wakivunja safu za ulinzi, na kufunga mabao rahisi.
Ilikuwa kama marudio ya kichapo cha kihistoria cha Ujerumani dhidi ya Brazil kwenye Kombe la Dunia mwaka 2014.
Kama Liam Delap, Joao Pedro na Pedro Neto wakicheza kule mbele wakawapress hao mabeki wa PSG ili wasipasiane wenyewe kwa wenmyewe tita wa botafogo nakuambia
Tusubiri jumapili tuone na tumuombee Maresca aone kama nilivyoona mimi na kuiandaa timu kwa kuwapress hao mabeki