Nimeona watu wengi Wana criticize Chelsea kutaka kumsajili Joao Pedro wanaona hana namba kubwa ya magoal nataka niwaambie kitu, Kuna wachezaji huwezi kuwahukumu kwa namba ila unatakiwa uwaangalie kwenye game Joao Pedro ndio mchezaji wa aina hiyo. Ukimuangalia mtu Kama Diego costa au Aguero hata Kama ni mara yako ya Kwanza unajua huyu ni striker kutokana na namna wanavyocheza huwa hawakai mbali na goal ila kwa Joao Pedro ni tofauti anaweza akawa amepangwa namba 9 ila ukaangalia uchezaji wake huwezi kujua ni namba tisa kwasababu hatulii kwenye eneo moja utamkuta mara Lw, advance midfielder au RW anashuka mpaka chini, work rate yake ni kubwa uwanjani, ana skills,ana Kasi, good passer na scoring mzuri huwa ana athiri mchezo mzima ana fanya vitu vitokee. Akija Chelsea tutakuwa tumepata mchezaji mzuri mwenye ubunifu hii itasaidia kutomtegemea sana Cole Palmer kwenye kutengeneza nafasi hata kwenye kufunga pia.Jamaa ni kiraka anaweza kucheza nafasi za mbele tofauti Kama namba 9, no 10,7 na 11 watu hawatakiwi kumjudge kwa namba.kiasi fulani nimeanza kuwaamini body yetu ya usajili Wana jicho la mbali