Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Dah !Alhamdulilah bora tumerudi UEFA ,Chelsea si ya kucheza ligi za mchangani aisee .Ilikuwa ni dharau kibonde arsenyani anacheza UEFA halafu Champion kama Chelsea anacheza conference , hii ilikuwa ni fedheha
Big up kwa boys , wakaze msimu ujao tugombanie ubingwa ,msimu huu kuna muda walikata moto ,tukawa tunapata matokeo ya ovyo ila tulianza vizuri sana
Alaaah ligi imekweishaa mkuu?? Nimeona juukwaa la manjesta city kuwa ligi imeshaisha na Sasa sisi tunaenda kuwa mabingwa wa uefa na Europe na epl yani ni mwendo wa ndoo Tatu msimu ujao hahahaha hahaha
 
Dah !Alhamdulilah bora tumerudi UEFA ,Chelsea si ya kucheza ligi za mchangani aisee .Ilikuwa ni dharau kibonde arsenyani anacheza UEFA halafu Champion kama Chelsea anacheza conference , hii ilikuwa ni fedheha
Big up kwa boys , wakaze msimu ujao tugombanie ubingwa ,msimu huu kuna muda walikata moto ,tukawa tunapata matokeo ya ovyo ila tulianza vizuri sana
Boehly na Eghbali walivyofurahi leo naona tutasajili sasa wachezaji wa kuongezea ili mwakani tubebe na UCl kabla ya Arsenal
 
Levi Colwill juu ya kupata kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa:

"Tumerudi pale tunapopaswa kuwa. Vijana wanapata kujithibitisha. Kila mtu amekuwa akizungumza mengi kuhusu sisi, lakini tumefanya."
Jamaa anaongea kwa authority ni Kama vile ni captain
 
  • Thanks
Reactions: K11
Kama kocha ni huyu huyu mwanafunz wa Pep, hatuwezi kuachieve chochote. Wanafunz wa Pep wote ni viazi.
Shida ni kwamba hakuna kocha proven winner anayezagaa bila timu hivyo naona tukiendelea na upside down hizi msimu ujao
 
Kama kocha ni huyu huyu mwanafunz wa Pep, hatuwezi kuachieve chochote. Wanafunz wa Pep wote ni viazi.
Tuna sababu ya kushangilia na wala hatutakuwa kama Arsenal. Tutabeba Conference na mwakani lazima tutashinda makombe zaidi. Uzuri mmoja Maresca ameshajua mahsabiki wa Chelsea wanataka nini. Zile hotuba zake za kijinga za Novemba hadi Feb kaziacha
 
Tuna sababu ya kushangilia na wala hatutakuwa kama Arsenal. Tutabeba Conference na mwakani lazima tutashinda makombe zaidi. Uzuri mmoja Maresca ameshajua mahsabiki wa Chelsea wanataka nini. Zile hotuba zake za kijinga za Novemba hadi Feb kaziacha
Ni kweli siku hizi amejifunza sana kabadilika kwenye kauli lakini kwenye selection watu wamecritise sana kwenye hili
 
  • Thanks
Reactions: K11
Shida ni kwamba hakuna kocha proven winner anayezagaa bila timu hivyo naona tukiendelea na upside down hizi msimu ujao
Tatizo sio kocha anayezagaa, wakati wamiliki wanatafuta kocha, Hans Flick alikuwa huru, Luis Enrique alikuwa huru. Profile ya kocha wanayemtaka ni Maresca hata tulie namna gani hawatambadilisha labda aboronge sana. Tena sasa ameipeleka timu Klabu bingwa ataongezewa miaka 10
 
  • Thanks
Reactions: K11
Reece James:

"Tunazungumza juu ya kuwa mchezaji mwenza bora na kila mtu alionyesha hilo. Watu wengi kabla ya msimu, wakati wa msimu walikuwa na kutoamini - walituambia 'tulikuwa vijana wachanga, hatuna uzoefu na hatungefanikiwa'.
Lakini tuko hapa..."
 
Katika mechi sita za mwisho, tumefungwa moja tena nadhani kwa sababu ya ujinga alioufanya Jackson na zingine tano zote tumeshinda
Points 18 tukaweka kambani 15 na kumaliza ligi kwa kishindo
Mpe Maresca maua yake hata kama badio humpendi

1748269199591.png
 
Kwa mabilioni tuliyotumia kuwekeza kununua wachezaji lori 6 na nafasi tuliyomaliza EPL haviendani. Kiuchumi tunaendelea kupata hasara
 
Kwa mabilioni tuliyotumia kuwekeza kununua wachezaji lori 6 na nafasi tuliyomaliza EPL haviendani. Kiuchumi tunaendelea kupata hasara
Halafu wanashangilia kama wamebeba ubingwa vile? Yaani tabia za Arsenal kabisa hizi za kushangilia nafasi ya 4, Yaani hata liva waliobeba ubingwa hawajashangilia Hivyo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom