Cash Money Forever
JF-Expert Member
- Mar 16, 2019
- 721
- 1,316
Timu inaweza kuwa na washambuliaji wachache ila wanaelewana, wanasomana na kucheza kwenye ubora mkubwa sana kupelekea kufunga magoli mengi.Mchezo dhidi ya Palace nilipata wasaa wa kuutazama nami nitie neno kidogo kutokana na nilicho kiona.
Thamani ya Enzo sijawahi kuiona toka amenunuliwa, ni mchezaji alie nunuliwa kwa pesa nyingi sana lakini uwanjani anacheza ugoro. Pasi anazo piga kwenda kwa wenzake ni upumbavu mtupu, eti nae ni kiungo, inasikitisha sana.
Sijawahi kumuelewa Jackson pindi anapo kuwa anakokota mpira anakuwa wazi kutoa pasi kwa mwenzake lakini hafanyi hivyo mpaka anapokonywa mpira. Jamaa ana upumbavu mwingi mwingi tu.
Mpaka sasa bado najiuliza huyu kocha kilaza tulie nae aliona nini cha maana kwa Sanchez ambacho Petrovic hana.
Na timu inaweza kuwa na lundo la washambuliaji ila wakacheza ili mradi ndio haya tunashuhudia THE BLUES sehemu ya kuachia pasi kutoa fursa kwa mwingine kwenye nafasi nzuri zaidi ya kufunga unakuta mchezaji anang'ang'ania kukokota tuu wakati uwezo wake kwenye kufanya maamuzi na finishing ni mdogo
Tujifunze kwa city washambuliaji hawalazimishi kucheza vitu ambavyo haviwezekani. Wanarahisisha uchezaji na ufungaji wa magoli kwa kutoa pass kwa mchezaji ambaye yupo kwenye nafasi kubwa zaidi ya kufunga.
