Kikosi cha kwanza cha Chelsea kinajivunia kuwa na wachezaji wengi wenye vipaji, na zaidi ya 90% ya wachezaji wanaweza kucheza nafasi zaidi ya moja uwanjani. Wachezaji pekee ambao yumkini wanacheza nafasi moja tu ni Madueke, Tosin, na walinda mlango. Ukiondoa hao, waliobaki wanaweza kucheza zaidi ya nafasi moja na huo wasifu ndio kocha anataka. Kwa hivyo, majerahi yakitokea, kuna uwezekano wa kutoathiri kikosi kwa kiasi kikubwa kama ilivyokuwa msimu uliopita. Wakiwa uwanjani, utashuhudia wachezaji wakicheza kila mahali uwanjani, mara nyingi kwa kubadilishana. Kwa mfano, Cucurella anaweza kujikuta akicheza jukumu ambalo kwa kawaida linashikiliwa na Enzo, huku Enzo akiingia kwenye nafasi ya Cucurella; vivyo hivyo, Gusto na Caicedo watabadilisha majukumu bila shida, na Nkunku anaweza kucheza winga ya kulia huku Palmer akihama kwenda kushoto. Ni muhimu kwa kocha kuingiza hali ya nidhamu kwa wachezaji wakati wa kubadilishana nafasi kati ya wachezaji ili balance ya timu isipotee; kwa mfano, Enzo akienda kwenye mrengo wa kushoto, Cucurella anapaswa kusogea ili kujaza nafasi ambayo Enzo anaacha nyuma ili kudumisha balance kwenye kiungo, na kanuni hii inapaswa kutumika katika nafasi zote ili kuhakikisha balance katika inakuwepo na hivyo kuepuka kushambuliwa kwa kushtukiza.