Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Hivi kwa nn Ngolo Kante aliuzwa? Dah. Namuona hapa france anakichafua kama ndio kwanza ana miaka 22
Kesi ya Kante kutopata majeruhi kule kwenye Saudi Pro League inaonyesha kuwa makocha waliokuwa wanaifundisha Chelsea wakati wa Kante ndio waliokuwa wanasababisha majeruhi kwa sehemu kubwa. Ndiyo!

Tuliaminishwa injury Chelsea haziepukiki, kumbe hawa makocha ndio wanasababisha hayo majeruhi
Pochettino watu walikuwa wanamtetea kuwa hasababishi majeruhi. Mimi nasema makocha wanayo sehemu kubwa sana kwenye kusababisha majeruhi. Na watu wasiseme mbona huko nyuma kulikuwa hivyo hivyo. Nasema hata nao walikuwa ndio sababu ya majeruhi. Mbona Kipara hana majeruhi ya kijinga jinga hivyo

Natamani Enzo Maresca asiwe ndie chanzo cha majeruhi ili wachezaji kama Nkunku, Fofana, Chilwell tuweze kuwafaidi
 
Kukosekana kwa majeraha kwa Kante kwenye Ligi ya Saudia Pro League kunatoa mwanga juu ya athari za makocha kwenye majeraha ya wachezaji huko Chelsea.

Inadhihirika sasa kuwa majeraha yaliyodhaniwa haziepukiki yalikuwa yanasababishwa na makocha. Dhana ya kwamba Pochettino hakukusababisha majeraha inaonekana sasa kuwa sio kweli kwani makocha wanachangia pakubwa katika majeraha yasiyo ya lazima.

Mfumo huu wa makocha katika mazoezi kwamba yanachangia majeraha ni kweli si tu kwa sasa bali hata kwa siku za nyuma.

Kutokuwepo kwa majeraha ya kipuuzi chini ya uongozi wa PEP Guardiola kunadhihirisha huu ukweli na inahalalisha kile ninachobainisha hapa.

Natamani sana, Enzo Maresca [kocha wetu mpya] hataleta majeraha ya kijinga kama ilivyokuwa huko nyuma ili kuruhusu wachezaji kama James, Nkunku, Fofana, na Chilwell wawe bora na kuirejesha Chelsea mahali inapostahili.

1718684956837.png
 
Goli la ajabu sana hili, what a Right Winger? Ana uwezo wa kunyang'anya mipira, kudrible na kufunga. Natamani aje haraka Chelsea yeye na Kendry Paez tutakuwa na jambo msimu kuanzia 2025/26
 
Leo ratiba ya ligi inatolewa

Kwa miaka ya hivi karibuni tumekuwa tukifungua league dhid ya top6 sitoshangaa na safari hii tukifungua nao tena
Chelsea, tunaanza na Man City mechi yetu ya kwanza pale Stanford Bridge
Last season tulianza na Liverpool
Hivi EPL wanatuonaje?
 
Umejuaje wakati ratiba kamili inatoka saa 5 asubuhi, acha urongo.
Chelsea, tunaanza na Man City mechi yetu ya kwanza pale Stanford Bridge
Last season tulianza na Liverpool
Hivi EPL wanatuonaje?
 
Krisimasi wametupa uji wa mgonjwa
Chelsea’s Matches on Christmas period
4/12/24 Southampton (A)
7/12/24 Tottenham (A)
14/12/24 Brentford (H)
21/12/24 Everton (A)
26/12/24 Fulham (H)
29/12/24 Ipswich (A)
 
Match Day 1 Bado mnajitafuta City atawaua nawaonea huruma, Nawashauri Msiingize Timu uwanjani.
 
Goli la ajabu sana hili, what a Right Winger? Ana uwezo wa kunyang'anya mipira, kudrible na kufunga. Natamani aje haraka Chelsea yeye na Kendry Paez tutakuwa na jambo msimu kuanzia 2025/26
View attachment 3019791
Kitu ambacho kinanishangaza kuhusu project yetu tunamsajili huyu wakati hapo hapo tunamtaka olise wote wanacheza nafasi moja kumbuka pia tuna Madueke hii imekaaje
 
Mbona kama mechi nyingi zinachezwa kwa siku moja yn sio kama vile mechi mpaka siku za katikati ya wiki?
 
Kitu ambacho kinanishangaza kuhusu project yetu tunamsajili huyu wakati hapo hapo tunamtaka olise wote wanacheza nafasi moja kumbuka pia tuna Madueke hii imekaaje
Wide players wana uwezo wa kucheza sehemu nyingi za mbele ikiwemo LW na RW, na Na. 10
Kumbuka pia sio kila mchezaji akija anaendelea kuwa kwenye form. Ziyech alikuwa moto sana kule Ajax, kaja hapa kaflop, tatu kunyatia vipaji ni gamble ambayo ikikubali timu itakuwa na advantage. Mfano Estevao na Paez wanaweza kuja kuwa akina Messi na aidha abaki au auzwe tutafaidi kama timu. Pia kumbuka Hao akina Paez na Estevao ni product ambazo bado hazijaiva, kuwafaidi sana sana hadi watimize 20 or above ambayo itakuwa ni 2028+
 
Tena Chelsea inahusishwa na mchezaji mweusi na mwenye nguvu. Samu Omorodion ana miaka 20 na urefu mita 1.93.

Atlético Madrid wamekataa leo ofa rasmi kutoka kwa Chelsea kwa Samu Omorodion ya takriban €30m pamoja na kifurushi cha addons ya €10m hadi €40m.

Chelsea wanaendelea kuwafikiria Omorodion na Jhon Durán kama chaguo la mshambuliaji mpya.

Atlético Madrid wanasisitiza juu ya mpango wao wa kumbakisha Samu Omorodion.

@FabrizioRomano

1718735936738.png
 
Kendry Páez amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Liga Pro Serie A (Hatua ya Kwanza) akiwa na miaka 17 tu

1718745107547.png
 
Kukosekana kwa majeraha kwa Kante kwenye Ligi ya Saudia Pro League kunatoa mwanga juu ya athari za makocha kwenye majeraha ya wachezaji huko Chelsea.

Inadhihirika sasa kuwa majeraha yaliyodhaniwa haziepukiki yalikuwa yanasababishwa na makocha. Dhana ya kwamba Pochettino hakukusababisha majeraha inaonekana sasa kuwa sio kweli kwani makocha wanachangia pakubwa katika majeraha yasiyo ya lazima.

Mfumo huu wa makocha katika mazoezi kwamba yanachangia majeraha ni kweli si tu kwa sasa bali hata kwa siku za nyuma.

Kutokuwepo kwa majeraha ya kipuuzi chini ya uongozi wa PEP Guardiola kunadhihirisha huu ukweli na inahalalisha kile ninachobainisha hapa.

Natamani sana, Enzo Maresca [kocha wetu mpya] hataleta majeraha ya kijinga kama ilivyokuwa huko nyuma ili kuruhusu wachezaji kama James, Nkunku, Fofana, na Chilwell wawe bora na kuirejesha Chelsea mahali inapostahili.

View attachment 3019773

Una uhakika?, kocha ana sababishaje injury kwa mchezaj?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom