UEFA imewapa Manchester United hadi Jumatatu kutafuta suluhu kuhusu ushiriki wao wa Ligi ya EUROPA msimu ujao.
Muda huu umewekwa kutokana na mgongano wa kimaslahi unaotokana na ukweli kwamba mmiliki mwenza wa United, Sir Jam Ratcliffe, pia anamiliki klabu ya Nice, ambayo imefuzu kwa mashindano hayo.
Kulingana na kanuni za UEFA, chombo kimoja hakiwezi kuwa na ushawishi mkubwa kwa vilabu viwili au zaidi vinavyoshiriki katika ligi moja.
Ikizingatiwa kuwa Nice walimaliza ligi wakiwa juu zaidi kuliko United, Mashetani Wekundu wanaweza kuhitajika kushuka hadi Ligi ya Conference ya Europa isipokuja na azimio la kutoa suluhisho.
View attachment 3004818