Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

😂😂😂

🤣🤣🤣

Najua lugha tunayoongea ni moja ila inapindishwa tu maana. Kidogo kidogo tunaelewana

BTW hongereni wote kwa ushindi japo hatuja hama nafasi.
Mkuu me siku zote sijawah sema tunashida ya wachezaji tofauti ya wewe na Cash Money
Huwa nasema tunawqchezaji wazuri ila wamekosa mwalim wa kuwaongoza na kuwaimprove

Nyie ndio mnaoamini tunawachezaj wa hovyo
 
Jim White wakati wa mchezo wa Chelsea dhidi ya New Castle:
"Kila mara Raheem Sterling akijaribu kupiga mpira golini alipokelewa na kundi la mashabiki wa Newcastle wakiimba kwa kumwambia Southgate alikuwa sahihi kumwacha kutoka timu ya taifa ya Uingereza. Ninafafanua. Ukosoaji wao ni wa maana zaidi."

Kwa maoni yangu
Katika mechi ya jana Sterling aligusa mpira mara 13 ambayo ni ndogo kuliko wachezaji wote kwenye timu
zote mbili na bado kocha ataendelea kumpa acheze mechi nyingi nyuma ya Mudryk

Jana Sougth gate alikuwa uwanjani kuwafuatilia hao wachezaji wa Uingereza na nadhani atafurahi sana kwa uamuzi wake wa kumtoa kwenye timu ya Taifa
1710216289771.png
 
Mkuu me siku zote sijawah sema tunashida ya wachezaji tofauti ya wewe na Cash Money
Huwa nasema tunawqchezaji wazuri ila wamekosa mwalim wa kuwaongoza na kuwaimprove

Nyie ndio mnaoamini tunawachezaj wa hovyo
Na inasikitisha sana kwa kweli wakati ubovu wa kocha unaonekana wazi kabisa
 
Pochettino akizungumzia bao la Mudryk:

"Nadhani lilikuwa bao zuri sana. Hilo ndilo tunalotarajia kutoka kwa mchezaji aliyetokea benchi - kuwa na impact

Sasa anatakiwa kushindania nafasi na wachezaji tofauti katika nafasi hiyo anayocheza. Ni [kama anaweza kuanza] juu yake mwenyewe kuliko kwangu."

Maoni yangu

Hivi Sterling anayecheza fyongo vile kuanza dhidi ya Mudryk ni juu ya Mudryk mwenyewe, ndio maana mimi namuita huyu kocha ni MLEVI
 
Lile goli la kwanza jana watu walidhani ni goli la kizembe na golikipa wa Newcastle alizembea, lakini nyuma yake kulikuwa na flick ya kijanja iliyofanywa na Jackson ambayo iliwahadaa mabeki na kipa mwenyewe.

1710217710707.png
 
Jana Mudryk kwenye goli lake dhidi ya Newcastle (goli lililotupa point zote 3) , uchezaji wake umefanana kwa karibu na ule uchezaji aliouonyesha dhidi ya Liverpool kwenye debut yake.
Napenda magoli yanayopatikana kwa style ile, iaburudisha sana
Na pia Jackson alicheza vizuri sana kwa kukaa na kuserereka na mpira hadi akampasia Gallagher aliyetaka kuremba kabla hajanyang'anywa na Mudryk na kufanya kama vile Hazard alivyokuwa anafanya

 
Michezo iliyosalia ya nyumbani msimu huu:
  1. Burnley
  2. Man Utd
  3. Everton
  4. West Ham
  5. Bournemouth
  6. *Tottenham (Itapangiwa tarehe)
Michezo iliyosalia ugenini msimu huu:
  1. Sheffield United
  2. Brighton
  3. Aston Villa
  4. Msitu wa Nottingham
  5. *Arsenal (Itapangiwa tarehe)
Maoni yangu
Hizi mechi nyingi sio ngumu na kama huyu kocha angalau atabakiwa na akili ndogo kama asilimia 60% ya mpira tunaweza okota points (20+) za kutufikisha kwenye nafasi ya 7 ili tuwe na uhakika wa kucheza ligi mojawapo ya Ulaya
 
Jana Mudryk kwenye goli lake dhidi ya Newcastle (goli lililotupa point zote 3) , uchezaji wake umefanana klwa karibu na ule uchezaji aliouonyesha dhidi ya Liverpool kwenye debut yake.
Napenda magoli yanayopatikana kwa style ile, iaburudisha sana
Na pia Jackson alicheza vizuri sana kwa kukaa na kuserereka na mpira hadi akampasia Gallagher aliyetaka kuremba kabla hajanyang'anywa na Mudryk na kufanya kama vile Hazard alivyokuwa anafanya

View attachment 2932424
Post na goal la palmer
 
Sisi Chelsea tuko kirasta fury tu, rege mbele kwa mbele

 
Habari nyepesi nyepesi
Todd Boehly alifanya safari ya hivi majuzi nchini Saudi Arabia, ambako inaaminika alikutana na waziri wa michezo na mkurugenzi wa soka wa SPL Michael Emenalo kabla ya mauzo ya Chelsea majira ya kiangazi. Chelsea pia wamefanya mazungumzo na Riyadh Air kuhusu udhamini wa klabu ya Chelsea

By Matlaw

1710257674915.png
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom