Mauricio Pochettino alalamikia waamuzi wa mechi ya Chelsea na Liverpool mwezi uliopita. Awataka kesho wasirudie hivyo kama zawadi ya kumpa Klopp anapoaga Liverpool.
ana wasiwasi kuwa maafisa wa FA watakaochezesha mtanange wa Chelsea na Liverpool kesho watachukuliwa na upepo wa SENDOFF (yaani KUAGA) ya Jurgen Klopp baada ya baadhi ya maamuzi yaliyofanywa Anfield mwezi uliopita kuipendelea Liverpool.
Amesema labda kuna watu wanaotaka kusheherekea na Klopp anapoaga
"Nadhani tulipocheza dhidi ya Liverpool kwenye uwanja wa Anfield nadhani maamuzi mengi sana...
hakuna uamuzi hata mmoja muhimu ulikuwa upande kwetu.
Penalti mbili hazikutolewa. Duels, 50-50s, mara zote upendeleo ulitolewa kwa rangi nyingine (yaani nyekundu) - mara zote nyekundu. Nataka kuwa kutendewa kwa haki."
"Walikuwa bora kuliko sisi [Anfield], bila shaka. Lakini uamuzi wa kwanza baada ya dakika tano ulikuwa penalti ya wazi. Kipindi cha pili ilikuwa penalti, Nkunku. Sisi ni Chelsea na tunahitaji kushindana na zana sawa." [telegraph]
Kwa maoni yangu niko na Poche kwa 80%
Mkwara kabla ya mechi ni muhimu
Japo hatukucheza vizuri ila waamuzi walitoa maamuzi ya upendeleo kwa Liverpool na ikijirudia tena kesho itaharibu hiyo fainali
View attachment 2914505