Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Poch analazimika kuwachezesha wachezaji out of position kutokana na ufinyu wa kikosi. Hata angekuja kocha gani kwa kikosi hiki mlitegemea kina Gallagher achezaje? Colwill au Disasi? Poch mwenyewe anajua tuna ufinyu wa kikosi na wachezaji average what do you expect hapo?

Huu ndio uhalisia
Hata wakija wote bado Poche atamchezesha Colwill kwenye LB
 
Sasa mkuu unasema mchezo umeukamata kwa dakika 70 hupati goli utafanya nini? Lazima ufanye sub kujaribu watu wengine uone watafanya nini. Halafu pia sub ni kama kamari pia. Juzi hapa tumeshuhudia game ya Egypt na Ghana. Ghana amecheza vizuri kufikia kupata uongozi wa goli 2-1 lakini kuna sub ya beki ilifanyika jamaa likaingia kuchoma kabisa.

Haya mambo kwenye mpira ni very normal kutokea. Mlitaka awaxhezeshe wachezaji walewale mwanzo mwisho bado mngesema hafanyi sub🤣
Huyo dogo Gilchrist asingetolewa, alikuwa anasaidia sana
 
Hata tukiungana wote tumchukie Poch au wachezaji hakuna kitu tunaweza badilisha, tunachofanya hapa tunabadilisha mawazo kulingana na kile tunakiona na kukielewa hivyo kwa lugha nyepesi ni kama burudani tu.

Back to the topic. Sikua na maana Gilchrist ni mbaya au alikua hasaidii ila nilichomaanisha ni lengo la Coach ni kutaka kushambulia kutokea chini. Hii inasaidia kuongeza idadi ya watu tunaposhambulia.
Unamtoa Gilchrist unamuweka Disasi na mara zote Disasi hakucheza vizuri kwenye RB, hawezi kukaba vizuri ni mzito na hawezi kufanya mashambulizi ya RB. Sisemi Disasi ni mbaya ila akicheza CB anatulia kuliko RB
 
Hivi jezi yenye jina lake ishawahi kulowa hata tone la jasho huyu jasusi???
😂😂😂😂😂
Fofana hana shida, Chelsea ndio wajinga, wameshindwa kuwahandle wachezaji. Ni Chelsea tu mchezaji anaumia akiwa mazoezini hata kabla hajacheza, Wengine wanaumia kwenye warmup
 
Weakness ya POCHE kwenye ukocha ni slow learner baadae akishawaelewa wachezaji wake, aina ya mifumo, mbinu, style za kutumia anakuwa balaa sana.

Kwa sasa Poche ameshaanza kuielewa timu, tusitegemee atapoteza mechi ovyo ovyo.
Sasa unaanza kuongea, weka na ubishi
Tendo la kumtelekeza Maatsen wakati alicheza vizuri Pre season
Tendo la kung'ang'ania kumchezesha Chilwell kwenye winga na Colwill kwenye LB wakati huo tuna LB watatu, Chilwell, Maatsen na Cucurella
Kitendo cha kuforce kumtumia Disasi kwenye LB wakati Gilchrist kashaonyesha uwezo mkubwa
Kitendo cha kumpiga benchi Petrovic hadi Sachez kaumia ndipo anapewa nafasi, Kumbuka Sacheza katuchoma sana
Hayo mambo na sub zake mbaya ndizo zilizokuwa zinatufanya sisi tumlalamikie. Akianza kuwatumia wachezaji bila ubaguzi na kuwachezesha kwenye nafasi zao pale anapoona mchezaji anayechezeshwa nafasi mpya hachezi vizuri, Pochettino atakuwa kocha mzuri na wale wote waliokuwa wanampinga watamfagilia
 
Alicheza RB na Badiashile LB, anacheza pia nafasi za CB, kote ni mzuri kwenye kukaba
Kwa mtazamo wangu huyo dogo Gilchrist anafaa zaidi kwenye nafasi ya central back rather than Rb kwanini? Dogo ni Mzuri zaidi kwenye kukaba but sio Mzuri kwenye kushambulia ndio maana kocha atampa nafasi alitaka kulinda Matokeo kutokana na hiki nilichoongea
 
Ni kwa sababu Chilwell ni mzuri katika kushambulia na kurudi chini. Yan ni mwepesi kufanya transition timu inaposhambulia na inaposhambuliwa
Tangu Chilwell acheze LW amekuwa akicheza hovyo tena sana. Anashambulia vizuri akicheza LB
Hakukuwa na haja ya kutumia hiyo kama kigezo wakati kwenye LW na RW tunao wengi. Chilwell ni LB mzuri kila mtu anajua hilo na kucheza LB haimzuii Chilwell kushambulia kama kawaida yake
 
Na wewe unaona ni sawa Chilwel akicheza LW huku unawachezaji wanaoweza cheza hizo nafas vizuri.
Kwa macho ya kishabiki naweza kusema sio sawa. Ila wenye macho ya coaching(proffessionals) na hata kwa ku crate simple logics kama navyofanya mimi(average knowledge) unaweza jua intention yake inakua ni nini hasa kulingana na mazingira na mahitaji ya game husika.

So kwangu mimi naweza laumu pengine labda kwa sababu kilichofanyika hakijaleta matokeo chanya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom