Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Hizi game za kushinda ushindi wa papatu papatu ndio zinawafanya waone waendelee kumpa muda ila kama wangekuwa wanaangalia performance huyu hakufaa hata game inayo kuwepo ilikuwa tu kesho asubuhi mnatupia virago

Sijawah kuona kocha mbishi kama huyu
The guy really stinks .
Yaani kila nikimuona natamani kutapika
 
Kiukweli kabisa ninaouona Colwill, Disasi na Gallagher hawa ndio wachezaji nawaona wanacheza kwa spirit ya hali ya juu muda wote wakiwa uwanjani. Pengine hiyo ndio sababu wanaanza zaidi.

Huwezi pata ubora wa colwil kama LB
Disasi mzito mda wowote unahisi anachoma

Huyu galagher ni mzuri kama team inatafuta mpira tofauti na hivyo hana maajabu.

Kuna wachezaj pochetino ndio chanzo cha wao kushuka viwango kwa sabab anawachezesha katika nafasi ambazo sizo

Poch katika swala zima la tactical ni hamna mtu mule

Kuna wachezaj hata wafanye vizuri game ila game ijayo bado wataanzia bench
 
Naunga mkono hoja yako kwamba sio lazima ufunge goli nyingi ushinde mechi.

Binafsi ni muumini sana uchezaji wa kupaki bus au ulinzi shirikishi. Na pia huwa naamini THE BLUES kiuchezaji utamaduni wake ni wa kupaki bus.

Poche apange 3-4-3/3-5-2


----- Mudyk -- Nkunku - Sterling ---

Matsen --- Caicedo - Enzo - Gusto

------Badi --- Silva - Disasi -----

Hata tucheze na hiyo formation stil tutafungwa tu.

Kama kocha anashindwa tengeneza ukuta hiyo ni shida hata atumie formation ipi. Lazima tupigwe

Uzuiaji wa mipira ya juu unaanzia mazoezini.

Ndio maana kila mech. Lazima tutaruhusu tu kwa mipira ya hivyo either free header au unmarked kama ya jana olise, vs newcastle etc

Shida sio formation shida ni mafunzo ya mwalim
 
Hawa ndio aina ya wachezaji tumewakosa kwa sasa, hawataki masihara, wakali na wenye amsha amsha. View attachment 2855403

Mwalim anaweza boost moral ya wachezaj au kuiua
Tuchel aliboost almost moral ya team nzima kwa spirit yake ya kutaka kuwin

Hawa wakina Rudiger, Christiansen chini ya lampard walionekana hawafai

Pochetino hata kule psg aliwafanya Messi,Neymar,Mbappe hao wote kuonekana ni wa hovyo akimchezesha Verrati mda mwingine kama 10

Mnao hisi shida ni wachezaji baada ya mda mtamkataa poch

Kama unafatilia game zetu utagundua Poch anabahatisha

Kila siku unalalamika injury spurs wenye kikosi finyu wanainjury ila matokeo bado wanapata
 
Mkuu Lukub ameeliza vizuri kwamba sio lazima ufunge goli nyingi ndio ushinde mechi. Sio lazima kosakosa nyingi za magoli za Jackson na sterling.

Nakubaliana na wewe Kocha anaweza kusuka team ikawa solid kutoruhusu kufungwa magoli ya ovyo, still goli 1 tutakalofunga likaamua matokeo.
na tukiwa na balance nzuri inaambukiza forward line wanaamini tukifunga magoli yanathamani , kwa sasa foward wanajua fika tukifunga goli moja halitoshi hata kwa low table team watachomoa TU, kwa team kama city, liver , arsenal hata tulifunga 2 hiyo mechi ni 2-2 kiufupi hatujui kuzuia, City, liver, Arsenal kwenye kufunga hawajatuzidi sana ila kwenye kufungwa tumewazidi mbali kabisa ndio sababu tuko namba 10 kwenye msimamo.
 
Mwalim anaweza boost moral ya wachezaj au kuiua
Tuchel aliboost almost moral ya team nzima kwa spirit yake ya kutaka kuwin

Hawa wakina Rudiger, Christiansen chini ya lampard walionekana hawafai

Pochetino hata kule psg aliwafanya Messi,Neymar,Mbappe hao wote kuonekana ni wa hovyo akimchezesha Verrati mda mwingine kama 10

Mnao hisi shida ni wachezaji baada ya mda mtamkataa poch

Kama unafatilia game zetu utagundua Poch anabahatisha

Kila siku unalalamika injury spurs wenye kikosi finyu wanainjury ila matokeo bado wanapata
maisha yetu yatakuwa magumu sana mpaka huyu jamaa aondoke.
 
Kweli kabisa. Yan hawa hawakua kwenye daraja la juu sana kwenye viwango ila walikua committed sana na timu. Hawacheki na kima kabisa

Hali hiyo inaanzia kwa kocha mkuu. Kocha akiwa mtu wa trust the process wachezaj na wenyewe hali hiyo wataingia nayo watahisi ni part yao ya kulearn

Ila kocha akiwa mtu anaedemand ushindi hawa wachezaj na wenyewe wataanza kuwa na roho hizo

Ila kocha baada/ kabla ya mechi anaanza trust the process blah blah nyingi hapo hata kwa wachezaj hiyo wataahisi mda bado .
Ndio maana card za njano tunazo nyingi sana kwa sababu kuna mambo yanafanyika kocha anaona ni kawaida tu anashindwa kuwacontrol wachezaji
 
HONGERENI SANA THE BLUES KWA USHINDI.

Sikubahatika kuangalia mechi ila kwa highlights za magoli nilizoona, kwa kasi walizonazo GUSTO & MUDYK ni mtaji tosha kwa kocha kimbinu.

Nafasi ya 10 inasema THE BLUES popote ulipo tupo.
Huu ushindi hata haufai pongezi, tumebahatisha, tumepapasa, timu bado sana
 
Ukiona ivyo ujue hakuna mchezaji wa maana anayeweza kumchallenge yule anayefanya madudu
Colwill kucheza kama LB na Disasi kucheza kama RB maana yake ni kunyima mashambulizi kwa sababu hawa wachezaji hawawezi kupanda na kuongeza mashambulizi kama natural fullbacks na hapo ndipo Chelsea inatesekea. Wewe unavyomweka Maatsena benchi na Madueke na kuwachezesha wachezaji wasiofaa kwenye hizo nafasi uanona ni sawa mkuu
Hao wachezaji walipoingia ndipo matokeo yao ikaanza kunufaisha timu

Tatizo kubwa la Pochettino ni kupanga timu vibaya na kufanya wachezaji wawe ineffective
Hali hii imemkumba pia Enzo yule wa Potter sasa hatumuoni kabisa

Makosa yako mengi wew fuatilia mechi na utaona
 
Lakini ni mara ngapi anawachezesha hawa wachezaji kwenye position zao na nini kilitokea? Ju,i kati kawachezesha Broja na Jackson kwa pamoja nini kinatokea? Wakati mwingine anafanya kubet tu aone wanaweza leta maajabu gani lakini inakua ngumu. Hakuna timu ilitotengeneza nafasi nyingi za kufunga kama Chelsea unataka Poch aingie yeye akafunge? Kina Jackson wanaruka ruka tu.

Spirit ya upambanaji hamna kabisa. Tukishafungwa mechi moja inayofuata ndio wanajua lazima wapambane
Shida ya Broja na Jackson inajulikana na sisi hatuzungumziii huko
Shida inaanzia hasa kwa mabeki na viungo
CB wanne bila fullback unategemea nini
Amemjaribu Enzo kwenye namba 10 amekuwa ineffective ila yeye analazimisha tu
Mchezaji yuko hovyop uwanjani anamuacha hadi dakika 90 ziishe
Shabiki anayefuatailia mechi haya madhaifu anayajua kabisa
 
Kiukweli kabisa ninaouona Colwill, Disasi na Gallagher hawa ndio wachezaji nawaona wanacheza kwa spirit ya hali ya juu muda wote wakiwa uwanjani. Pengine hiyo ndio sababu wanaanza zaidi.
Ni sawa ila Colwill mechi nyingi anacheza vibaya kwa sababu ya kuwa fullback
Disasi anaspirit nzuri ila uwezo wake ni mdogo sana, hana mbio na kujiposition vibaya ni kawaida yake
Bahati mbaya hata Badiashile baada ya kurudi majeruhi sio yule tena wa kabla
Mchezaji pekee ambaye ana consistency nzuri ni Gallagher
Hitimisho
Colwill hafai kucheza LB ila Poche ni sturbone
Disasi hafai kucheza RB ila kocha wako ni mjeuri
Madueke ana kitu ndani yake anastahili kupewwa muda hata asipoanza, Cole palmer hata akirudi awe anapumzishea. Sio mechi zote Palmer anacheza vizuri na hasa akichezeshwa kama namba 10
 
Madueke ana kitu.
Ana kitu tena kikubwa ila Pochettino sijui kama anaona, yuko attack minded, na anacheza kwa juhudi. Mimi naamini akicheza Madueke na Muderyk upande mwingine Nkunku atatengenezewa nafasi nyingi
 
Hawa ndio aina ya wachezaji tumewakosa kwa sasa, hawataki masihara, wakali na wenye amsha amsha. View attachment 2855403
Wakati wa Lampard Rudiger alikuwa auzwe, ni TT ndie alikuja kuonyesha kuwa Rudiger ni beki bora
Naamini vilew vile wakati wa Pochettino Rudiger bado angeendelea kuwa hovyo kama wakati wa Lampard
Hii observation ndio inawafanya baadhi ya mashabili wa Chelsea kutomkubali P{chettino kwani anaua vipaji na kuwafanya wachezaji bora waonekana wa hovyo
 
Ebu leo tumuongelee Di Zerbi na wale watoto wake wanavyokokota mpira, wadogo na hawana uzoefu na EPL
Kwetu huku hiyo ya udogo na kukosefu uzoefu kwenye EPL ndio kisingizio cha kucheza vibaya
Bado nawachukia wanaomfagilia Pochettino huku akituharibia vipaji tulivyonavyo Chelsea

Brighton 4 - 2 Spurs
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom