LEGENDS
3. CLAUDE MAKELELE:
Huyu mchezaji hajatokea kama yeye kabla na baada yake. Alikuwa anacheza mbele kidogo ya mabeki wa kati kama kiungo mkabaji.
Alisajiliwa kutoka Real Madrid msimu wa 2004.
Alikuwa anavaa #4.
Website ya Chelsea inasema hivi kuhusu Makelele; "The only Chelsea player to have had a position named after him."
Yaani jukumu alilokuwa nalo uwanjani hakuna mtu amewahi kuwa nalo kabla yake. Huyu jamaa alikuwa anakaba; Kushoto kwake Thiago #30, na Frank Lampard #8. Nyuma yake John Terry, Calvaho,Gallas na Paulo Ferreira.
Msimu huo tulicheza mechi zote za ligi (mechi 38) na kupata clean sheets 25.
Tulifungwa magoli 15 tu msimu mzima na tukawa mabingwa wa kihistoria kwa kufikisha points 95.
Tulifungwa magoli 6 tu msimu mzima kwenye uwanja wetu wa Stanford Bridge. Yote hayo kwa sababu huyo Jamaa Claude Makelele. Aliondoka mwaka 2008, akiwa mchezaji huru. Chelsea walimwacha aende huru kwa sababu ya heshimu aliyokuwa nayo kwenye timu.