Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Mudryk kacheza dk 19 na akatengeneza big chances 3 kuliko mchezaji yeyote wa Chelsea au Arsenal

0_Liverpool-FC-v-Chelsea-FC-Premier-League.jpg

FvJuTD4X0BII2-P
Hapa napo tuliibiwa pesa
 
Ukiweka ushabiki pembeni, Jana ndiyo nimejua Chelsea hamna timu,.mna wachezaji.

Ukiacha zile movement za odegard za magoli. Kuna movement moja, ilikuwa Saka na odegard, wamecheza one-two, alafu odegard anapita mbele ya wachezaji wawili wa Chelsea. anaenda kujiposition kupokea pass ya Saka, Cha ajabu hakuna anayejaribu kumpa pressure Saka Wala odegard, hata kujaribu kuziba njia ya pass hakuna.

Yani hii timu Pochetino aje na bunduki akiaMungu ndiyo mtatoboa. Kuna vitu basic kabisa wachezaji wanashindwa kufanya, hata kugombani mpira, wachezaji wa Chelsea wamelegea kama mlenda, easily kabisa anadondoka chini.

Kwa mlipofikia inabidi kocha amuige Tenhag. Tenhag game za mwanzo timu inacheza hovyo, haifanyi vitu basic, kafuta ratiba ya kupumzika, kaenda kuwakimbiza mazoezini.

Poch akiwa mpole mtabadilisha makocha karibu Dunia nzima
 
Kuna uwezekano mkubwa mechi ya mwisho ikawa ya maamuzi ya Kubaki EPL au muende championship
 
Lampard hana akili, Uingereza umemjaa.
Sio Mudryk tu, utaona hata Badiashile hachezi ila Chalobah anacheza

Katika maamuzi mabov ya Boehly ukiachana na Potter ni kumleta Lampard tena mtu ambae hana tactics zozote yani anategemea wachezaj tu,

Tuna wachezaj wazuri sema wamekosa mwalim wakuwaongoza.

Kulikuwa hakuna haja ya kumleta Lampard kwa aina ya matokeo tuliyokuwa nayo.
Ndio maana mimi wengine wanaposema kocha mbovu mimi nasema aliyemleta kocha mbovu ndie mbovu zaidi
Haya yote yasingetokea kama sio maamuzi mabaya na ya kukurupuka ya Boehly
Typical style ya wamerekani
 
chelsea mechi tano za mwisho asipokaza anashukaa daraja, nimeacha kushabikia the blues
Tatizo haliko kwetu tu, hata tufungwe zote hatutashuka daraja, zile timu tano za mwisho ni choka mbaya wakijitahidi ni points 4 kwa mechi zilizobaki wataishia kwenye 34pts
 
Ukiweka ushabiki pembeni, Jana ndiyo nimejua Chelsea hamna timu,.mna wachezaji.

Ukiacha zile movement za odegard za magoli. Kuna movement moja, ilikuwa Saka na odegard, wamecheza one-two, alafu odegard anapita mbele ya wachezaji wawili wa Chelsea. anaenda kujiposition kupokea pass ya Saka, Cha ajabu hakuna anayejaribu kumpa pressure Saka Wala odegard, hata kujaribu kuziba njia ya pass hakuna.

Yani hii timu Pochetino aje na bunduki akiaMungu ndiyo mtatoboa. Kuna vitu basic kabisa wachezaji wanashindwa kufanya, hata kugombani mpira, wachezaji wa Chelsea wamelegea kama mlenda, easily kabisa anadondoka chini.

Kwa mlipofikia inabidi kocha amuige Tenhag. Tenhag game za mwanzo timu inacheza hovyo, haifanyi vitu basic, kafuta ratiba ya kupumzika, kaenda kuwakimbiza mazoezini.

Poch akiwa mpole mtabadilisha makocha karibu Dunia nzima
Mbinu moja ambayo naijua ya Lampard kwenye kujilinda ni Zonal marking ambayo inamtaka mchezaji arudi nyuma badala ya kupress au kufanya man to mana marking. Hapo ndiko Lampard anapoangukia pua puu. Timu ndogo ndizo zinafanya zonal marking. Wachezaji wamechanganywa kabisa na mbinu za Poter mara Lampard
 
Uhakika ni huu, Bornemouth wanatufunga na kuingia rasmi nafasi ya 13
Atakayebisha akabeti aliwe pesa
Na hiyo nafasi ya 13 nadhani ndio itakuwa nafasi yetu hadi ligi iishe
 
Hivi ni mimi tu niliona jinsi jana Sterling anavyotoa pasi kama toto la miaka miwili

Ndio maana PEP kamuondoa city haraka, hakuna tena mchezaji pale.

DTW_7928.jpg
Sijui kwanini anan'gan'ganiwa na makocha hasa huyu lamps Bora hata chini ya Potter angalau alikuwa anaonesha performance sio kwa huyu lamps
 
Kwan Chelsea kuna shida gani je kweli tatzo kocha au tatzo wachezaji aje unaweza timuwa wachezajo wote ukaanza upya au nn kifanyike
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom