Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea nyie ndio FAHARI ya London sio ile misule ya Arteta.
Tunawaomba leo msituangushe kuanua matanga rasmi pale kwenye makaburi ya Emirates.
Hizi kima za Arteta sasa hivi ziko very dispirited, mimi nina imani mtazifunga, na hata ikishindikana kuzifunga ila mnauwezo wa kutoa kudraw.
Hakikishe huyu marehemu Tembo asirudi tena juu ya mti hata kwa sekunde mbili.

Chelsea ingawa ni kweli msimu huu hampo kwenye ubora wenu lakini hizi Arsenyau zinapaswa ziwaheshimu na zitambue kuwa nyie ndio:

- Klabu ya mwisho ya kiingereza kushinda Ligi ya mabingwa Ulaya

- Klabu ya mwisho ya kiingereza kushinda Europa League

- Klabu ya mwisho kutoka London kushinda kombe la Ligi kuu ya Uingereza

- Klabu ya mwisho ya kiingereza kushinda kombe la Super Cup

- Klabu ya mwisho ya kiingereza kushinda kombe la dunia la vilabu la FIFA
tapatalk_-764896337_540x624.jpg
 
Wachezaji wa kawaida wapo kibao kama:-

1. Miss epl
2. Waruwaru
3. Mpira vurugu
4. Paparazi
5. Kwashakoo
6. Mtumishi hewa
7. Ndege John

Labda useme kwamba timu ikiwa na mfumo bora, wale wachezaji bora watawabeba hawa wa kawaida nao waonekane bora, hence timu bora.

Dah
Mbavu zangu Mimi

Huwa naenjoy nikisoma comment zako Mkuu.
 
Yatapitaaa
Yana mwishoo
Iko siku mutayasahau
Watawaheshimu wanaowadharau
 
Wachezaji wazuri ila waliosajiliwa hivi karibuni sio wa utamaduni wetu, sio type yetu, sio style yetu.

Ni wazuri ila sio wazuri kwenye utamaduni/style yetu ya kutupa mafanikio.

Wachezaji waliotupa mafanikio huko nyuma hawakuwa style ya kina:-

Kai, Mudyk, Madueke, Pulisic, Badieshile, Cucurela, Enzo.

Turudi kwenye utamaduni wetu wa kusajili wachezaji wanaume wa kazi, vipaji kazi sio vipaji bleach, tatooes, kudeka.

Vipaji vyenye uchu wa mafanikio, uchu wa upambanaji na kujituma sio vipaji vya bora liende, bora tulipwe mshahara, vipaji mzigo.


Mtasema mpira wa siku hizi umebadila blah blah, ila nawaambia kamwe Chelsea haitabadilika kwenye uchezaji wake, utamaduni wake, sajili za wachezaji wa aina yake, jinsi ya kubeba makombe yake
Style yetu ndio ipi? akina Drogba, Hazard na wengineo walianza hivi hivi baadaye wakaja kuwa moto
MOU aligombana sana na Hazard alipokuwa 22, hajitumi, anadeka lakini baadaye akaja kubadilika hasa akiwa 24
Tuacheni kulalamika bure, wachezaji ni wazuri, uongozi urekebishe tu makosa na kocha mzuri aajiriwe mambo yatarudi normal. Meli imeyumba haitazama
 
Kwa mpira gan anaocheza mount nyie ndo mnaharibu mpira kwa kupandisha mishahara ya wachezaji wa kawaida sana
Mount amekuwa victim wa unyanyapaa wa kwenye social media tangu muda mrefu huku mkijisahaulisha kuwa miisimu miwili Mount kawa mchezaji bora, UCL yeye alikuwa critical factor sisi kubeba UEFA. Kama haumjui mchezaji just nyamaza
 
Sijawahi kuona duniani, timu inashinda bila kufunga magoli. Labda Ushindi wa mikwaju ya penati.

The blues haina uwezo wa kufunga magoli. Kwenye Miezi 5 tumefunga goli 1.

Labda mabeki wa Aser8 wafungwe jicho 1 na kitambaa cheusi na mikono yao ifungwe pingu.
Gabi atajifunga leo au atatoa penalti
 
Leo ndiyo siku tunaenda kumuonesha Boehly na genge lake la wahuni, Nini ya maana ya project (trust the process)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom