Naomba unijibu kiufupi tu. What are the achievements of arteta in three year with Arsenal????
Alafu ndio unajiita eti unajua mpira.....! Unabishana kitoto sana, huna unachojua na ni aibu kuendelea kubishana na member wengine humu wanaojua mpira na tunaheshimu michango yao
Jurgen klop alipata mafanikio gani pale Liverpool ndani ya misimu 3 ya Kwanza? Kwa team iliyopoteza momentum ya makombe kama ilivokuwa Liverpool kushinda taji haraka hivo haiwezi kuwa priority ndomana klop akaachwa awin ndani na nje ya uwanja
unauliza Mikel ameachive nini pale Arsenal ndani ya misimu mitatu kwamba hujui au ndo unaendeleza utoto wako? Umeanza kuangalia mpira baada ya potter kuwa kocha wa Chelsea au sio?
Mikel amepata community shield na FA cup ndani ya misimu yake miwili au hizo sio Achievement? Ukiachana na hayo mafanikio ambayo ni tangible, ila ana mafanikio mengine mengi tu kapata pale Arsenal
Mikel kurudisha traditional ya club,karudisha club Kwa mashabiki maana mashabiki walikuwa washapoteza Imani na team Yao, karudisha bond Kati ya wamiliki, wachezaji,kocha na mashabiki na kama hiyo haitoshi karudisha IMANI tena Kwa mashabiki
Ingekuwa Liverpool wajinga kama wewe wangekuwa wameshamtimua klop Kwa sababu ndani ya misimu mitatu basi hajashinda chochote, ila kwakuwa wanajua mafanikio ni progress na klop alikuwa anaonesha hiyo progress ndomana akavumiliwa na leo wapo hapo walipo
Acha kufananisha mafanikio ambayo wanapata makocha wanaopita Chelsea, maana wale wanakuta team ina kila kitu, Kwa miaka 10 sasa Chelsea imekuwa ni club yenye momentum ya mafanikio na pia bado identity Yao haijapotea kama ilivokuwa Kwa Liverpool,Man u na Arsenal
Tuchel ungepeleka Man u saiz angekuwa kafukuzwa na hana ata Community shield,mpeleke dimateo Arsenal asingemaliza ata nusu msimu,mpeleke Boas Liverpool angemaliza nafasi ya 8
Sio kwa sababu wao ni makocha wabaya, ila hizo team zina changamoto nyingi sana tofauti na Chelsea ambayo yenyewe imekuwa ni sehemu salama Kwa kila aina ya kocha anaeenda maana wapo kwenye kilele Chao cha mafanikio kabla hawajaingia kwenye anguko
Kutokana na hizo sababu ndomana karibia kila kocha aliepita Chelsea alivuna mafanikio na kwenda kufia huko pasipojulikana, Kwa sababu kufanya kazi Chelsea ukiwa kocha ilikuwa ni rahisi sana na itaendelea kuwa rahisi sana hadi pale mtakofika kwenye diminishing point nanyie
Wanaokwambia Arsenal atamaliza top four sio wajinga kama wewe, wanaangalia progression ya Arsenal tangu Mikel kapewa team, wanafatilia wachezaji waliotoka na waliongia, wanafatilia uchezaji wa Arsenal ya zamani na sasa, we endelea kuishi Kwa kukalili na endelea kujiita unajua mpira kumbe huna unachokijua