Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chukwuemeka juzi alifunga goli mbili kwenye mechi ya kirafiki kujiweka fit. Nadhani ataanza kupewa dakika za kucheza uwanjani.
Yah ! Wafanye hivyo ,hawa akina Kante cova na Jogi Zama zao zimeisha msimu ujao wote waondoke tuanze upya kusuka mildfield , in the mean time tuanze kuwazoesha hawa madogo kulitawala dimba .wapewe muda WA kutosha
 
Ramires alikuwa anajua kufunga kukiko hata viungo washambuliaji tulionao sasa
Kimpira kuzaliwa Brazil ni zaidi ya baraka. Hebu waangalie hawa kina Vini Jr, Richarlson, Raphinha, Rodrygo, Antony. Huwa namfuatilia pia Pedro kule Lazio mambo anayofanya kama hana miaka 35.

Ndio maana mimi nilikua namlaumu Willian siku zote kile sio kiwango chake. Alikua anatudanya sana na sijui kwa nini alikua ana under perform.
 
Sikumbuki nilisoma wapi ila katika pitapita zangu mitandaoni niliona kuna mahali wameandika katika hizi mechi za kirafiki Potter kamchezesha Chalobah kama kiungo mkabaji na amefanya nae mazungumzo kuona kama anaweza kumbadilisha position.
Chilwell hawezi ila James anaweza akacheza kama DM, hata Cucurella nazani na Fofana. CB wengi wanaweza kucheza kama DM
 
Sikumbuki nilisoma wapi ila katika pitapita zangu mitandaoni niliona kuna mahali wameandika katika hizi mechi za kirafiki Potter kamchezesha Chalobah kama kiungo mkabaji na amefanya nae mazungumzo kuona kama anaweza kumbadilisha position.
Ila Chalobah naona kama Mzito ila sio kama Jorginho
 
Taarifa kutoka Ujeruman, zinasema Nkunku alifanyiwa vipimo vya afya mwishon mwa dirisha la usajil vya kujiunga chelsea msim ujao,huku chelsea wakijiandaa kuactivate release clause yake hapo baadae
Hii taarifa sielewi kitu kimoja nkunku kasajiliwa teyari ni mali ya chelsea anasubiri msimu uishe ajiunge rasmi na Chelsea au Chelsea walikaribia hatua za mwisho wa kumsajili lakini dili likashindikana kukamilika katika hizi statement nilizoanisha ipi ni sahihi? Wadau nipeni ufafanuzi kwenye hili lembu Cash Money Forever Southern Highland
 
Hii taarifa sielewi kitu kimoja nkunku kasajiliwa teyari ni mali ya chelsea anasubiri msimu uishe ajiunge rasmi na Chelsea au Chelsea walikaribia hatua za mwisho wa kumsajili lakini dili likashindikana kukamilika katika hizi statement nilizoanisha ipi ni sahihi? Wadau nipeni ufafanuzi kwenye hili lembu Cash Money Forever Southern Highland
Hizo ni tetesi, ukweli bado hauko wazi
Naona pia tetesi hizi zimekosewa, mchezaji afanye medical kabla ya makubaliano ya pande zote tatu!
Kama muda wa kuactivate release clause ndio huu basi inaweza ikawa kweli Nkunku na Chelsea wamefikiana makubalino ya siri na klabu sio lazi9ma ihusishwe kwa sababu mkataba ndio unaoongea

Taarifa zinasema akishamaliza medical anasaini mkataba ambao atakaa klabuni hapoo hadi June 2023
 
Ben ni mzuri zaidi ya Cucurela, kilichokuwa kinamuweka bench ni fitness yake bado haijapanda
Kwasasa fitness yake imerudi wewe si umeona alichofanya dhidi ya newcastle kilichobakia ni kuaminiwa tu
 
Apart from Nkunku, the Blues are also said to be targeting other midfield signings, including West Ham’s Declan Rice and Borussia Dortmund star Jude Bellingham.
 
Apart from Nkunku, the Blues are also said to be targeting other midfield signings, including West Ham’s Declan Rice and Borussia Dortmund star Jude Bellingham.
Declan rice ni mchezaji wa kawaida wakusema tujivunie nae ni Bora hiyo nafasi tumsajili Edson Alvarez au de jong ambao wapo vizuri zaidi ya huyo
 
1664548016580.png
 
Declan rice ni mchezaji wa kawaida wakusema tujivunie nae ni Bora hiyo nafasi tumsajili Edson Alvarez au de jong ambao wapo vizuri zaidi ya huyo
Kwenye DM Declan Rice ni mzuri kuliko hao wote, sema Declan rice sio mzuri na sio mbunifu kwa kupeleka mipira ya mashambulizi, De Jong anaweza kumshinda kwa attacking phase, Alvarez simjui kwa undani
Kama tunamtaka DM tu wa kuwalinda CB Rice is the best option ila kama tunamtaka a multipurpose MF, De Jong anaweza kuwa bora. De Jong kwa pasi na kupeleka key passes ni better than Rice, ila kwa kulinda goli Rice ana pumzi ya kutawala eneo la hatari na ana uwezo mkubwa wa kublock au kufanya clean tackles kuliko hao wengine

Hizi screenshot mbili ni stats za attacking phase kwa msimu huu ambazo zinaonyesha De Jong ni mzuri sana kule mbele kuliko Rice
1664549076062.png


1664549428437.png


Hizi ni stats zinazoonyesha defensive ability ya hao wawili, Rice kamuacha mbali De Jong

1664549257615.png
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom