Shujaa wetu wa ubingwa wa UCL 2012 Ramires katangaza kushusha madaluga katika umri wa miaka 35
Tutamkumbuka sana kwa goli lake dhidi ya Barcelona 2012
From nowhere wakati muhimu kwa ushindi anajitokeza na kufunga bao la kiufundi
Hii ilikuwa mechi ya marudiano nusu fainali za UCL ambapo Chelsea ilishinda darajani kwa goli moja bila goli lililofungwa na Drogba dk ya 45+2 kabla ya HT kutoka kwa pasi murua ya kushtukiza kutoka kwa Ramires
Mechi ya marudiano Camp Nou Chelsea ilizidiwa sana na matukio haya makuu matano yalitokea
- Terry kupewa kadi nyekundu dakika 36 huku chelsea ikiwa nyuma kwa goli moja
- Dakika ya 43 Chelsea inabandikwa goli la pili huku wakichezaji 10 uwanjani
- Dakika ya 45 Ramires akitokea katikati ya mabeki wa Barcelona anafunga kwa maringo bila panic yeyote goli na kufanya matokeo kuwa 2-1 kabla tu ya HT
- Dakika ya 47 kipindi cha pili Drogba anasababisha penalti huku akionyesha hali ya kukata tamaa, penalti ambayo Mesi alipiga akagonga mwamba wa juu kulia na kurudi uwanjani. Lost chance
- Toress anashindilia msumari kwa goli la dakika ya 90 na kufanya matokeo kuwa 2-2
Chelsea ilishinda mechi hiyo kwa aggregate ya 3-2
View attachment 2371033