Papaa Gx
JF-Expert Member
- Oct 10, 2016
- 11,508
- 18,668
Kwenye dirisha hili la usajili Chelsea imeweka rekodi mpya kwa kutumia pesa nyingi katika usajili wake.
Nichukue nafasi hii kumpongeza Tajiri wetu Boehly kiukweli amefanya kazi kubwa Sana kwenye Hili dirisha ametuprove wrong wapenzi wengi wa chelseafc dirisha la kwanza tu ametumia kiasi kikubwa Cha fedha kwenye usajili nadhani kuliko Tajiri wowote wa Teams za Ulaya na kikubwa zaidi amezingatia mahitaji ya kocha hata pale ambapo kuna wachezaji alikuwa anawataka binafsi kama Ronaldo lakini kwazingatia Mapendezo ya TT ameamua asimsajili tu kwasababu TT amemkataa.
Kutokana na usajili Huu uliofanyika TT ana deni kubwa kwa mashabiki kwasababu kapewa kila kitu na Wamiliki hana excuses zozote zaidi ya kuona tunapata matokeo yenye kutupa makombe.Kazi imebaki kwake tuone nini atafanya na hamu kubwa leo nini ataongea kwenye press conference atakayoifanya jioni ya leo baada ya dirisha kufungwa.


