Wakipewa wakakosa mtaanza auzwe auzwe. Mchezaji asiye na experience inabidi apewe kidogo kidogo, akitendea wema muda mdogo aliopewa anongezewa hadi anapewa kabisa
Kocha anapokupa dakika 6 kila dakika moja unavyocheza na mpira au bila mpira anarekodi. uchezaji wako ukiridhisha anaongeza muda au unaanza kabisa. Compusure ya Broja na Galagher sio ya kurudhisha kwa hizo dakika chache wanazopewa. EPL sio Development league au mazoezi ya pale Cobham. Ligi ya wanaume hii ukifanya majaribio ya wachezaji kama preseason unafanyiziwa ile mbaya
TT ameahidi atawapa muda lakini sio kama zawadi, they must fight for it
Wakati Chalobah anpopewa muda alicheza vizuri akawa anapewa zaidi. Pale alipoanza kucheza sarakasi badala ya mpira akazimishwa OUT, yuko wapi sasa hivi. Hizi academy wa chini ya 22 ninyi hamuwajui tu. Hata kiakili bado havijakomaa, unaona Galagher ile penalti alivyopiga dhidi ya Charlortte FC? hata game za pre season Galagher hakucheza kama alivyokuwa anacheza Palace hadi wengine tukaanza kumlinganisha na Mount. Kwa maoni yangu Broja na Galagher bado sana kwenye first squad, watatupotezea muda. Kama wana haraka wasepe, kama wanaipenda timu wafuate utaratibu wa kocha na ushauri wake. KOcha na wasaidizi wake wa ufundi wanawafahamu hao vijana kuliko sisi