Binafsi sikutegemea TODDY BOEHLY angefanya sajili hizi mpaka sasa.
Nilishajiandaa na maumivu ya ubahili wa wamarekani kwenye soka.
Aisee BOEHLY apongezwe sana mpaka sasa, ameturudishia ile furaha ya Roman Abramovich kwenye dirisha ya usajili.
Kama Dirisha hili ambalo hatuna Mkurugenzi wa michezo, tunaruka na sajili za maana pengine hazikuwa kwenye target ya Marina.
Embu vuta picha ndio tumempata huyo Mkurugenzi wa michezo na akakaa meza moja na TT, wakaanza kusuka timu, huku BOEHLY anasindikiza na mpunga kama kawaida, mbona tutabeba EPL mfululizo.
Kwa mchezaji anayesajiliwa dirisha hili, hata akiflop simlaumu kabisa tajiri BOEHLY.
Kwa sababu amejaribu kutuonyesha kwamba yuko tayari kuwekeza kishindani zaidi na yuko tayari kuendeleza utamaduni wetu wa kubeba kombe kila msimu.
Wana BLUES tumshukuru Mungu sana kumpata TODDY BOEHLY (Mmarekani mwenye asili ya kiarabu na Urusi kwenye kumwaga mpunga).