Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Kama hamna ni bora tukacheza na false 9 kuliko kuwa na striker atakaeza nafasi. Yaan ni bora tungebak na Lukawise kuliko kutegemea huyo mhindi.
Kama hamna huyo striker wa uhakika sokoni ndio maana jamaa akakwambia ni Bora tukabaki broja tumuamini anaweza kutupa kitu mbona wakina james,mount wamefika hapo walipo baada ya kuaminiwa na club
 
Kwa maelezo ya kocha wa Sevilla ni kama dili la Kounde ni "DONE"

Sevilla boss Julen Lopetegui decision hints at Jules Kounde's Chelsea transfer being 'done deal'

And Julen Lopetegui has done something revealing that hints at movement on the deal for Sevilla's No.23. This is because as per @InfoSevillismo, Lopetegui told local media: "Kounde arrived at the Ciudad Deportiva of Sevilla FC on Wednesday morning but has not trained with his teammates. Departure is imminent."

1658328858870.png


1658328826527.png
 
Hivi mnajuta nini kwa Tammy Abraham jamani? mmekosa vitu vy kujuta.
Broja pia ni wa kawaida sana, chelsea inahitaji striker wa uhakika sio hao wa kuunga unga.
Nitajie wachezaji waliofunga magoli 15+ toka mwaka 2020.

Hata wakina Mount na James walianza kuwa wa kawaida lakini kwakua walipata nafasi wakaonyesha uwezo leo hii panga pangua hawa wachezaji wakiwa fit huwezi acha kuwapanga. Leo hii Broja anakuja mulemule walipotokea kina Mount wamecheza mikopo kama misimu miwili na kwenye timu kuna uhitaji mkubwa wa namba tisa sokoni hakuna mchezaji wa maana sasa kwa nini huyu dogo asipewe nafasi kama ilivyokuwa kwa hawa wengine?
 
[emoji117] Chief tumefanya jitihada nyingi na kubwa kusajili mastriker, nadhani mwisho wa siku tukubali hiyo no 9 ina mkosi THE BLUES.

[emoji117] Sidhani kama watatokea tena mastriker wengine wakaimudu hiyo nafasi zaidi ya Drogba, Costa na Anelka Mapungo.

[emoji117] Muda mwingine nawaza ubora wa mawinga na attacking midfielders tulionao kwa sasa baada ya Hazard, Willan, Lampard na Fab kuondoka.

[emoji117] Je Lukaku angewakuta wachezaji caliber ya Hazard, Willian na Fab angefail namna hii?

[emoji117] Kuna maswali mengi sana ya kujiuliza kuhusu hii No 9 THE BLUES.
Mkuu hii ya kusema namba 9 ina gundu ni nadharia tu lakini haina ukweli ni sisi wenyewe tu. Hivi mgoja nikuulize kwa mfano tunapata nafasi ya kusajili mchezaji mzuri na huyo mchezaji anaona namna tunavyowatendea wachezaji wa academy unadhani yeye atajisikiaje? Wakati mwingine kuna mambo tunayapuuzia ila kwa namna fulani tunakua tunapoteza competitive advantage globally. Tunajiuliza Barca hawana hela ila wachezaji wanataka kwenda huko tumemtaka Lewandowski lakini yeye mwenyewe kajipeleka Barca, Kounde alikua anataka ila ya huko yamemshinda saivi ndio anakuja huku.

Tutakua watu wa kuomba omba mpaka lini na zama za sasa sio zile timu haiwezi kuspend hela nyingi tena tunaweza promote hawa wachezaji na bado wakatusaidia. Unaomba iwapo una uhitaji tunao uwezo wa kuziba nafasi za kina Drogba na Costa ni sisi tu hatujaamua.
 
[emoji117] Lakini Chief uongozi wa Roman ndio haukuweka kipaumbele sana kwenye vijana wa academy kupenya timu ya wakubwa.

[emoji117] Utawala wa Roman ulikuwa unaamini katika Ready made/Matured players/Mastaa, ndio maana THE BLUES ni club iliyoongoza duniani kutoa wachezaji wengi (Academy) kwa mkopo.

[emoji117] Ndio maana unaona hata ile ban ya kutosajili iliwaleta wakina Mount, Abraham, James n.k kama alternative ya usajili wakapata nafasi ya kutumika kukosi cha kwanza

[emoji117] Swali limebaki kwa Uongozi wa tajiri TODDY BOEHLY, je utaamini katika kutumia rasilimali ya vipaji kutoka academy?
Sio kweli, Abramovich aliwadhaminiu academy kwa kiwango kinachotakiwa. Kuna wachezaji wengi hadi wengine ni malegend wa chelsea wametokea academy. Kama tulivyogusia huko nyuma, ligi za sasa hivi muda wa kumsubiri academy akue haupo kwa hiyo ni lazima academy ajitume ili awe na sifa ya kupewa nafasi sio kwa upendeleo. Timu zote kubwa ukianzia City, Liverpool na wengineo hawawapi academy nafasi kwa urahisi unless wamepambania. Timu pekee EPL iliyokuwa inawapa academy nafasi ni Arsenal na wako wapi,

Huwezi shinda makombe kama unawafanyia academy ukarimu uliokidhiri na tukumbuke kuwa kila mwaka academy wanazaliwa na ikiwa kila mwaka lazima uwaingize first team basi within 3 to 5 yrs utakuwa na academy team tu

Mimi nafikiri academy nao wawe na adabu, wasiwe na papara kuingia kwenye first team. Hakuna kocha anayemuacha mchezaji akionyesha uwezo uwanjani

Timu ndogo kama Westham wanamtaka kwa sababu kwanza watamnunua kwa bei rahisi na pili wao hawapiganii makombe na tatu, kamari ikienda vizuri akaja kuwa great player watamuuza kwa faida

Tayari kwa sasa tuna products za academy wengi
Kuna
  1. Conor
  2. Mount
  3. James
  4. Cheek
  5. Levi Colwill
  6. Broja
  7. Chalobah
  8. Odoi
  9. Gilmour
  10. Ampadu
Wanaotaka kuingia
  1. Charlie Webster
  2. Harvey Vale
  3. Lewis Hall
  4. Xavier Simon
Ukiwachnagnay na wale wenye umri wa academy
  1. Havertz
  2. Pulisic
  3. Malang Sarr
Na wote wanataka kupewa nafasi, tukiwasikiliza hawa watoto tutapoteza dira ya kugombea makombe
Broja, Colwill wakubali muda kidogo watakaopewa na waonyeshe kuwa wanastahili kupewa zaidi. Sasa hata hawakuonyesha halafu waingizwe tu tuache kusajili wazoefu wa kutupa makombe kama wanavyofanya City, Liver na wengineo kweli tutatoboa.

Hakuna anayekataa wasipewe muda ila na wao waheshimu muda kidogo watakaopewa kwenye mashindano yeyote iwe friendly, Karabo, Fa, UEFA EPl nk
 
Nitajie wachezaji waliofunga magoli 15+ toka mwaka 2020.

Hata wakina Mount na James walianza kuwa wa kawaida lakini kwakua walipata nafasi wakaonyesha uwezo leo hii panga pangua hawa wachezaji wakiwa fit huwezi acha kuwapanga. Leo hii Broja anakuja mulemule walipotokea kina Mount wamecheza mikopo kama misimu miwili na kwenye timu kuna uhitaji mkubwa wa namba tisa sokoni hakuna mchezaji wa maana sasa kwa nini huyu dogo asipewe nafasi kama ilivyokuwa kwa hawa wengine?
Broja nadhani hata yeye hajatulia, analo wenge. At 20 bado ni mdogo sana na future kubwa kama kweli anaipenda Chelsea. Halafu advantage nyingine aliyonayo ni kwamba kocha anataka asiondoke. Kama ataondoka aende kwa mkopo, lakini yeye anashinikiza aondoke permanently. Kule WHU anaenda kuwa backup pia kwa Mikhail Antonio. Fursa kwa hawa watoto zipo nyingi sana tu given that 5 subs zitaruhusiwa msimu ujao. Mvumilivu hula mbivu, hata wahenga walinena.
Screenshot_20220720-203828_OneFootball.jpg
 
Nitajie wachezaji waliofunga magoli 15+ toka mwaka 2020.

Hata wakina Mount na James walianza kuwa wa kawaida lakini kwakua walipata nafasi wakaonyesha uwezo leo hii panga pangua hawa wachezaji wakiwa fit huwezi acha kuwapanga. Leo hii Broja anakuja mulemule walipotokea kina Mount wamecheza mikopo kama misimu miwili na kwenye timu kuna uhitaji mkubwa wa namba tisa sokoni hakuna mchezaji wa maana sasa kwa nini huyu dogo asipewe nafasi kama ilivyokuwa kwa hawa wengine?
Sasa kina mount na james ni mastriker, halafu goli +15 kwenye ligi gani, mana hata huyo lukaku alikua italy huko anapga double figure si mchezo.
Kama namba tisa sokoni hakuna ni bora kucheza false9, au si bora wangemwacha tu bongoli, kuliko kumtegemea huyo dogo.
Halafu kucheza na namba 9 wakat kiungo mbunifu hakuna tutarud kulele kule kumtukana huyo dogo.
 
Hili la BROJA kusalia THE BLUES naliunga mkono. Usajili wa namba 9 umekuwa kimeo.

Dogo abaki tuu kama ulivyoshauri huko nyuma anaweza kuitoa mkosi hiyo namba.

Hivi Batshuayi anaondoka tena kwa mkopo au anamalizia mwaka 1 wa mkataba wake THE BLUES?
Hawa watoto wenye big egos at such a tender age, mara nyingi mafanikio yanakuwa ya kusuasua. Wengi wameishia championship. Broja atulie tu, ana future kubwa klabuni.

Batman yuko kama kuku wa dawa [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Nadhani Broja akilazimisha kuondoka yeye atabaki. Lakini TT hinted kwamba anaweza kubaki maana amebakiza mwaka mmoja.
 
Sasa kina mount na james ni mastriker, halafu goli +15 kwenye ligi gani, mana hata huyo lukaku alikua italy huko anapga double figure si mchezo.
Kama namba tisa sokoni hakuna ni bora kucheza false9, au si bora wangemwacha tu bongoli, kuliko kumtegemea huyo dogo.
Halafu kucheza na namba 9 wakat kiungo mbunifu hakuna tutarud kulele kule kumtukana huyo dogo.
Misinterpretation kabisa, kiongozi kataja Mount na James kama academy waliopambania nafasi zao sio kama striker. Pili Abraham ndie anaongoza Chelsea kwa kufunga magoli mengi tangu aondoke, hakuna aliyemfikia. Tunazungumzia magoli 15+ ya EPL aliyofuunga Abraham msimu wa 2019/20
 
Mechi dhidi ya Charlotte ni kesho saa nane na nusu mchana sio usiku kama walivyodokeza wengine
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom