Jamani niliwahi kusema hapa kwamba hauhutaji kutoa maelezo mengi sn kuelezea ni namna gani umefanikiwa ktk maisha yako au elimu yako au biashara y'all.....
Huitaji kusema ooooh Mimi nilisoma na Obama Harvard University wakati Obama ni rais wa serikali chuo...
Huitaji kusema ooooh Mimi nilimkopesha Bill Gets mtaji na Mimi ni tajiri....
Huitaji kusema ooooh Mimi nilikuwa naogelea kwenye pool moja na Tony Blair huko mitaa London....
Yaani huitaji kutoa maelezo meeeengi kweli ya kujieleza kuhusu mafanikio yako....
Kile unachoweza kufanya unatakiwa kuacha vitu vijieleze vyenyewe na ndicho anachofanya Tomasi Tuko sasaivi.
Yaani anaacha goma linajieleza lenyewe.....
Alafu nikuchekeshe kidogo
Wakati Tomasi Tuko anaichukua Chelsea last season alisema anataka kutengeneza timu ambayo hakuna timu itapenda kucheza nao.....
Sasa hayo maneno yameanza kutimia.... Hakuna Timu kabisa inapenda kukutana na Chelsea kwa sasa!
Alafu nikuongezee kicheko kidogo kingine yaani hii ni kutokana na vitu vinavojieleza venyewe.... Rio Ferdinand anasema hivi yaani Chelsea ni timu inayoweza kukufunga kila upande yaani kila mchezaji anakufunga tu.....
Timu inatisha sn yaani tena unakuta Pounds milioni 150 iko nje yaani Lukaku na timu inafunga tu magoli kibao.... Timu inatisha sn yaani inatisha mno.... Sasa ilivokuwa inacheza na Leicester City yaani Leicester City walionekana km watoto wanapambana na dubwana kuuuba kweli....
Sasa ndio nakumbuka na maneno Mauricio Pochetinho eti eeeeti Chelsea ni timu inayo jilinda sn ndio maana haifungwi magoli sn.... Jamani jamani hivi huyu Mauricio hamnazo? Chelsea inapaki bus wakati muda wote Banuchi wa juve alikuwa analambishwa nyasi?
Huyu nataka tukutane nae kwenye second legs ya KO ili atujue sisi kuwa ni mabingwa wa Ulaya....
Mwisho tumkaribishe Michael Carrick next Sunday.....