𝐓𝐔𝐂𝐇𝐄𝐋 𝐀𝐋𝐈𝐇𝐈𝐓𝐀𝐉𝐈 𝐃𝐊 𝟒𝟓 𝐓𝐔 ....

Kipindi cha kwanza Nuno Santo alipatia mbinu na shape ya timu yake ..alitengeneza shape ya Diamond ( Alli, Lo Celso, Ndombele na Pierre ) ..kwenye mbinu ni pale alipoamua kuwa press Chelsea wakianza nyuma ( Kane, Son na Lo Celso ) wote wanawapa presha Silva, Christensen na Rudiger huku Alli akifanya " Man Marking " kwa Jorginho na matokeo yake Chelsea walikuwa wanapoteza mipira kirahisi . ....

Kwanini Spurs walishindwa kutumia hiyo faida kipindi cha kwanza ?? Tunaamini hakuna mtu mmoja anaweza kuzuia peke yake ... lakini Thiago Silva alikuwa daraja la pekee yake, alinusa hatari vizuri kuondoa mipira, alifika kwenye mwili wa Kane na Son pale alipotakiwa na aliondoa presha kwa kuchukua mipira kwa Kepa kuanzisha mashambulizi kwa mipira mirefu ili kukabiliana na press ya Spurs .

Kipindi cha pili Thomas Tuchel alijibu mapigo kuingia kwa Kante kuliongeza idadi ya viungo kwa Chelsea ili kukabiliana na namba ya Spurs ...lakini Kante alichofanya ni kuomba mipira nyuma ya safu ya kiungo ya Spurs ...lakini sio katikati bali kulia na kushoto kwa Pierre na hapo shida ndio ilianza kwasababu Alli harudi nyuma wala Lo Celso wala Ndombele . Kante alikuwa nusu kiungo mshambuliaji na nusu kiungo wa kati ( katika hali mbili Chelsea wakiwa na mpira na bila mpira ) .

Hii ni mechi ambayo pia Santo angetamani kuwa na Lucas Moura ...mchezaji ambaye anaweza kukimbia na mpira lakini pia anaweza kushambulia " space " nyuma ya viungo . Ndombele , Lo Celso na Alli wote kipindi cha pili walikuwa wanacheza mbele ya viungo wa Chelsea kitu ambacho rahisi kukabiliana nacho
NOTE
1: Muundo wa uzuiaji wa Chelsea ni hatari upo imara sana hasa wakipoteza mpira ...kila mchezaji anajua nini cha kufanya
2: Harry Kane ndio maana alitaka kuondoka Spurs ...sasa hivi anatamani angekuwa jezi ya Blue ( Chelsea ) au Blue bahari ( City )
3: Uimara wa Chelsea unaokoa kiwango cha chini cha Mount, Havertz, Ziyech
4: Thiago Silva ...umri ni namba tu , kwangu mimi ndio Man of the Match

5: ATAKAYEMALIZA JUU YA CHELSEA NI BINGWA .....CHELSEA NI BEST TEAM IN THE LAND




Hands up
