Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Hawa liverkuku wapo serious aisee. Huyu ni kwenda naye jino kwa jino tusipoteze mechi kizembe

Nyumbu wanatania/masihara mengi Kwenye kupambania ubingwa

City hayuko tayari kutetea ubingwa
Hata mimi nimwewaona hizo timu za Manchester msimu huu hawatakuwa na consistency na hivyo Chelsea ikimaintain consistency tutakula sahaniu moja na Liver hadi achoke
 
Hawa liverkuku wapo serious aisee. Huyu ni kwenda naye jino kwa jino tusipoteze mechi kizembe

Nyumbu wanatania/masihara mengi Kwenye kupambania ubingwa

City hayuko tayari kutetea ubingwa
Mapema sana kumuhukumu City maana hata mwaka jana alianza vibaya hivyo hivyo lakini alipoanza kukaza mguu kwa mguu hakupoteza chochote zaidi ya kuchukua ubingwa wa EPL.
 
Sawa Chief ila mwaka jana timu nyingi za TOP 4 zilikuwa hoiii, Liverkuku majeruhi kibao tangu msimu unaanza.

Kwa sisi pale tunapotakiwa tushinde mechi moja tuongeze ligi tunafanya kinyume chake tunapoteza mechi mfulilizo. Tulimpa city gap kubwa sana la kujiimarisha

Kwa nyumbu kama kawaida masihara mengi tangu msimu unaanza.

Msimu huu Liverkuku na sisi tumejipanga vema kuanzia mwanzo sioni tukitoa gap la kupoteza mechi kizembe mfululizo.

City ajipange haswa msimu huu hakuna gap la dezo dezo
Ni sawa kabisa Kaka, nami natamani sana iwe hivyo ili Chelsea iendelee kuwa timu tishio duniani kote.

Tatizo mpira huwa unadunda Chifu.

Hivi uliona ile mechi tuliyocheza na Aston Villa ilivyokuwa ngumu sana kwetu?

Unajua hadi 90 kipenga cha mwisho Chelsea tulipata shuti 1 tu golini mwa Aston Villa ambapo Lukaku aliitumia nafasi hiyo hiyo toka kwa krosi ya Azpilicueta?

Unadhani kwanini mwaka huu timu yetu imekuwa ikitengeneza nafasi chache sana za kufunga magoli ktk EPL tofauti na mwaka jana?
 
Ni sawa kabisa Kaka, nami natamani sana iwe hivyo ili Chelsea iendelee kuwa timu tishio duniani kote.

Tatizo mpira huwa unadunda Chifu.

Hivi uliona ile mechi tuliyocheza na Aston Villa ilivyokuwa ngumu sana kwetu?

Unajua hadi 90 kipenga cha mwisho Chelsea tulipata shuti 1 tu golini mwa Aston Villa ambapo Lukaku aliitumia nafasi hiyo hiyo toka kwa krosi ya Azpilicueta?

Unadhani kwanini mwaka huu timu yetu imekuwa ikitengeneza nafasi chache sana za kufunga magoli ktk EPL tofauti na mwaka jana?
Are you sure unaongelea match ya Aston Villa?
 
Jana ungepigwa tu mande maana tishakuchoka.

Na Jmosi ijayo tunakupiga mande ili upotee kabisa humu.
Man City ina fan base ndogo sana, tumvumilie tu hivyo hivyo japo kinafki maana kule kwenye uzi wao hauna wapenzi, wachambuzi wa mpira wala wanaoipenda Man City kindaki ndaki zaidi ya wanaocheza kamali ya mikeka tu...
 
Kuhusu kutengeneza nafasi chache za kufunga jibu ni kwamba pale mbele kuna uzembe au ubinafsi unaanza kutamalaki.

Kabla ya Lukaku kuja pale mbele vijana walikuwa wanapambana haswa kufunga na kutoa assists, kosa kosa za kumwaga

Huyu Mount wa sasa ni tofauti na Mount wa msimu ulioisha, Werner amepunguziwa dakika za kucheza ule utengenezaji wake wa nafasi za kufunga upo benchi, Pulisic spana mkononi, Ziyech anajulikana ni pure selfishness

Chief ujio wa Lukaku kuna watu wanategea pale mbele, wamemtwisha Lukaku mzigo wote. Mount, Ziyech hawawajibiki kumtengenezea Lukaku magoli

Ukiangalia magoli aliyofunga Lukaku hakuna assists hata moja kutoka pale mbele (Ziyech, Mount, Kai).

Pale mbele kuna tatizo kubwa sana, Pulisic angekuwa full fit, Ziyech ni benchi na auzwe kabisa dirisha lijalo.

TT amrudishe Werner 1st eleven atamsaidia sana Lukaku.
"TT amrudishe Timo Werner 1st eleven atamsaidia sana Lulaku"

Nimekubaliana nawe, pia Ziyech awe anatokea benchi ikiwa timu imeshapata matokeo.
 
Au unaongelea Zenit?
Hata ile ya Aston Villa pia tulibanwa zaidi ya kutumia uzoefu tu kama sikosei, Chelsea sasa hivi tunakosa maelewano mazuri ya kutengeneza pasi za mwisho pale mbele.

Yani mwaka jana tulitengeneza nafasi nyingi sana mfungaji hakuwepo, ila mwaka huu ni kinyume kabisa na nilivyokuwa natarajia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom