Ndio maana timu kubwa kama Chelsea inatakiwa kuwa na timu A na B zenye uwezo unaofanana, timu C ndio iwe ya Karabao cup NK
Kumbuka pia sio wachezaji wote wanaochoka, mimi naona kuanzia mabeki wa pembeni, viungo na washambuliaji ndio wanaochoka kwa sababu wanakuwa busy sana kila saa, Kipa na CB wanaweza wakawa walewale. Kwa hiyo TT anaweza kuwarotate wachezaji wanaoonekana wamechoka au kufululiza kucheza sana kama jana alivyofanya kwa Mount, Benchilwell, Havertz na Silva hata benchi hawakuwekwa
Kwa rotation hii timu inakuwa fresh kila mechi
Zimebaki za ligi tatu tu, hiyo ya Leicester city ni mechi ndogo kwa sababu LCFC hawana timu pana na wataingiza wacheza wamechoka na kuwa na confusion kubwa kwa sababu ya kutolewa top 4 na hivyo tutajipigia kirahisi tu. Mechi na City UCL wataingia wakiwa na hofu ya kufungwa mechi mbili mfululizo na sisi tutaingia tukiwa na confidence na uchu wa kunyanyua Ndoo kubwa yenye heshima Ulaya ambayo akina Bayern, Real Madrid, PSG na wao City wanaimezea mate