Mkuu timu kubwa kama Chelsea haina muda wa kumsubiri mchezaji azoee. Italeta maumi makubwa kwenye timu. Njia pekee ya kumvumilia mchezaji kwenye klabu kama Chelsea ni kumtoa kwenye mkopo ilapate mechi nyingi akomae. Mchezaji mwingine form yake haipandi kabisa EPL hata ukimsubiri misimu miwili mitatu. Kuna wachezaji wengine wanang'ara tu kwenye ligi ndogo, akija EPL anakufa kabisa. Kuna wachezaji wengine wangebaki Chelsea wasingeng'ara ila kwa sababu walidharauliwa ndio maana wakapambana ili kuoesha kuwa wanaweza. Mmoja wa hao wachezaji ni Mo Salah. Mo Salah alioshawahi kukiri mwanzoni tu baada ya Liverpool kumsajili kuwa aliamua kujituma zaidi awapo uwanjani ili kumuonyesha MOU na Bodi ya Chelsea kuwa anaweza. Tunahitaji kwa ufupi wachezaji wanaopaa kwenye form kama akina Mount, Reece James, Promising Billy Gilmour. Lakini wachezaji kama RLC anaweza kuwa hot cake lakini yuko slow kwenye kupandisha form. asili ya Chelsea inahitaji wachezaji kama akina Ronaldo, Kante, Ziyech, sio hao wanaokua taratibu wakati timu zingine kama akina Liverpool, Man city na wengineo wanakimbia. UKWELI NDIO HUO, tunahitaji wachezaji wanaopaa kwa kukua. Muda mfupi ujao sitashangaa nikiwaona akina Werner, Havertz wakiuzwa Genoa ya Serie A au Monaco ya Ligue 1. Na pia sitashangaa Tammy Abraham akitolewa mkopo Championship. Kocha akiwang'ang'ania ataondoka nao