Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Huyo jamaa yenu toka asaini mkataba mpya kashuka kiwango mpaka huruma.

Bora ww kule jukwaani kwenu unaonekana sio kama wale waropokaji wamekimbia kabisa.
Mi siamini kama kusaini mkataba ndiyo kumesababisha. January transfer window itatupa majibu, kwa sasa Arsenal ifanye mpango wa kujishikilia tu kama kocha alivyosema.
 
Nyie jamaa naona mnatutia jambajamba kwenye ubingwa.

Hivi Timo ana shida gani? Maana nashindwa kumwelewa kabisa makosa yake.

Jana mmecheza game kali sana; Kante, Zouma, Ziyech, Pulisic, James (awesome), Giroud! Mlinipunja siku ya game ya Tottenham, ila jana mmenipa zaidi ya nilicholipia.
I think timmo needs physiological therapy
 
Waza kibarua chako na watukufu mbwa mwitu wolves...maana km desturi ya EPL hamna kubwa jinga aliyepatikana mpk sasa wiki hii mmebaki nyie na spurs(wale wengine midtable team)

Nikiwaga na mechi Anfield by default ni points 3.

Kwa hiyo tushamaliza hiyo.
 
CHELSEA 3-1 LEEDS UNITED, Premier League: Post-match reaction

By Mlanzi

Olivier Jonathan Giroud, Kurt Happy Zouma Pamoja na Christian Mate Pulisic kwa pamoja wamekamilisha comeback na kuipa Chelsea ushindi Mbele ya Mashabiki wapatao 2,000 katika Dimba hatari kuliko Madimba yote duniani, nalizingumzia Dimba la Stamford Bridge.

Makosa madogo kutokea dimba la kati yalimpa nafasi Patrick Bamford kuipatia Leeds United bao la kwanza kabla ya ile clinical finish kutoka kwa Olivier Jonathan Giroud dakika ya 27 akipokea assist kutoka kwa Reece James.

Kabla nisahau! Kina kitu sijakipenda kutoka kwa Mashabiki walipokuwa wakisema "TAKE A STAND AND BOO THE KNEE. WE ENGLISH DON'T KNEEL FOR CRIMINALS" haya maneno ni ya kibaguzi na hayana nafasi katika soccer!

Ukiachana na performance ya team, kuna ukomavu unazidi kujengeka unaoifanya team yetu iwe tushio...!! Ile Character ya team pindi inaporuhusu bao la mapema. Team inapambana kupata come back na ushindi Juu. Kwa mfano, hii game dhidi ya Leeds, Game dhidi ya WBA nk. Hii ndiyo proper energy itakayotupeleka mbali.

Katika hii game Manager Frank Lampard alikuwa amepanga kikosi bora kabisa kwa upande wangu ! Kikosi kilichokuwa na veteran Olivier Jonathan Giroud kuanza mbele ya Tammy Abraham. Nina uhakika Jibu litapatikana hivi karibuni la nani aanze mbele ya nanini na wakati gani sub zifanyike.

Timo Werner asipokufunga basi atafanya assist..!! Hebu check ile pace na assist yake dakika ya 93!!!! Mabepari wanaita brilliant. Baada ya kurejea kutoka half time, turning point ilikuja kupitia corner kick, ambapo Mason Mount alim-assist Kurt Happy Zouma dakika ya 62.

Pongenzi kwa goalkeeper wa Leeds Meslier kwa kuokoa rundo la mashambulizi kutoka kwa Timo Werner Pamoja na Mason Mount. Bao la tatu lilikuja Kutoka kwa Christian Mate Pulisic dakika ya 90+3 Akipokea assist kutoka kwa Timo Werner.

Subs zetu ZIlikuwa Christian Pulisic akimtoa Hakim Ziyech, Huku Mateo Kovacic akiingia upande wa Kai Havertz na Tammy Abraham upande wa Olivier Jonathan Giroud.

Next up: Tutawakaribisha Krasnodar pale pale Stamford Bridge katika Champions League group stage.

KTBFFH!
Huyu mwamba naukubali yupo fb
 
Pale England ni mashabiki wa Chelsea ndio wanaongoza kwa ukorofi, hawa jamaa ni wakorofi tena hasa. Fuatilia matukio yao utaelewa tu huwa wanafoka sana uwanjani. Na wanaongoza kupigwa Ban kisa matukio yao.

Ata ushindi wa jana mashabiki wamehusika kwa namna moja ama nyingine, wale walikuwa ni 2,000 tu, sasa jiulize wangejaza uwanja. Kuna kipindi niliona wanamfokea lefa sijui nani alichezewa rafu akashindwa kutoa kadi.

Yule beki wa Leeds Llorente sijajua ni kwann walikuwa wanamzomea kila akipata mpira.
Mashabiki kea kiasi kikubwa wamechangia ushindi wetu nimependa namna walivyokudanganya wanafoka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom