Mara nyingi wachezaji wanaomudu nafasi nyingi huwa wanahamishwa hamishwa mara kwa mara na kocha kulingana na uhitaji wa nafasi hizo
Mfano kabla Pulisic hajaanza kucheza vizuri Mount alikuwa akicheza left winger na alicheza vizuri, Pulisic alipopanda form, Mount akawa anachezeshwa kiungo wa kushoto au kulia na mara chache winger wa kulia
Havertz alishakiri mwenyewe kuwa anategemea siku moja atacheza wide winger wa kushoto
Werner alishasema nae anapenda kucheza mpira, mchezaji mshambuliaji akikuambia anataka kucheza mpira maana yake anapenda aidha kucheza kiungo au wide winger no. 10. Kwa maneno haya Timo hapendi kucheza kama striker, sijui kwa nini analazimishwa. Hata uchezaji wake wa leo kama mumemfuatilia alikuwa anacheza mara nyingi katikati ya uwanja , anarudi nyuma kuja kuchuklua mipira tofauti na Tamy au Giroud
Hata Hazard alipoikuwa akihojiwa mara kwa mara alikuwa akisema hivyo hivyo kuwa anapenda kucheza mpira, anapenda kukaa na mpira
Ukiwa striker huwezi kucheza mpira kwa sababu utakuwa unasubiri tu upikiwe
Mimi nashangaa watu wanaongea sana kuwazidi wachezaji wenyewe