Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Kwa kufanya hivyo anamkosea heshima Pedro kwani huyo odoi yupo Chelsea Huu msimu wa ngapi? Je unaamini kuja kwa Ziyech na kubaki kwa Willian ndio kutamfanya odoi apate time playing? Pedro ameperform vizuri Sana tangu aje Chelsea na kashinda makombe na still yupo vizuri mpaka leo Kuna aja gani kumpiga benchi mpaka game za mwisho?
Siyo kumkosea heshima. Anafanya ivyo kwa manufaa ya baadae ili kuwapa mwanga hawa madogo. Kwenye mpira siku zote lazima uzipe nafasi damu changa kwanza kabla ya kufikiria wakubwa ambao jua lishaanza kuzama.
 
Naangalia play off kati ya Brentford na Swansea
niseme tu huyu Saïd Benrahma anayetajwa Chelsea wanamfukuzia ni zinga la winga sio size ya Championship
kwa jinsi wanavyocheza Brentford watakuja EPL msimu huu for sure
 
lembu Kwa hiyo kwako wewe odoi Ni better than Pedro?Pedro ajafika stage kutomweka kabisa hata kwenye sub Kama issue ni consistence Abraham game ngapi kaboronga mbona still akawa first eleven baadae kidogo Tena mwishoni ndio Lampard akamgeukia Giroud hata mount mwenyewe game nyingi tu kachemka na still akawa anamuamini kwa Nini isiwe kwa Pedro?
Mimi siko kwenye comparability, Odoi anakua na Pedro ana fade out of football career. hata hivyo Odoi sio first choice ndio maana Ziyech Havertz wanasajiliwa. hata mimi ningepewa nichague sub ya kudumu kati ya Odoi na Pedro ningemchagua Odoi kwa sababu ya umri na sio nani bora kuliko mwingine
 
Ampadu hakunyimwa nafasi mkuu kwa sababu ya mkopo, totally hakufit in kwenye timu kocha anataka kuijenga. Masharti ya mkopo huwa inaendana na kununua kabisa kama mchezaji anafaa, ukiona timu inamkataa mchezaji wa mkopo ni kwa sababu hatafit kama wao wanavyotaka
Ampadu badio ana safari ndefu kama anataka kucheza timu kubwa ligi kubwa Ulaya
Mkuu mbona unachoeleza hakina utofauti na nilichosema. Kocha aliona hana mpango nae kabisa kama ni mfumo dogo anacheza CM au sometimes CB na huo mfumo ana umudu vyema. Shida ni kwamba hakuweza kumpa nafasi mchezaji ambaye anajua ni wa mpito hawana hakika kama anaweza kuwa sehemu ya kikosi chake.
 
Naangalia play off kati ya Brentford na Swansea
niseme tu huyu Saïd Benrahma anayetajwa Chelsea wanamfukuzia ni zinga la winga sio size ya Championship
kwa jinsi wanavyocheza Brentford watakuja EPL msimu huu for sure
Huyo jamaa ni noma mkuu
 
Katika wachezaji ambao nina mashaka nao ni huyu havertez... Nahs anaweza ku flop pale wingereza.. Nimechk clip zake u tube nimeona wa kawaida sana, japo u tube sio sehemu nzuri ya kumtwzama mchezaji..( maoni yangu tu )
 
Fabrizio Romano
Screenshot_20200730-030938.jpg
 
Katika wachezaji ambao nina mashaka nao ni huyu havertez... Nahs anaweza ku flop pale wingereza.. Nimechk clip zake u tube nimeona wa kawaida sana, japo u tube sio sehemu nzuri ya kumtwzama mchezaji..( maoni yangu tu )
Usajili wowote ni kamari. Board imeshafanya mahesabu yake mpska kufikia uamuzi wa kumtaka. Tumtakie kheri tu awe kiwembe
 
Mchakato wa Usajili ni mahesabu, inategemea Chelsea inapiga hesabu gani kwa sasa. Mfano:-

1. kumsajili matured HARVETZ kwa €80M au
2. Kusajili wachezaji wawili au watatu wanaocheza nafasi ya Harvetz kwa jumla ya €80M na kocha akaimprove vipaji vyao kufikia level ya Harvetz.

Tunatakiwa tujiulize maswali haya tumetoa £58M kwa Pulisic, tumetoa £48M kwa WERNER, tumetoa £44M kwa Ziyech

Swali kwanini tutuoe £80M kwa Harvetz? Na sio kwa kiasi hicho kwa wachezaji wawili? Sababu ni zipi?

Kiwango bora sana cha Harvetz?

Shinikizo la kocha anamtaka?

Shinikizo la Marina anamtaka?

Shinikizo la Roman anamtaka?

Recommendations za scouting team?
Mimi upande wangu dogo naon sio mzuri kivile ukilinganish na bei ake
Kinachomfavour anaweza cheza kama kiungo thus y lampard anamtaka
 
Mimi upande wangu dogo naon sio mzuri kivile ukilinganish na bei ake
Kinachomfavour anaweza cheza kama kiungo thus y lampard anamtaka
Hatuna creative midfielder since fabregas aondoke, kama yupo sokoni tumnunue tu hela zenyewe hatutoi mkuu, soko LA wachezaji lishavurugwa kama kuna timu imetoa hiyohiyo 80m kumnunua Maguire...
 
Ila kwa hela io uero100 ni kubwa sana apo tunapigwa
Mkuu huyu mchezaji nimeanza kumfuatilia toka msimu uliopita kesha prove kitambo ni promising player. Sisi tutabaki kusema tunapigwa lakini hakuna tunachoweza kufanya kubadili kinachoendelea kwa sasa.

Tuheshimu tu maamuzi ya bodi sijui kwa nini wachezaji wadogo hivi wanakua wanauzwa bei kubwa.
 
Siyo kumkosea heshima. Anafanya ivyo kwa manufaa ya baadae ili kuwapa mwanga hawa madogo. Kwenye mpira siku zote lazima uzipe nafasi damu changa kwanza kabla ya kufikiria wakubwa ambao jua lishaanza kuzama.
Ndo maana nimekuuliza kuja kwa Ziyech na willian kubaki ndio kutafanya huyo odoi kupata time playing?mbona hili swali limekuwa ngumu kujibu
 
Ndo maana nimekuuliza kuja kwa Ziyech na willian kubaki ndio kutafanya huyo odoi kupata time playing?mbona hili swali limekuwa ngumu kujibu
Amini nikwambiavyo Odoi ana nafasi kubwa ya kuwa regular starter chini ya Lampard hata kama Willian akiendelea kuwepo. Lampard anajenga timu ya vijana wataotengeneza chemistry nzuri ndani ya muda mfupi Willian hawezi kuwa sehemu ya 1st eleven ya Lampard.

Pia ujio wa Ziyech hauwezi zuia nafasi ya Odoi kwa sababu mechi ni nyingi pia kuna kuumia na kadhalika bado Odoi ana nafasi kikubwa tu aendelee kujituma. Nakumbuka hata kipindi Mahrez anasajiliwa na Pep watu wakasema anaenda kupotea na kipindi hicho B. Silva alikua moto lakini Mahrez aliendelea kujituma na mpaka leo wanacheza wote kwa mafanikio tu.
 
Amini nikwambiavyo Odoi ana nafasi kubwa ya kuwa regular starter chini ya Lampard hata kama Willian akiendelea kuwepo. Lampard anajenga timu ya vijana wataotengeneza chemistry nzuri ndani ya muda mfupi Willian hawezi kuwa sehemu ya 1st eleven ya Lampard.

Pia ujio wa Ziyech hauwezi zuia nafasi ya Odoi kwa sababu mechi ni nyingi pia kuna kuumia na kadhalika bado Odoi ana nafasi kikubwa tu aendelee kujituma. Nakumbuka hata kipindi Mahrez anasajiliwa na Pep watu wakasema anaenda kupotea na kipindi hicho B. Silva alikua moto lakini Mahrez aliendelea kujituma na mpaka leo wanacheza wote kwa mafanikio tu.
Shida n kuwajenga katika upendo like auba na laca
 
Odoi ni wastage of time. Nafasi hiyo ya RW ni Ziyech na willan kama atabaki. Odoi asubirie FA na CARABAO
Ndg, Odoi kwa uchezaji wake atakuja kuwa very dangerous winga. Utoto unamzuia kwa sasa kwenye baadhi ya maeneo hasa ya kinidhamu. Juzi alipoingia kwenye mechi ya Liverpool alicheza vizuri sana zile papara papara za kutotulia na mpira ameanza kuziacha. Makocha wanaona kuliko sisi. Bayern waliona future ya Odoi kuliko present yake. Present ya Odoi haiwafai wale wanaopenda ready-made. Ila kama una jicho la kesho ya Odoi ni nzuri sana. Odoi anaweza kuwa sub msimu mmoja tu. Nakuapia kuanzia 2021/22 Odoi kama hatasumbuliwa na long-term injury atakuwa kwenye first 11 ya kocha. Weka hii kumbukumbu. Tukimruhusu Odoi aondoke kwa sababu tu tunawataka ready made kama wanavyofanya Manure, Real madrid na timu zingine kubwa tutakuja juta. Hawa vijana wote, Pulisic, Mount, Tammy, Gilmour, Tomori, Reece ni bunduki za kesho tutazihitaji sana
Ila kama tunataka matokeo ya haraka, let us sign ready made tallents, wengi wao wana umri mkubwa kama akina Oblak, Hata Ronaldo tumsajili na tuwaachie akina Odoi waondoke, lakini tutakuwa tunabomoa nyumba badala ya kujenga
 
Nimekuelewa ndugu, hatuwatengi wala hatuwachukii hawa madogo wa academy. Tunachotaka waheshimu jezi ya Chelsea, wajitambue na wafocus kwenye kujenga career na brand zao.

James, Mount, Glimour, Tomori hawa ni vema

Odoi, Tammy, RLC hawa wamechagua kula mshahara bure

Yaani Tammy angekuwa determined kama Giroud basi angekuwa mbali sana. Pulisic yuko determined ndio maana matunda yake yanaonekana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom