Nilichogundua jana ukiweka mbali mfumo na mbinu za Lampard, kilichotupa ushindi ni quality ya mchezaji mmoja mmoja.
Hii quality ndio huwa tunaikosa kupelekea kufungwa, ule uchezaji wa jana ukiambiwa ni ile Chelsea dhaifu usingeamini kabisa.
MABEKI:- Angalia beki jana walivyojipanga, walivyokuwa organized, walivyokuwa wanacheza kwa kujituma na sio kukabia kwa macho. Ule unaitwa ulinzi shirikishi.
ZOUMA:- pale katikati alihakikisha hakuna kinachokatiza. Matial mfukoni hakuwepo uwanjani
ALONSO:- nilichogundua huyu jamaa sio mchezaji wa kucheza mechi nyingi mfululizo, huwa akirudi mapumzikoni what a player.
JAMES:- Huyu jamaa userious wake jana umeniogopesha control ya hali ya juu, ana nguvu na hachoki kupanda. Rashfod mfukoni jana hakuwepo uwanjani
CAPTAIN:- What a performance
VIUNGO:- Bruno alikuwepo uwanjani? Yah nilimuona kwenye kupiga penati.
KOVACIC:- Huyu ni mchezaji wa mechi kubwa, zile mechi ndogo ndogo tuwe tunampumzisha asikidhalilishe kiwango chake kikubwa. Jana what a perfomance, alicharuka sana pale katikati pakawa moto
JOGINHO:- Jana umeninyamazisha uvivu na uzembe haukuwepo huyu ndio Jognho tunayemtaka Chelsea, kasi kwenye kukaba na kupora mipira, pass za haraka. Kiufupi alikamata katikati, Matic alikuwepo?
FORWARD:- Hapa sasa ndio ushindi ulikuwepo (MOUNT, GIROUD, WILLAN), kazi ya kwanza ilikuwa kukabia juu kuhakikisha manyumbu hawaanzishi mashambulizi kutokea nyuma, walihakikisha mabeki wanajichanganya kuanzisha mpira, wanafanya makosa na kuwaadhibu kwa makosa yao.
LAMPARD:- Nilivyomsoma jana mechi alishaimaliza uwanja wa mazoezi. Jana ilikuwa wachezaji kutekeleza maelekezo yake. Hongera Lampard.
Nimemuongelea mchezaji mmoja mmoja kwa sababu jana kila mchezaji ameonyesha quality ya hali ya juu. Kila mchezaji alionekana nini anatakiwa akifanye uwanjani.
Changamoto iliyobaki sasa ni Kuipata tena ile quality ya wachezaji jana kwa mechi zilizobaki.
SUB:- LFC alipaform vizuri sana alitoa pass kwa haraka na kuhakikisha mashambulizi yanaendelea kupamba moto.
ODOI & PEDRO:- Safii walihakikisha mashambulizi hakuna kupoa mayumbu washindwe kupanda juu.
ABRAHAM:- Huyu alistahili abaki uwanja wa mazoezi aendelee na mazoezi binafsi.
HONGERENI SANA WANABLUES KWA KUTINGA FAINALI, POLENI KWA KELELE ZA MANYUMBU KABLA YA MECHI.