Kwanza umekosa like yangu sababu ya neno nyumbu, japo umeongea point
Pamoja na Chelsix kuonekana ni underdog kwenye mechi ya kesho lakini kuna mambo mengi sana bado hayapo dhahiri
Mfano Man Utd ambayo inazipa nafasi kubwa sana mbio za top 4, tarehe 13 wamecheza game ngumu na Sotton, ikafuata game nyingine ngumu ya Palace tarehe 16, halafu baada ya siku 3 baadae inakutana tena na Chelsea huku ikiwaza game yake muhimu sana ya Westham tarehe 22. Nimeongea hayo kukupa picha kwamba mechi zinafulizana sana, wachezaji wanachoka huku kila siku wakikutana na mechi ngumu.
Kwa upande wa Chelsea japo mechi hazijafululizana sana kama za Man Utd kabla ya mechi yao, lakini baada ya mechi ya United Chelsea ana kibarua kizito sana cha kwenye mbio za top 4. Baada ya kucheza na United, Chelsea atakutana na Liverpool moja kati ya mechi muhimu sana msimu huu kwake. Kwahiyo top 4 race ita determine vikosi vya kesho.
Nakukumbusha tu, Chelsea akipigwa na Liverpool, halafu United akishinda dhidi ya Westham na Leicester ashinde dhidi ya Spurs, mechi ya mwisho United na Leicester wanaweza kucheza kutafuta draw ili waingie top 4. Ili hiyo draw isiwasaidie Utd na Leicester, Chelsea anapaswa kuifunga Wolves goli 15 - 0
Kutokana na hali hiyo niliyoielezea hapo juu, sitashangaa kuona Utd na Chelsea wakichezesha wachezaji wa kikosi cha pili ili kujiimarisha zaidi kwenye top 4 race.
Endapo kocha mmoja hatajali mambo ya top 4 race na mwingine akijali, yule anayejali zaidi anaweza kupoteza mechi ya kesho.
LAMPARD alichosema ni kweli kabisa. Manyumbu kwa sasa mko form baraa, hii chelsea tunaingia kama underdog kwa sababu ya madhaifu makubwa timu tuliyonayo kwa sasa (beki ovyo, ushambuliaji butu, viungo nyanya).
Sisi kuwafunga nyie inategemea na madudu mtakayofanya uwanjani, tutatumia makosa yenu kama fursa kwetu kuwaadhibu. Fursa moja wapo pia ni De gea