Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Tatizo pia ni kocha, hapo watakuja hao akina werner na ziyech, kiungo akawe barkley. nao wakina wener wataanza kuonekana hawajui, mwisho wa siku na comfidence inapotea wanakua akina batshuay wazungu.
 
Waungwana kama mjuavyo kule nyuma sio kuzuri kabisa, twende na nani kati ya Ibrahima Konate, Dayot Upamecano ama Pau Torres au tuchukue wote watatu tuwe na ukuta hatari dunia nzima. Napenda kusikia mawazo yenu wana blues wenzangu, KTBFFH
Hili peleka kwenye board maana hapa mtapigizana kelele alafu hamna hata mbuni.
 
Kujadili mchezaji mmoja mmoja tutakesha kubishana. Kila shabiki kuna mchezaji ambaye anampenda kwa sababu zake binafsi either kwa muonekano wa mchezaji au uchezaji wake.

Kuna mashabiki wa Barkely hapa huwaambii kitu kuhusu hii mashine yao ya kazi.

Kuna mashabiki hapa wanampenda Abraham, ndio striker wao bora, wanahisi kutofunga magoli ni kwamba anahujumiwa hapewi pasi za kufunga, pia hapewi penati za kupiga.

mashabiki hapa wanampenda Abraham, ndio striker wao bora, wanahisi kutofunga magoli ni kwamba anahujumiwa hapewi pasi za kufunga, pia hapewi penati za kupiga.
😂😂😂😂😂😂
 
Tena ishia hapo hapo hiyo kenge takataka inajiita Abraham anahujumiwa na nani.?? Yeye mwenyewe ndio anajihujumu hapaswi kuwa kwenye klabu kubwa kama Chelsea, hiyo takataka si ndio ilikosa penalti ya mwisho kwenye kombe la Super cup.
kwahiyo mtu akikosa penati anakuwa hajui! Washabiki wa haka katimu ndio mnakafanya kaendelee kuwa katimu kadogo hapo Epl kwani mna utoto mwingi.
 
Ukiondoa mechi za Mancity dhidi ya Aston villa na Watford ambazo Mancity ilishinda 8-0 na 6-1, Chelsea ndio timu inayoongoza EPL kwa kuwa na magoli mengi ya kufunga kwa mechi moja ikiwa na average ya 3.16 per match na ukiweka hizo mechi mbili nilizozitaja ndipo Mancity inakuja ya kwanza, Chelsea ya pili. Kilichotuangusha ni kufungwa magoli. Tunazo clean sheet chache sana

Chelsea ni ya 15 kwa clean sheet (7)- too bad
Chelsea ni ya 3 kwa kushinda mechi (17) mbele ni Man city (21) na Liverpool (29) tu
Chelsea ni ya 4 kwa kufunga magoli 60, walio mbele ni Leicester city (63), Liverpool (72) na Man city (81)
Unaona kinachotuangusha ni kufungwa tu, hata mechi nyingi tulizoshinda tulifungwa magoli kadhaa
Katika mechi 17 tulizoshinda 10 tumefungwa hata kama tulitoka na point 3 zote
Kwa maelezo haya mafupi, uwezo wa kufunga tunao, wakiongezeka akina Ziyech na Werner ndio itakuwa hatari
Tatizo kubwa ni kujilinda na nashangaa mpaka sasa hivi hatujalishughulikia hilo tatizo. Ndio maana naungana na wanaosema dili la Havertz liwekwe kando kwanza, tuwalete akina LB kama Ben Chilwell au Álex Grimaldo, au CB kama akina Upamecano, Konate, Alex Telles ana miaka 27, kuwa na senious wengi kwenye timu sio afya, Azpi anatosha kuwapa uzoefu akina James na watakaokuja. Hata Alonso akibaki atasaidia.
 
Lampard amuanzishe leo jorginho uzoefu wake utatubeba leo asijiroge akamchezesha gilmour atafanya kosa kubwa Sana
Cash Money Forever
Papaa Gx
lembu
Hilo liko wazi kabisa, nimeona Gilmour yuko bado ni too risky. Juzi Billy alipoingia badala ya Kante kuna mpira aliuzembea kidogo tufungwe kama sio umaridai wa Kepa na Zouma
 
kwahiyo mtu akikosa penati anakuwa hajui! Washabiki wa haka katimu ndio mnakafanya kaendelee kuwa katimu kadogo hapo Epl kwani mna utoto mwingi.
Mashabiki wengine hapa ni wa 2020, hata huko kwako Arsenal wako kama hao unaowasema, wakikosolewa ni matusi na kujifanya wao wanajua kuliko wengine
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom