View attachment 1499020
Hiki kilikuwa kikosi cha kwanza Liverpool miaka 4 iliyopita klop alipopewa kandarasi ya ukocha liver
Liverpool kupata mafanikio waliyopata sasa Takribani wachezaji 8 wa 1st eleven waliuzwa na Wachezaji 3 wamejeuka kuwa sub.
Kwa lampard Chelsea huu ndio kwanza msimu wake wa kwanza, tusitegemee mabadiliko ya kikosi chetu yatatokea ndani ya msimu ujao, bado tuna safari ndefu wazee.
Wachezaji hawa tulionao watatoka taratibu na wapya wataingia taratibu mpaka baadae tunajikuta tuna kikosi super cha kubeba makombe.
Tuweni wavumilivu wazee, najua inatuuma sana kuwa na kikosi cha moto baridi moto baridi, tumpe kocha muda asuke kikosi kipya.
Na nyota njema imeanza kuonekana asubuhi kwa usajili wa Werner na Ziyech na bila shaka dirisha hili la usajili pia tutasajili beki wa kushoto na beki wa kati.
Hawa watakuwa ingizo Jipya la wachezaji 4 kwenye 1st eleven, wachezaji wa zamani watabaki 7, january 2021 tukaingiza labda mmoja na dirisha kubwa lijalo tukaingiza labda 3 tayari kikosi kimeshakuwa na sura mpya kabisa.
Msimu wa 21/22 ni mwendo wa kukusanya vikombe bila huruma yoyote hakutakuwa na msalie mtume ni mwendo wa kutoa vipigo heavy