WEST HAM 3-2 CHELSEA, Premier League: Post-match reaction; player ratings
By Mlanzi
Kuna muda nilikosa amani kabisa especially upande wa defence yetu. Yes, ilikuwa London derby but kama tuliwafunga City iweje hawa

?
Ukuta wetu ulikuwa na matobo kibao. César Azpilicueta hakuwa vizuri, Antonio Rudiger hakuwa powa, Andreas Bødtker Christensen hakuwa kwenye form.
Inawezekana kabisa wachezaji wamechoka kutokana na congestion ya matches hivyo itoshe tu kusema hii ni sehemu ya mchezo. Bao la Andriy Yarmolenko dakika ya 90 ndilo limetunyima point katika hiyo London derby.
Pamoja na Chelsea kuanza vizuri ukilinganisha na weekend ilyopita, team ilikuwa iki-create chances kabla ya West Ham kuanza kuisakama defense yetu kwa mipira ya Juu. David Moyes alikuwa akitumia lowest possession tactics na kupoteza muda kama kawaida ya team yake kiasi kwamba Chelsea ilikuwa iki struggle kucheza katika kiwango chake.
Tatizo kubwa kwa Chelsea lilikuwa ni kushindwa kuzuia set pieces, especially corners kiasi kwamba Tomas Soucek alitupia mara mbili kwa mipira ya corners katika first-half japo bao mmoja lilikataliwa kwa kuwa alikuwa offside
Na katika hizo incidents mbili, Willian alitunyanyua katika viti baada ya kufunga kwa njia ya penalty mara baada ya Christian Pulisic kuangushwa ndani ya penalty box na Diop.
West Ham walifunga bao lao la pili kwenye second half kupitia kwa Michail Antonio
Chelsea made ilifanya mabadiliko na baadae Willian alifunga bao la kusawazisha kwa njia ya free kick. Wakati tukiamini kutoka na point japo moja Yarmolenko alifunga bao la tatu na la ushindi linalotusononesha mpaka sasa.
Frank Lampard alikuwa amemuacha Mason Mount pamoja na Jorginho kwenye bench, huku Ross Barkley sambamba na N'golo Kante pamoja na Mateo Kovacic wakianza katika dimba la kati. Christian Pulisic na Willian walikuwa mbele sambamba na Tammy Abraham.
Mason Mount aliingia upande wa Mateo Kovacic na Oliver Giroud upande wa Tammy Abraham na baadae Ruben Loftus-Cheek upande wa Ross Barkley.
Kutupia kwa Willian kunamfanya kuwa mchezaji wa kwanza katika PL history kufunga katika kila mwezi uliopo katika Callender.
Kwa matokeo haya Chelsea inabakia katika nafasi ya nne nyuma ya Leicester kwa tofauti ya points mbili na mbele ya Manchester United kwa tofauti ya points mbili
Next up: tutawakaribisha Watford siku ya Juma Mosi
KTBFFH