Shabiki asiyejua mpira utamjua tu kwa namna anavyodakia mada
Mchezaji kushuka kiwango ni jambo la kawaida wala sio la kushangaa na kuanza kutema maneno magumu
Tumeshuhudia mara nyingi hata wachezaji wa class ya juu kama akina Messi viwango vinapanda na kushuka
ukimchukulia mchezaji mmoja mmoja wa Chelsea hakuna hata mmoja ameenda mfululizo na kiwango kile kile, aidha safari hii imepanda au safari nyingine imeshuka, kuanzia kwa makipa, mabeki, viungo na washambuliaji. Sasa mimi leo kusema Reece James kiwango chake kimeshuka kidogo wala sio sana nashambuliwa sijui mpira
Na ndio maana mchezaji kama Alonso kiwango chake kilishuka muda mrefu tangu Enzi za Sarri mpaka Emerson akampiku, au tumeshasahau. Leo hii Alonso amekuwa hot cake kwa sababu kiwango chake kimepanda na cha Emerson kimeshuka. Muda mrefu kiwango cha Pedro kilishuka mpaka wengi humu tukasuggest aondoke muda wake ukiisha,, leo kiwango kimerudi maoni tofauti. Mount kiwango chake kinashuka kinapanda tena yeye ndio kiwango kinabadilika hapa na hapa. Tammy Abrahama alipokuwa anatumbukiza vizuri alisifiwa sana, leo form yake imedrop mpaka anaambiwa hajui mpira. Mimi naamini hakuna mchezaji ambaye yuko immune na kiwango kushuka au kupanda na kama yupo mniambie. Wanachotofautiana wachezaji kwenye viwango kushuka au kupanda ni
- Lini (When)
- Itachukua muda gani (How long) na
- Kiwango cha kushuka au kupanda (Degree of dipping)
Sasa hata Lampard aliyesema kiwango cha Reece kimeenda chini katika wiki za hivi karibuni hajui mpira??
Lampard anaendelea kusema kuwa hata Desemba mwaka jana kiwango cha Reece kilishuka kidogo akaamua kumpa break na kwa hiyo hata hii break ya sasa sio ngeni.
Reference hii hapa:
Lampard’s Reece James decision lost in Billy Gilmour hype