Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Tammy katika mechi 36 alizocheza msimu huu kafunga goli 16 ametoa assist 4 yaan amehusika katika magoli 20 na ana umri wa miaka 22. Sawa ndio anakosa nafasi nyingi anazopata lakini hana uwiano mbaya wa magoli nadhani ni swala la muda tu atakua sawa. Naye kama binadamu lazima awe na pressure ya kutegemewa hasa akiwa anaichezea timu kubwa kama Chelsea. Tumpe muda Tammy atazoea pressure na kikubwa ninaamini atakua bora zaidi ni kwa sababu yupo chini ya Frank Lampard.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Me nahisi tammy kajitahidi sana msimu huu coz ndio msim wake wa 1 na huenda akascore 20 goals in his 1st season katik premier league
Wakina morata,batshuay wote hawa wameshindwa

Striker atakaekuja labda aje kusaidiana na tammy, tuwe na striker ambao hata siku mmoja asipokuwepo mungine anacover nafasi yake vizuri

Mfano mzuri ni miaka ya nyuma wakat drogba alipokuwa afcon anelka alireplace nafasi yake vizur tu. Kuna mech unakuta unahitaj mastriker wote wawili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nafasi ngapi Abraham anakosaga? Au uangalii mwangalie game dhidi ya man city alipata nafasi mbili za wazi kakosa, Kuna game pia tulicheza na Liverpool Stamford bridge kakosa chance za wazi.Team kubwa Kama Chelsea haiwezi kumtegemea Abraham kuwa striker wao tegemezi
Kukosa ni jambo moja. Kama unafuatilia michezo yopte sio Chelsea tu, strikers wazuri wanakosa chances nyingi kuliko wanazofunga. kinachoangaliwa kwenye striker ni conversion rate
Ebu tuangalie hiyo conversion rate ya strikers
EPL
Jamie Vardy 69% - huyu ni counter attack strikers mara nyingi wanakuwa na touches chache kwa sababu ya nature ya uchezaji wao
Marcus Rashford 58% - kama Vardy hapo juu
Dany Ings 58% - kama hao wa juu
Tammy Abraham 56% - purely one touch football, touches kwenye box zinakuwa nyingi na hivyo shot golini zinakuwa nyingi likewise. Uchezaji wa nature hii strikers kuwa na accuracy percentage kubwa ni vigumu
Sergio Agüero 51% huyu nature ya uchezaji wa timu yake ni kama Chelsea
NJE YA EPL
LALIGA
Karim Benzema 51% uchezaji wao ni kama Chelsea - Box to box football

SERIE A
Ciro Immobile 62% - huyu ndie striker kwenye big legues aliyempita Abraham kwa goal acuracy
Romelu Lukaku 65% striker mwingine aliyempita kwa mbali Abraham

Budesliga
Robert Lewandowski - 58% pia huyu kampita Abraham kwa mazingira yanayofanana
Timo Werner 63% - na huyu pia kampita Tammy

Frech League One
Kylian Mbappé - 60% kamzidi pia
Mouser Dembele - 53% - huyu ni mojawapo ya target ya Chelsea kwenye ligi ndogo tu Abraham kampita mbali kwa accuracy na kwa assists

Kwa maelezo haya, Abraham anashutumiwa bure, yuko kwenye nafasi nzuri tu

Jambo lingine nilishasema huko nyuma Sio striker ndie peke yake anaamua timu kubeba makombe, ni safu nzima
Liverpool kwa mfano wako mbali sana kwa ufungaji na mechi walizoshinda lakini sio kwa sababu ya striker wao
Striker wa Liverpool mara nyingi ni Firmino ana magoli 8 na assists 7 accuracy 59%. Hii inaonyesha kuwa Liverpool hawamtegemei yeye tu kwenye kufunga
Mawinga kama akina Mane na Salah wanafunga. Viungo wanafunga
Ukija kwa Mancity ni hivyo hivyo hata kwenye misimu yote miwili waliochukua ubingwa hawakumtegemea striker pekee afunge
Chelsea tukikazania sana kusajili striker na kuondoa obligation za kufunga kwa wachezaji wengine kama viungo na wingers hatutaweza kuchukua kombe lolote.
Tunahitaji kutengeneza Chemistry ya timu nzima iwe na wachezaji wa kubeba makombe
Kipa awe ni caliber ya makombe
Mabeki wawe ni caliber ya kubeba makombe viungo hivyo hivyo

Tuache kuweka matumaini makubwa sana kwa striker kwa sababu hata Ciro Immobile akija Chelsea na kuwa na watoa huduma wavivu, wazembe na wasio kuwa wabunifu. Atashindwa kazi ile anayofanya Lazio
 
With modern football lazima timu iwe na options nyingi za kupata magoli. Mfano pale Liverpool; Firminho asipofunga basi Mane, au Salah, au Anord au Robertson watafunga.



Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo ya Option nimeelezea vizuri hapo juu ni kwamba watu wanatumia mioyo Zaidi ya akili kwenye kujudge. Mancity kuchukua ubingwa back to back, Aguero kawa mfungaji wa kawaida tu, magoli ambayo hata Tammy atafikia pamoja na Chelsea mbovu
Liverpool wanaendea kuchukua ubingwa wamechukua UEFA na sasa EPL, Firmino ambaye ndio striker wao tena mzuri ndio kwanza ana magoli 8 na hakuwa kuwa top scorer
Sayansi ya mpira hasa modern football watu hawajui jinsi inavyofanya kazi, Chemistry ya timu ndio inaamua ubingwa na sio umahiri wa one person
Ujio wa Ziyech na Sancho utaongeza orodha ya wafungaji na dependency ya striker itakuwa imeondoka. Na Abraham akiondolewa majuku mazito atakuwa mfungaji mzuri tu
 
Kumfananisha Tammy na firmino unakosea sana. Kule Liverpool wachezaji wamegawana magoal. Ndio maana inakuwa ni ngumu kumuona firmino ana goal nyingi.

Huyo Firmino ana goal 8 na assist 7, Salah ana goal 14 na assit 6 Pia Mane ana goal 12 na assist 6.

Sisi chelsea Baada ya Abraham goal 13 na assist 3 tu na anayefuata ni Pulisic ambaye ana goal 5 tu.

Hivi huoni tofauti hapo?

Sent using Jamii Forums mobile app
Na hicho ndicho kilichokosekana Chelsea. Hatuna wafungaji Zaidi ya Tammy na ndio maana tunamtafuta mchawi ambaye ni Tammy. Timu inayomtegemea mtu mmoja tu kwenye kufunga ni mbovu na huo ubovu ndio urekebishwe. Firmino ni striker kwa nini yeye asishutumiwe ana magoli machache kule Liverpool? badala yake wanamsifia ndie top player wao. Tujenge timu tuache kumshambulia Abraham. Tujenge kuanzia kwa Kipa, Mabeki, viungo, wingers na striker wa pili waje kushindana Chelsea yetu itakuwa bora
 
Mkuu Tammy anaonekana hivyo kwa sababu wachezaji wengine hawafumgi pia. Kumbuka hata Tammy anatoa pass kwa wengine wanashindwa kufunga. So cha msingi ni kuelewa ni swala la muda Tammy atakua vile mnataka awe. Subirini msimu ujao akipata mawing wa pembeni waliochangamka zaidi mtamshangaa

Sent using Jamii Forums mobile app
Nani kampa pasi kashindwa kufunga? Basi huyo mtu/tungemuona kwenye big chances missed.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili nmeshalielezea. Na reference yangu ilikuwa Liverpool.

Lyon Mousa Dembele anaongoza magoal kwa timu yake akiwa na magoal 13. Anayemuatia Ni Depay ana goal 9. Mpaka tayari kuna mgawanyiko wa kufunga magoal.

Njoo Chelsea. Anayeongoza ni Tammy ana goals 13 anayefuata na Pulisic ana goal 5. Unaiona tofauti iliyopo?

Lyon wapo nafasi ya 11 kwenye League yao wakati chelsea yupo nafasi ya nne. Lyon wana msimu mbaya.

Kuzibeba tu hizo namba na kuzileta hapa bila kuangalia parameters zingine unakosea....
Dembele mechi 23 league goli 13
Uefa mechi 6 no goal assist 1

Tammy 24 match goals 14 assist 3
Uefa 6. Goals 2


Kwa uwiano huo wote wanalingana so dembele uwezi sema atasolve scorring problem otherwise achukuliwe tomm werner sio dembele

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nani kampa pasi kashindwa kufunga? Basi huyo mtu/tungemuona kwenye big chances missed.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani mwenye jukumu lw kufunga ni Tamny peke yake? Hebu fikiria msimu wake wa kwanza kucgeza kama striker wa kutegemewa ame perform ivyo, jeakicheza pasipo na pressure huku mawings nao wakimsaidia kufunga unadhani atakuwaje?

Kila mwanadamu huwa anakosea na kuna muda game inakukataa lakini kiukweli mpaka sasa bado sijaona Tammy alipokosea.

Nakupa mfano Rashford naye kipindi anaanza Man U alikua na mistake za ovyo, anacheza mechi nyingi magoli machache sana lakini sa hivi huu ni msimu wake wa 4 angalia anavyo washa moto uko.

Judgement yenu ipo kwa kuangalia umri wake na kulinfanisha na wachezaji wengine wa umri sawa naye bila kuzingatia vigezo vya kucheza kwa mkopo timu nyingine amerudi kipindi ambacho pressure darajani ni kubwa msitegemee perfomance ikawa kubwa. Mpaka hapa tulipo amejitahidi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata Giroud/Batshuayi anaweza kumsaidia kushikilia nafasi pale anapoomia. Tunataka striker ambaye watashindana/kukimbizana kupachika mabao.

Sent using Cash Money Wings
Mkuu jifunze kumsoma mtu akili yake, ninaposema kusaidiana ina maana kubwa anapoumia mmoja tunakuwa na replacement ya level ile ile, Giroud na Bat wanaweza saidia nini hasa hapo na kwa nini wanatakiwa kuondoka!
kuchallenge ni kushindana naye hii sijaipinga
kusaidiana ni nje ya kushindana
Angalia Spurs, Kane kaumia hawana striker wa maana
Tunapokuwa na strikers wa level ya juu wanasaidiana kwa maana ya mmoja akiumia tayari tunaye mwingine mwenye uwezo wa kufunga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom