ARSENAL 1-2 CHELSEA, Premier League: Post-match reaction, ratings
By Mlanzi
Tammy Abraham na Jorge Luiz Frello Filho a.k.a Jorginho wameiangamiza Arsenal pale pale Emirates Stadium dimba lililokuwa likifahamika kama Ashburton Grove enzi zile.
Ngoja nianze na hii formation ya 3-4-3. Naweza kuwa tofauti kidogo but mfumo huu bila ya Marcos Alonso kuwepo uwanjani 3-4-3 inakuwa useless. Chelsea inakuwa toothless. Sijasema Emerson Palmieri ni mbovu hapana, lakini mfumo huo hauwezi. Kulingana na kikosi chetu 3-4-3 inahitaji tireless wingbacks kama MarcosAlonso. Marcos Alonso anapanda na kushuka kumliko Emerson Palmieri, isitoshe Marcos Alonso ni strong na ana experience. Marcos Alonso ni hatari zaidi kwenye box la wapinzani.
Kuutumia mfumo huo tunahitaji mbadala sahihi ambae ni left footed player kama Marcos Alonso. Nadhani Frank Lampard analiona hilo. Na huenda wanamfuatilia Ziyech mchezaji mwenye uwezo wa ku-unlock wale stubborn defenders. Emerson Palmieri atatuchoma sana unless tumtumie katika formation nyingine.
Chelsea tuliuanza mchezo vibaya na tulicheza ovyo dakika 30 za mwanzo kiasi cha kuruhusu bao kutoka kwa Arsenal bao lililofungwa dakika ya 13 na kudumu kipindi chote cha kwanza. Frank Lampard alibadili mfumo dakika ya 34 na kuanza kutumia 4-3-3.
Ujio wa Jorge Luiz Frello Filho a.k.a Jorginho dakika hiyo ya 34 ulibadilisha kabisa appetite ya team. Jorginho ni midfielder lakini ni kama kocha awapo uwanjani, Jorginho ni vice-captain lakini ni kama full captain awapo dimbani. Anaipanga team, anapandisha team, anahamasisha team kama sote tulivyo ona mara baada ya Frank Lampard ku change formation dakika ya 34 na kuanza kutumia 4-3-3 ambapo Jorginho alimpumzisha Emerson, alafu Cesar Azpilicueta akahamia left back, na Fikayo Tomori kuhamia right back.
Dakika chache baadae Chelsea tulitakiwa kupata penalty na Arsenal walitakiwa kuwa 10 uwanjani baada ya Guendouzi kumvuta Tammy Abraham ndani ya penalty box. Cha ajabu siyo referee wala VAR walioiona hiyo.
Juhudi za Chelsea katika second half zilikuwa nzuri especially wakati team ikitafuta equalizer goal. Kazi na temper ya mchezo ilipanda na bao la kusawazisha lilipatikana kutoka kwa Jorginho dakika ya 83 mara baada ya keeper Bernd Leno kushindwa kuokoa free kick kutoka kwa Mason Mount na mpira kumkuta Jorginho aliyekuwa katika nafasi nzuri.
Yes! Kunawatu tunadhani Jorginho hakutakiwa kuwa uwanjani baada ya kumvuta mkono Guendouzi, but Guendouzi hakupaswa kuwa uwanjani pia kabla ya hilo tukio. So perhaps tuliozoea jiji tunasema ngoma draw

!.
Chelsea tulifanikiwa kujenga momentum na counter iliyochezwa na Tammy Abraham wakiwa na Willian ilitosha sana kuwaangamiza Arsenal katika dakika ya 87 bao likifungwa na Tammy Abraham. Na mpaka dakika 90+7 zinakamilika Chelsea ilikuwa mbele kwa mabao mawili kwa moja na kuondoka ikiwa kifua mbele katika London derby
Na kwa maana hiyo Arsenal watauanza mwaka 2020 wakiwa umbali wa points 11 nyuma ya top four.
Kulikuwa na changes kadhaa kutoka katika kikosi kilichocheza Alhamisi ambapo Mateo Kovačić alirejea kutoka katika suspension na kuchukuwa mikoba ya Jorginho, huku Mason Mount akichukuwa nafasi ya Callum Hudson-Odoi katika ile front three.
Nafasi ya Fikayo Tomori ilichukuliwa na kinda Lamptey ikiwa ni debut kwa kijana huyo fresh kutoka Academy dakika 20 za lala unono. Callum Hudson-Odoi alimpumzisha Mateo Kovačić na team ikaanza kutumia formation ya 4-2-3-1.
Katika mchezo huu tumeshuhudia yellow cards tisa ikiwa ni cards nyingi zaidi katika Premier League msimu huu. Kutokana na Spurs kudondosha points mbili, Chelsea inajikita katika nafasi ya nne ikiwa mbele ya Manchester United kwa tofauti ya points nne huku Spurs ikiwa nyuma kwa tofauti ya points tano.
Next up: tutawatembelea Brighton siku ya Juma tano katika Premier League
KTBFFH
Sent using
Jamii Forums mobile app