PEP tena kilaza jamani, kwani vilaza huwa wakoje?
Kumbuka huyo kilaza huyu ndie analipwa zaidi katika ligi za Ulaya kwa mshahara wa £15.3 millioni kwa mwaka, pia kumbuka kuwa PEP ndie aliyeifumua Man City iliyokuwa kichwa cha waenda wazimu na sasa ni tishio England na Ulaya kote.
Mimi ni mfuasi mkubwa sana wa Mou lakini Mou hawezi mkuta PEP kwa creteria zote za ubora wa kocha
Mfano katika wingi wa trophies PEP yuko juu ya Mou PEP anazo kama 23 wakati Mou ni 21 tu. Kwa makombe ya kimataifa kama UEFA nk, PEP anazo 8 sawa na Furgie, Ancelotti wakati Mou anazo 4 tu hata akina Banitez-5, Zizzu-7 wamempita Mou
Winning %age
PEP ana wingning %age ya 73 wakati Mou ni 65 tu hata Zizzu wa 70% amemshinda Mou
Kwa hiyi nahitimisha kwa kusema kuwa Kocha wa Football mzuri kwa nyakati zote anaweza kuwa ni Alex Furgusson lakini kwa current coaches ni PEP Guardiola. Mou inabidi ajitahidi sana ili afikie rekodi ya PEP.
Wakati Mou ana karibu miaka 20 akifundisha soka, PEP anazo 10 tu na haya mafanikio yote kayapata ndani ya hizo miaka 10
Kwa hiyo ukipima mafanikio ya makocha kwa rate ya mwaka mmoja PEP ni wa tatu baada ya Zizzu akifuatiwa na Bob Pasley kocha wa Liverpool aliyeipa jina Liverpool hii ya leo ambayo akina King NGwaba wanaishabikia, nafikiri asingekuwa Bob hawa washabiki wa Liverpool leo wangekuwa aidha man united, arsenal au Chelsea. Mou anakuja nyuma sana akipitwa na akina Luiz Enrique na Antonio Conte