Unapoutazama Mpira Kwa Upofu Siku zote Utaendelea Kuwa Kipofu...
Kinacholeta Mashaka Ni Mpale Mshabiki Wa Chelsea anaposema "Chelsea ina Miezi Miwili tu Kwa Sarri lakini inafanya Vizuri"!!!!
Hivi Kwa Pale Uengereza Ukitoa Chelsea na Spurs Ni Timu gani Nyengine Wachezaji Wake Waliokaa Kwa Muda Mrefu na Kutengeneza Chemistry ya Muda mrefu?
Kinachowaangusha Spurs Ni Kuwa Uwekezaji wao Ni Mdogo Wanawekeza Kwa Wachezaji Wa kawaida (Average)..
Lakini Chelsea Kwa Muda Mrefu Wamewekeza Kwa Wachezaji Waliokuwa Talented hapo Mwanzoni ambao Wapo Kwenye Timu Kwa Muda Mrefu 3+ years.
Sasa Sarri ana miezi Miwili lakini Wachezaji hawana Miezi Miwili na Ndiyomana unakutia Hata Yule Kocha Wa Ndondo Conte alibebwa na Timu akachukua Kombe.
Tofauti na Timu Zetu Man United, Arsenal na Liverpool ambazo Kila Window unakutia Sura Mpya Makocha Wakihangaikia Kutengeneza Chemistry jambo ambalo Linahitaji project ya Muda mrefu.
Mkuu ukiangalia Chelsea kwa misimu mitatu/minne ivi imekuwa na wachezaji tofauti tofauti waliokaa mda mfupi na kuzoeana mapema.
Mfano kikosi kilichobeba europa, baada ya mourihno kuja alikibadilisha na baadhi ya wachezaji kama Oscar, Luiz, Ramires, Pert Cetch, na nk...waliondoka.
Mourihno akaleta Diego Costa, Matic, Willian, Qotwaa nk.. ambao ndo alichukuanao ubingwa epl. Msimu unaofata akaboronga na timu kuishia nafasi ya kumi.
Alipokuja Antonio Conte, baadh ya players waliondoka mf ivanovic, john terry, nk.. ambapo Conte alimrudisha tena David Luiz, akamleta Alonso, Kante Ngolo na Mitch Batshyuai nk.. ambao nao pia walibeba ubingwa. Msimu uliofata timu ikavurunda ambapo ndo alikuja Alvaro Morata, Rudger, Zappacosta, nk..
Msimu huu sasa chini ya Sarri ambaye amesajili mtu kma Jojinyo, Kepa, na Kovavic ...
Kwaiyo mkuu ukiangalia kikosi cha Chelsea kwa misimu kadhaa kimekuwa kikibadilika kutokana na kila kocha anayekuja, anakuja na wachezaji wake..
Ni wachezaji wachache sana wenye misimu zaid ya mitatu apo darajani mf Hazard, labda Luiz, Cahill, Moses, Azpcweta, Willian, nk ..
Tofauti na Liverpool au Tottenham au man u wachezaji weng wana misimu zaid ya mitatu.