Nini tunafeli kwa sasa Chelsea?
1. Kucheza direct football.
Hii ina maana tunacheza mpira unaosomeka kirahisi na kikubwa ni kwamba mbinu kubwa tuliobaki nayo ni kufanya substitution ya Pedro na Willian , hakuna kingine ndio maana tukikutana na mpinzani anaepaki basi inatusumbua sana.
2. Mabadiliko ya kimfumo, tambua kabisa ,mabadiliko ya kimfumo kutoka 3-4-3 kwenda 3-5-2 yanainyima timu usahihi wa kushambulia yani ukitazama utaona kabisa timu inakosa uwezo wa kufanya counter attack, mashambulizi ya kushtukiza kwa wakati.
3. Uwepo wa sesc fabrigas & bakayoko.
Binafsi timu inapohitaji kufanya fast movement inashindwa kulingana na utaratibu wa sesc, naamini sesc n mchezaji mzuri kwenye uwezo wa kucontrol game na kupiga long and short passes accurately, lakini kuna muda anahitajika asiwepo kwa manufaa ya timu.
- bakayoko bado hajiamini na hana macho mazuri ya kupiga pasi sahihi kwa washambulizi pia sipendezwi na na ukabaji wake marnyingi.
Suluhisho :
1. Drinkwater :
Muweke ndani Drinkwater na ngolo kante wacheze kama key figures za ulinzi.
2. Turudi kucheza mfumo wa zamani:
Rudisha 3-4-3 timu ishambukie sana na sio kupiga pasi nyingi katika eneo la adui.