Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Kwa hii sera ya Conte kubadilisha na kuwabadilishia namba wachezaji mimi siiaamini Che against Barca. Naona kama tukijitahidi game la kwanza ni draw. Chelsea ina wachezaji wa kuaminika kama akina Kante, Hazard na Kipa. Beki pia ni nzuri isiposumbuliwa huko mbele kwa game za hivi karibuni Morata amekuwa striker wa kawaida sana. Bakayoko ndio usiseme kabisa, Fab ni mzuri kwa mbele lakini umri unaonyesha kuwa hana pumzi tena kama yule Fab wa 2014/15 akicheza na Costa. Moses ni mzuri sana akitumiwa vizuri. Akna Willian na Pedro wanahitaji chemistry nzuri ndipo watacheza vizuri.
Natumain kwenye dirisha dogo la January Conte ataibalance timu ili iweze kushindana Championship na akna Barca
 
Bakayoko ameshindwa kuonyesha kile kilichotarajiwa kutoka kwake ingawa mchango wake kwenye timu bado ni muhimu, na Kante amemba Mfaransa huyo asaidiwe
Kiungo wa Chelsea N'Golo Kante amesema kuwa timu yake ina jukumu la kumsaidia mchezaji mwenzao Tiemoue Bakayoko anapoendelea kuzoea maisha ya Ligi Kuu Uingereza.
Mfaransa Bakayoko, anahangaika kuonyesha tofauti Chelsea tangu atue London akitokea Monaco kwa £40m, alitolewa kipindi cha pili klabu hiyo ikifungwa 1-0 na West Ham Jumamosi.

Kante, ambaye ameshinda tuzo ya PFA ya mchezaji bora wa mwaka msimu uliopita, ameitaka klabu kumsaidia Mfaransa mwenzake.
"[Bakayoko] anafanya mazoezi kwa bidii na anajitoa kikamilifu. Tunapaswa kumsaidia acheze katika ubora wake," Kante alikiambia Evening Standard.
"Je! Timu inawajibika kuweza kumsaidia kucheza katika kiwango bora? Naam. Lakini si Tiemoue pekee, kwa kila mtu. Ni budi tushirikiane kwa ajili ya mafanikio ya timu, kwa kujaribu kushinda mechi. Hilo ndilo tunalofanyia mazoezi.
Kama anahitaji ushauri, Naweza kumshauri. Lakini kama ilivyo kwenye kila klabu - jaribu kufanya mazoezi, elewa anachotaka kocha na ujitume dimbani. Ipo hivyo kila mahali."

Chelsea wataikabili Huddersfield Town Jumanne jioni wakitaka kurejea kwenye njia za ushindi baada ya kuangukia pua wikiendi.
 
Muitaliano huyo amesisitiza kuwa Ligi ya Uingereza ndiyo kipaumbele chake lakini amekiri kuwa Barcelona ni mpinzani mgumu anayehitaji nguvu kumfunga
Bosi wa Chelsea Antonio Conte amedai kuwa timu yake italazimika "kucheza kwa 120%" ili kuweza kuing'oa Barcelona Ligi ya Mabingwa hatua ya 16-Bora.
Blues wamepangwa kucheza dhidi ya miamba wa Hispania katika droo iliyofanyika Jumatatu, mechi ya kwanza ikitarajiwa kufanyika Stamford Bridge Februari 20.

Conte amesisitiza kuwa nguvu zake ameelekeza kwenye Ligi Kuu Uingereza, lakini Muitaliano huyo amekiri kuwa timu yake imepangwa dhidi ya mpinzani mgumu ambaye ni kinara wa La Liga.
"Ni lazima tuwe tayari kucheza nyumbani. Hakuna faida ya kuanzia nyumbani. Dhidi ya Barcelona ni lazima ucheze kwa 120%," Conte aliwaambia waandishi.

Kipaumbele chetu ni ligi na kubaki juu kupigania kutinga nafasi ya nne - kwa sasa. Utakapofika muda wa kuikabili Barcelona tutaanza kuifikiria mechi hiyo."
Chelsea wanataka kurejea kwenye njia za ushindi baada ya kuchezea kichapo cha 1-0 kutoka kwa West Ham United Ligi Kuu Uingereza watakapoitembelea Huddersfield Town Jumanne usiku.
 
Kwa Hiyo Unaiogopa Barcelona?

Mkuu wewe Mwanamme Bhana Usiogope Vita! Mimi Nawasupport Chelsea Muidonoe Hiyo Barcelona Coz Washabiki Wa La Liga wana Kidomodomo sana juu ya EPL.
Mbona unawashwa na timu za watu
Au kisa yako magumashi
 
Ninyi Chelsea mna gemu na Huddersfield ugenini mnakalia gemu ya february shauri yenu
 
Kikosi kizuri ila sasa tukishinda hapa kocha atadhani tumeshinda kwa sababu tumecheza na timu dhaifu. Nimipenda hiyo forward.

Hapo wakiongeza bidii, game ya Barcelona atoke Bakayoko acheze Drinkwater.

Wengine wabaki hivyohivyo....
 
Game ikifikia dakika za mwisho unamtoa mmojawapo kati ya Willian na Pedro unamweka Fabregas. Anarudi kwenye midfield tunacheza 3-5-2.
 
Bacelona kwa chelsea ni sawa na mtori kwa mgonjwa huyu barca ajiandae kwa mvua ya magoli
 
Kikosi kizuri ila sasa tukishinda hapa kocha atadhani tumeshinda kwa sababu tumecheza na timu dhaifu. Nimipenda hiyo forward.

Hapo wakiongeza bidii, game ya Barcelona atoke Bakayoko acheze Drinkwater.

Wengine wabaki hivyohivyo....


Leo Munalazwa nyie! Trust me.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom