Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

17bb9d4a64ed42fb2421b4440529785a.jpg
 
Wachezaji kuwakataa pamoja na kucheza UCL kunaashiria nini? Yaani mchezaji anaona bora abaki Everton kuliko kuja darajani, kweli??? Yaani mchezaji anaona bora aende Loserpool kuliko kuja kwenu, kweli??? Hii sio ishara nzuri hata kidogo blauzi fans.
 
Sijui mnakiona ninachokiona mimi. ila mtakiona katika michezo ijayo. Kama Drinkwater akipona na akawa fiti 100% basi Chelsea eneo la katikati litakuwa kama eneo la ufalme..... Muunganiko wa wanadamu hawa sina shaka na aina ya uchezaji wao, shaka yangu ni namna Bakayoko atakavyotakiwa kutumia nguvu kubwa kuvunja muunganiko huu.... Wamecheza pamoja Msimu mzima, wametesa viungo wa upinzani pamoja, wameshinda pamoja, wamechukua ubingwa pamoja na sasa wamerudiana na kuamua kucheza pamoja...

Bakayoko ni bora sana kuliko Dany Drinkwater ila muunganiko wa Kante na Drinkwater ni muunganiko matata sana kuliko wa Kante na Bakayoko.... Kama Conte ataruhusu muungano basi kazi kubwa ya sifa itakuwepo, ila kama hata ruhusa muungano basi kazi ndogo ya matusi itakuwepo.....
66d83d7f2f7ba44dd68fb476e0bb2c56.jpg
 
Kutoa pesa nyingi hakumaanishi mchezaji hawezi kuwa garasa, na uzuri Chelsea tuna rekodi nzuri katika kulipa hela nyingi kwa magarasa, kwa hiyo kama Garasa hili limetupita pembeni kwetu ni habari njema

Sizitaki mbichi hizi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom