Chelsea is leading by 1 goal scored by Anelka... Dakika ya 14 inakwenda hiyo
RESULTS:
CHAMPIONS ... Chelsea players celebrate their Premier League title triumph
MAJUMUISHO
Hongera Chelsea kwa USHINDI - Pamoja na Matatizo yote ya kuwakosa wachezaji wenu Mastaa kwa nyakati tofaut eg. Michael Essien, Bosingwa, John Cole, Ashley Cole lakini mmeonyesha bidii na kiu kubwa. Naweza sema kutolewa UEFA na Inter pia kumeshangia chachu ya ushindi wenu - Binafsi baada ya game ya Liverpool ilipoisha kwa ushindi basi nikajua sasa inaenda kwenye double for the first time in the history of this Club.
Hongera pia kwa kuwa club ya kwanza kufuga magoli mengi (103) tangu mashindano haya yaanzishwe pia Hongera kwa kukaribia kuweka Club history kwa kushinda Double endapo mtawafunga porthmouth kwenye Fainali ya FA jmosi.
Kipindi cha msimu kilivyoanza tuliona tactics safi ya Diamond Midfield, mfumo ambao ni mgumu kuucheza na kuufundisha lakini ukieleweka huwa ni wa kuvutia sana ambapo Essien, Belletti, Ballack, Lampard, Obi na Deco wote wakibadilishana kwa nyakati tofauti kutokana na choice ya kocha - Tulidorora baada ya Essien na Deco kuumia na tukapoteza game kadhaa ndipo kocha akabadili tena na kucheza wings na striker mmoja na wachezaji wawili pembeni yaani Anelka or Kalu kulia, Marouda or J.cole Kushoto na Didieee Kati ndipo tukaanza kuona vipigo mfululizo ya 4, 7 na 8 cha jana.
Kuumia kwa Ashley cole naweza kusema kulidhoofisha defence ya Chelsea katika game ya UEFA na inter, endapo angekuwa mzima basi tungeongea mengine, katika game ya marudiano pia Yury Zhirkov (wingi ambaye anaweza cheza beki wa kushoto) pia Akaumia kwa hiyo tukacheza na Malouda, hapo ikawa tatizo kwetu kuchangia kichapo cha 1-0 toka kwa Josee tukiwa darajani.
Binafsi Kikosi cha chelsea kimekamika sana idara zote kwa sasa, tunategemea kuwa na Bosingwa na Essien fiti msimu ujao kwa hiyo hatuhitaji major Transfer next season may be one or two - Aguerro kama atatua Darajani itakuwa big boost sababu tunahitaji mchezaji kwenye kipaji cha pekee.
Kawaida Chelsea haina wapenzi wengi, binafsi najipongeza kwanza kuwa mshabiki wa timu ya darajani -na washabiki wenzangu wa Chelsea wote. Kinachonifurahisha zaidi ni uongozi wa club yenye uchu wa ushindi - Roman ni mtu kwenye nia ya ushindi, shabiki number 1 wa Chelsea, Mwepesi kuchukua maamuzi magumu kwake tatizo la contract huwa halipo akiamua kumfukuza kocha kwa manufaa ya timu basi anafanya hivyo mara moja. Kumbukeni baada ya kichapo na inter ilibidi baada ya game aende dressing room kuwaambia wachezaji - Ninyi ni wachezaji wazuri au Ninyi ni wachezaji mnaolipwa vizuri" kisha akaondoka.
Hongera sana INVISIBLE, hongera pia kutuhabalisha live game ya jana, mimi nilikuwa offline kwa JF lakini nilishangilia sana hasa goli la kichwa la didieeeeee -
We look forward for FA CUP on sat to wind up this season with the DOUBLE.