CHADEMA mnatuchanganya. Tunataka Katiba inayosimamia haki na sio Katiba Mpya. Kamwe Katiba hiyo haiwezi kutengenezwa na Wanasiasa

William Mshumbusi

JF-Expert Member
Mar 27, 2012
1,657
2,252
Kitu wapinzani wanachofeli ni kuongozwa na hasira na ushindani na kupigania maslahi binafsi ya kisiasa hivyo kukosa logic na plan nzuri kufanikisha mipango yao.

Jakaya Kikwete alianzisha mchakato wa Katiba mpya Ila mchakato mzima katika mazingira hayo ulitawaliwa na wanasiasa. Bunge lilijaa wanasiasa na kwa maamuzi yao lingeleta katiba mbovu Tena iliyoegemea kuibeba CCM kwani walikuwa wengi na wenye nguvu ya maamuzi. Wangekuja na katiba mpya lkn isiyofaa. Jk alijua akaitupilia mbali mwishoni.

Sasa mnavyoomba tuimalizie mchakato mnataka tuimalizie kwa staili hiyo hiyo?!

Je, mnataka katiba mpya au katiba nzuri?

Mi nadhani kwa busara CHADEMA ombeni tume huru na chaguzi za haki. Piganieni mabadiliko hayo ya Sheria na katiba Ila swala la katiba liacheni. Waacheni watu wasio wanasiasa watuundie katiba.

*Katiba itakayowasimamia na kuwawajibisha wanasiasa pia. Katiba hiyo wanasiasa hawawezi kuiunda.

*Katiba itakayojibu kila kitu na kuondoa mizengwe kwenye kila sekta kuanzia kilimo, biashara, Viwanda, madini na Mikataba yote isiyo ya kiusalama Kama madini na manunuzi, ubia, hesabu za taasisii na mashirika ya umma kuwa wazi kwa umma wakati wote.

*Katiba itakayomlazimisha mbunge kabla ya kwenda bungeni kwenye kikao chochote akae vikao vyenye maandishi angalau vitatu na wadau wote katika Jimbo lake na kuikusanya mawazo na Kisha kuyafikisha bungeni au serikalini na sio Sasa wabunge kwenda kuzungumza mawazo binafsi na marafiki zao wachache wanaokunywa nao bia vijiweni.

Bunge jipya la katiba lisizidi 10% ya wanasiasa. Waingie wakulima, wafugaji, wafanyabiashara, bunge lijae wataalamu kwa 30% mfano walimu, madaktari, wanasheria na wachumi. Na wanaoshiriki kwenye bunge Hilo wakubali kutokugombea au kuteuliwa nafasi yoyote ya kisiasa au za kiuteuzi kwa miaka kumi ili kuondoa bunge Hilo Hilo kuja kugeuka chombo Cha utawala Mara baada ya kuunda katiba.

Bunge lililopita na mchakato mzima wa Katiba ndio uliowaibua akina polepole na Kabudi. Watu watashindwa kutoa mawazo kwa Uhuru wakitarajia hisani za watawala

Na nawaomba wimbo isiwe katiba mpya Bali tunataka katiba yenye kulinda haki. Na katiba yenye kutenda haki kamwe haiwezi kuletwa na wanasiasa. Kila sehemu wanasiasa huvutana tu kutafuta msindi. Kwenye katiba lazima kila mtu awe msindi.
 
Miye wapinzani wa inchi hii nishawadharau wapo kupigania maslahi yao wameona mama Samia anaupiga mwingi wanakuja na hoja ya Katiba mpya mama kawambia sawa Ila tulieni wao hawataki wanataka mama afanye waanavyotaka

MY TAKE

Mmaa usiwachekee hawa watakuzoea vibaya tena usiwachekee kabisa wanyooshe maana wanakosa adabu si unaona kwa mwendazake aliwaonyoosha mpaka wakakimbia nchi maaana walijua jamaaa hatanij
 
Miye wapinzani wa inchi hii nishawadharau wapo kupigania maslahi yao wameona mama Samia anaupiga mwingi wanakuja na hoja ya Katiba mpya mama kawambia sawa Ila tulieni wao hawataki wanataka mama afanye waanavyotaka...
Ndio maana hayati JPM hakucheka na HAO JAMAA.

JPM alikuwa na maono....ni kweli vyama vingi vya UPINZANI BARANI AFRIKA viko kwa ajili ya kuchelewesha tu MAENDELEO, viko kuchochea UHASAMA...UTENGANO, VURUGU.

Vyama vingi vya Afrika viko kuona kila SERIKALI iliyoko madarakani INASHINDWA NA KUANGUKA hata Kama INAFANYA VYEMA....ni siasa mahsusi za "domokrasia" zilizoasisiwa KULETA SINTOFAHAMU HUMU AFRIKA.

Nitapingwa sana kwa kusema hayo....ila ukichunguza utamaizi kuwa kuna ukweli angalau 51%.

#MamaSSHAnaupiga MWINGI
 
Huu ndo ukweli ninaouamini siku zote. Chadema ikiingia madarakani hawawez kubadilisha katiba kwani itawabeba.

Wananchi tunataka uchumi mzuri, ajira, miundombinu ma uwekezaji na afya njema. Hivyo vikilatikana mengne yatafuata. Tatzo Chadema wanataka watimiziwe wao huju sisi tykiumia. Jiwe katunyoosha jaman watuache kidogo mama atupe neema wananchi. Haya mambo wanayoyataka sio kipaumbele chetu.
 
Yaani DEMOKRASIA ya kiliberali 100% ya UJERUMANI na MAREKANI unaileta kwa WANDENGEREKO ,WAMATUMBI NA WANYAMWEZI? Khaaa 🤣🤣

Nchi hii ni ya UJAMAA WA KIAFRIKA. Chadema wasijisahaulishe. Kwanza chama chao hakiendani na MISINGI YA KUASISIWA HILI TAIFA, afadhali hata ya ACT WAZALENDO.

Wamekosa hoja, wanadandia KATIBA MPYA.

Hayati JPM aliwashinda katika hoja ya UFISADI walioipambania miaka tele, wakahamia katika "DEMOKRASIA NA MIKUTANO YA HADHARA NA MAANDAMANO" 🤣🤣🤣🤣
 
Ndio maana hayati JPM hakucheka na HAO JAMAA....

JPM alikuwa na maono....ni kweli vyama vingi vya UPINZANI BARANI AFRIKA viko kwa ajili ya kuchelewesha tu MAENDELEO....viko kuchochea UHASAMA...UTENGANO....VURUGU...
Yani mama apite mule mule kwa magu maana wanakosa adabu kwa hizi siku Mia za mama tumeona angalu vitu vinaanza kurudi kwenye mstari

Mwakani Kuna sensa unaitaji pesa, haya mchakato wa Katiba mpya unaitaji pesa mama anawambia uchumi wetu haupo sawa subilieni, wapi wao tunataka Katiba mpya

Haya akifanya ambayo wanayasema baada waseme sawa mama wanaanza mzodoa yani hawana wema so mama awanyooshe
 
Yani mama apite mule mule kwa magu maana wanakosa adabu kwa hizi siku Mia za mama tumeona angalu vitu vinaanza kurudi kwenye mstari

Mwakani Kuna sensa unaitaji pesa, haya mchakato wa Katiba mpya unaitaji pesa mama anawambia uchumi wetu haupo sawa subilieni, wapi wao tunataka Katiba mpya

Haya akifanya ambayo wanayasema baada waseme sawa mama wanaanza mzodoa yani hawana wema so mama awanyooshe
Hizi nchi za KIAFRIKA wakati mwingine zinahitaji misimamo kama ya watu aina ya hayati Magufuli.....

Mama SSH ni rais Bora mno....wanataka tu kumfelisha....hao jamaa hawana jema....kwao hayati JPM alikuwa mbaya....mama naye mbaya....yaani jamaa HOPELESS sana Khaaa 🤣🤣🤣
 
Kama si mh.Rais SSH hivi Hawa akina MDUDE NYAGALI wangetoka RUMANDE?

Kama si mh.Rais SSH hivi masheikh wa UAMSHO wangetoka RUMANDE?

Mungu ana funzo kubwa sana kwetu WATANZANIA.

Alimleta madarakani HAYATI JPM kuwa kama "REDEEMER".....JPM alikuwa FUNZO kwa makosa TULIYOFANYA ili tujirekebishe....baadaye akamleta Mh.Rais SSH....kwanza mwanamama....pili MPOLE NA MSIKIVU HASA kama lilivyo jina lake....hakika ni FUNZO NA ZAWADI KWETU WATANZANIA WENYE KUTAFAKARI....WENYE KUTAFAKARI....WENYE KUTAFAKARI.

Chadema wanataka kuiyumbisha NCHI....hawana lolote.....wana hadaa tu za KISIASA.

JPM mwamba,Mama SSH Mwamba!

#KaziInaendelea
#StaunchSupporterOfSSH
 
Ni lini wamesema Mama ni mbaya?
Wao wanajua.
Kuleta suala la katiba mpya hasa kipindi hiki cha mdororo wa uchumi wa nchi ni kutaka tu MIGONGANO na dola.

Tusisahau pia hiyo dola iliyo chini ya CCM, Katiba mpya si KIPAUMBELE CHAKE.

KATIBA MPYA ni KIPAUMBELE cha makundi ya wanasiasa na NGO's ambazo wao ni lazima wapiganiye hayo kama MATAKWA YA WAHISANI WAO, bila ya hayo FEDHA HAZILETWI KWAO huo ndio ukweli ambao wengi hawataki KUUSIKIA.
 
Chadema wanajisahaulisha kuwa TANZANIA ni nchi ya KIJAMAA...UJAMAA WA KIAFRIKA...na si ULIBERALI anaotuhadaa nao TUNDU LISSU.....

Tanzania si KENYA....na haitokaa iwe kama KENYA.....

Misingi ya UASISI wa taifa hili imeo ekana kama INAWACHELEWESHA baadhi ya "watu".....ila ndiyo INAYOLINDA AMANI....UMOJA WETU.....na UTU WETU....

Upekee wa WATANZANIA huupati popote pale....

Kenya imejaa UKABILA....
Kongo imejaa VURUGU....
Uganda nchi ya "KIJESHI"....
Burundi Kama "ilivyo".....
Rwanda Kama "ilivyo".....
Msumbiji uhasama na "UGAIDI"....
Ethiopia Kama "ilivyo"........
Somalia "ubaguzi wa KOO ,UGAIDI ,tabu tupu tabu tabu tupu"....
Nigeria UFISADI ULIOTOPEA ,UKABILA ,UGAIDI...tabu tupu tabu tupu"

KILA NCHI ni afadhi ya NYINGINE....

TANZANIA PEKEE ITABAKI NA UPEKEE WA AJABU......

TUENDELEE KUENZI TUNU ZETU KWA KUIUNGA MKONO CCM....

#ChadoomoWababaifu
#KaziIendelee
 
Mi nadhani kwa busara CHADEMA ombeni tume huru na chaguzi za haki.
Ushauri wako huu baki nao. Huwezi kuomba kuomba uji halafu ukaletewa kwenye kopo la chooni ukanywa. Tunataka uji lkn kwenye kikombe safi

Kopo la chooni =katba ya 1977.
Uji. =. Tume huru.
Kikombe = katiba mpya.
.
 
Wao wanajua....
Kuleta suala la katiba mpya hasa kipindi hiki cha mdororo wa uchumi wa nchi ni kutaka tu MIGONGANO na dola.....

Tusisahau pia hiyo dola iliyo chini ya CCM ,Katiba mpya si KIPAUMBELE CHAKE.....

KATIBA MPYA ni KIPAUMBELE cha makundi ya wanasiasa....na NGO's ambazo wao ni lazima wapiganiye hayo kama MATAKWA YA WAHISANI WAO....bila ya hayo FEDHA HAZILETWI KWAO...huo ndio ukweli ambao wengi hawataki KUUSIKIA.....
Hakuna binadamu ulimwenguni humu ambaye anaishi bila mfumo wa siasa. Bahati mbaya kuna watu mmekaririshwa kwamba siasa ni kwa ajili ya kundi fulani la watu wanaoitwa wanasiasa
 
Ushauri wako huu baki nao. Huwezi kuomba kuomba uji halafu ukaletewa kwenye kopo la chooni ukanywa. Tunataka uji lkn kwenye kikombe safi

Kopo la chooni =katba ya 1977.
Uji. =. Tume huru.
Kikombe = katiba mpya.
.
Shida huwa hamsomi hoja vizuri. Mnakimbilia kwenye ushabiki.

Kwa mchakato upi tunaweza kupata Katiba inayofaa!? Ule ule wa Jk?! Ule ule uliojaa wanasiasa.

Lazma ngeuze azma yenu kutokea kwenye Katiba mpya na kwenda kwenye tume na chaguzi huru na chaguzi za haki la Katiba likianza Sasa litatuletea Katiba isiyofaaa.
 
Hakuna binadamu ulimwenguni humu ambaye anaishi bila mfumo wa siasa. Bahati mbaya kuna watu mmekaririshwa kwamba siasa ni kwa ajili ya kundi fulani la watu wanaoitwa wanasiasa
Elewa hoja. Sijawabeza wanasiasa ata kidogo kwenye kumsukuma Hilo. Ila nachopinga NI wanasiasa kiutawala mchakato wake mzima. Kwanza hawataafikiana na Pili watajadili maswala ya kiuchaguzi tu na kuacha maeneo mengi nyeti. Wawepo Ila wasitawale mchakato
 
Ndio maana hayati JPM hakucheka na HAO JAMAA....

JPM alikuwa na maono....ni kweli vyama vingi vya UPINZANI BARANI AFRIKA viko kwa ajili ya kuchelewesha tu MAENDELEO....viko kuchochea UHASAMA...UTENGANO....VURUGU....

Vyama vingi vya Afrika viko kuona kila SERIKALI iliyoko madarakani INASHINDWA NA KUANGUKA hata Kama INAFANYA VYEMA....ni siasa mahsusi za "domokrasia" zilizoasisiwa KULETA SINTOFAHAMU HUMU AFRIKA...

Nitapingwa sana kwa kusema hayo....ila ukichunguza utamaizi kuwa kuna ukweli angalau 51%.....

#MamaSSHAnaupiga MWINGI
Utakuta na wewe ni mkuu wa wilaya au hata nasary kada mpya unatetea ugali dah tuna safali ndefu sana kufika tutakapo kama taifa
 
Back
Top Bottom