Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 62,510
- 104,783
Sidhani kama hata kwa katiba hii kama ilivyo leo kama kusingekuwa na wizi wa kura mambo yangeharibika kama yalivyoharibika sasa. Tatizo linaweza kuwa katiba ila tatizo kubwa zaidi ni jinsi katiba hiyo inavyofatwa.Kama nimekuelewa vizuri ni kwa nini ASP walipinga ushindi ambao upo kikatiba?
Hili ukiunganisha na hali iliyopo Sasa Tanzania utawaelewa CHADEMA kugomea uchaguzi wa 2025.
Katiba ni ramani ya nchi, kama Katiba haipo sawa nchi pia haiwezi kuwa sawa.
Pamoja na hayo hakukuwa na malalamiko ya katiba kutoka kwa ASP kabla ya mapinduzi, ASP hawasemi kama walishinda uchaguzi halafu wakanyang'anywa viti vya ubunge au walizuiwa kushiriki uchaguzi. Masuala yao hayafanani na ya CHADEMA ya sasa.